Jumapili, 26 Shawwal 1445 | 2024/05/05
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

[سُبْحَانَ الَّذِي أَسْرَى بِعَبْدِهِ لَيْلاً مِنَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ إِلَى الْمَسْجِدِ الْأَقْصَى الَّذِي بَارَكْنَا حَوْلَهُ لِنُرِيَهُ مِنْ آيَاتِنَا إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ]

“SUBHANA, Ametakasika aliye mchukua mja wake usiku mmoja kutoka Msikiti Mtukufu mpaka Msikiti wa Mbali, ambao tumevibariki vilivyo uzunguka, ili tumuonyeshe baadhi ya Ishara zetu. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia na Mwenye kuona.” [Al-Isra’: 1]
(Imetafsiriwa)

Safari ya Usiku na Kupaa, Al-Isra’ Wal Mi’raj, ni muujiza mkubwa ambapo Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), aliona moja ya alama kuu za Mola wake. Ambapo milango ya Bait al-Maqdis na milango ya mbinguni ilifunguliwa kwa ajili yake baada ya kukata tamaa na watu wa Makka na Taif.

Hivyo, ilikuwa ni thibitisho na bishara njema kwa Waumini. Kisha ikateremshwa Sura Al-Isra kuhusiana na qadhaa ya Mwenyezi Mungu juu ya Bani Israil na ufisadi wao, Mwenyezi Mungu (swt) asema.

[وَقَضَيْنَا إِلَى بَنِي إِسْرَائِيلَ فِي الْكِتَابِ لَتُفْسِدُنَّ فِي الْأَرْضِ مَرَّتَيْنِ وَلَتَعْلُنَّ عُلُوّاً كَبِيراً]

“Na tukawahukumia Wana wa Israili katika Kitabu kwamba: Hakika nyinyi mtafanya fisadi katika nchi mara mbili, na kwa yakini mtapanda kiburi, kiburi kikubwa.” [Al-Isra’: 4]

Fungamano hili la busara baina ya Msikiti wa Al-Haram, Msikiti wa Al-Aqsa, na ufisadi wa Bani Israil katika ardhi hii, ni ujumbe wa onyo kwa Wana wa Israil na bishara njema kwa umma bora ulioletwa kwa ajili ya wanadamu.

Enyi Watu: Bani Israil wamevuka mipaka katika ardhi na wakawa na kiburi cha hali ya juu katika ufisadi wao, mpaka ufisadi wao ukaiathiri ardhi yote, sio Al-Quds peke yake. Mumeona huzuni na dharau zao kwa watu. Wanawatazama watu kwa dharau ya kuchukiza. Bali wao wanawaona kuwa ni duni kuliko wanyama, na wanadhani kuwa kutoa msaada na ulinzi kwao ni haki ambayo nchi za dunia ni lazima ziitimize, na haya ndiyo aliyoyataja Mwenyezi Mungu (swt) kuwahusu:

[وَقَالَتِ الْيَهُودُ وَالنَّصَارَى ‌نَحْنُ ‌أَبْنَاءُ ‌اللهِ وَأَحِبَّاؤُهُ] “Na Mayahudi na Wakristo wanasema: Sisi ni wana wa Mwenyezi Mungu na vipenzi vyake.” [Al-Ma’idah: 18] Bali, walimtusi Mwenyezi Mungu (swt):

[وَقَالَتِ الْيَهُودُ يَدُ اللهِ ‌مَغْلُولَةٌ غُلَّتْ أَيْدِيهِمْ وَلُعِنُوا بِمَا قَالُوا] “Na Mayahudi walisema: Mkono wa Mwenyezi Mungu umefumba. Mikono yao ndiyo iliyo fumba, na wamelaaniwa kwa sababu ya waliyo yasema.” [Al-Ma’idah: 64]

[لَقَدْ سَمِعَ اللهُ قَوْلَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللهَ ‌فَقِيرٌ وَنَحْنُ أَغْنِيَاءُ سَنَكْتُبُ مَا قَالُوا وَقَتْلَهُمُ الْأَنْبِيَاءَ بِغَيْرِ حَقٍّ]

“Mwenyezi Mungu amekwisha sikia kauli ya walio sema: Mwenyezi Mungu ni masikini, na sisi ni matajiri. Tumeyaandika waliyo yasema, na pia kuwauwa kwao Manabii bila ya haki” [Aal-i-Imran: 181] Je, kuna watu wakubwa katika uhalifu na ufisadi kuliko wauaji wa Mitume?! Mwenyezi Mungu awalaani! Wanawezaje kupotoka kutoka kwenye ukweli?

Wao ndio vinara wa riba, rushwa, kununua watu, uzinzi, ponografia, ushoga, uwongo na uzushi. Ametakasika Mwenyezi Mungu Mtukufu. Mnapofuatilia ufisadi huu, mtawakuta wale “waliomkasirisha Mwenyezi Mungu’ wanatangulia mbele kuwa wa kwanza kuyatekeleza na kuharakisha kuyasambaza kwa watu, mpaka dunia nzima imeanza kuteseka kutokana na ufisadi huu. Zikiwemo nchi za Magharibi kwa njia ya mbaya sana, na huu ndio uhalisia wao katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu:

[سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ أَكَّالُونَ لِلسُّحْتِ] “Hao ni wasikilizaji kwa ajili ya kusema uwongo, na ni walaji mno vya haramu!” [Al-Ma’idah: 42]

[وَيَسْعَوْنَ فِي الْأَرْضِ فَسَاداً] “...na wakawania kufanya uchafuzi katika nchi” [Al-Ma’idah: 33].

Umbile la Kiyahudi limezidisha ufisadi wake na kudhihirisha ukali wa uadui wake katika vita vya maangamizi ambavyo vimeendelea kwa zaidi ya miezi minne katika Ardhi Iliyobarikiwa. Wamefanya maafa makubwa, wakaua wanawake na watoto, wakazuia chakula na vinywaji, wakabomoa nyumba, misikiti, makanisa, shule, vyuo vikuu na hospitali, wakaharibu vituo vya umma na barabara, na kukata mawasiliano. Wamewalenga wafanyikazi wa matibabu na vyombo vya habari katika mandhari ya uhalifu ya kutisha ambapo walikiuka matukufu, sheria, desturi, na maadili ya kibinadamu na ya kiakhlaqi, na uhalifu huu ulipeperushwa kwa ulimwengu katika matangazo ya moja kwa moja! Na kuwadhalilisha Waislamu, na kuzikanyaga kanyaga sheria na desturi zote za kimataifa.

Enyi Waislamu: Uhalisia wa watawala wenu vibaraka, na uhalisia wa nchi za Magharibi na taasisi zao za kihalifu, umedhihirika kwenu. Mnajua kuwa yaliyokusibu na yanayokutokeeni ya mauaji, kugawanya, kudhalilishwa, na kupora mali yasingekupateni chini ya Uislamu na mamlaka ya Uislamu. Kutokuwepo hukmu kwa yale yote aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu kumekufanyeni muwe wanyonge. Watawala madhalimu ni walinzi waaminifu wa Mayahudi na nchi za Magharibi, kwani walizifungua nchi za Kiislamu kwa ajili ya maadui wa Uislamu, wafanye uharibifu na kuupora mpaka riba ikawa inabisha hodi kwenye kila mlango na uzinzi uko mbele ya kila jicho. Wameyafunga minyororo majeshi ya Waislamu na kuyafisidi ili yawe walinzi wa viti vyao vya enzi na mipaka, sio majeshi ya kivita ambayo yanamtisha adui, kuhami fahari ya Ummah, na kuhifadhi Uislamu.

Angalieni hali yenu, enyi Waislamu, “wale waliokasirikiwa na Mwenyezi Mungu” wanaunajisi Msikiti wa Al-Aqsa asubuhi na jioni, na wanaendelea kukuueni na kukudhalilisheni, na huku usambazaji wa silaha na chakula ukiwafikia kutoka katika nchi za Waislamu, na badali yake, tawala za wahaini, zikiongozwa na tawala za Jordan na Misri, zakaza mshiko wao kwa watu, kuizingira Ardhi Iliyobarikiwa na kuzuia mahitaji ya kimsingi yasiwafikie isipokuwa yale ambayo Mayahudi wanayaruhusu. Tazameni Ash-Sham na Iraq na yaliyowapata, na kwa Sudan na Somalia na yaliyowasibu, na Libya, Yemen, Hijaz, Kinana (Misri), Pakistan, Turkestan, Kashmir, Burma... n.k. Nchi zote za Waislamu zinateseka chini ya kila aina ya udhalilifu. Umaskini, ukandamizi, dhulma na uimla.

Enyi Waislamu: Je, haujafika wakati kwenu kuanza mapinduzi ambayo ndani yake mtakata mizizi ya ukafiri na watawala madhalimu kutoka nchi za Waislamu?

Je, sio wakati sasa wa nyinyi kutambua kwamba kimya chenu juu ya tawala za wasaliti kwa kuhofia maisha yenu na mali zenu imekusababishieni hasara kubwa sana katika upande wa damu yenu, heshima yenu, mali zenu na utu wenu?!

Je! haujafika wakati wa nyinyi kuona kwamba uhai wenu, na wokovu wenu, na kumridhisha Mola wenu ni katika kumuitikia Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Ili nyote muinuke kupindua viti vya wahaini na kuziunganisha nchi za Waislamu chini ya mtu mmoja anayemuamini Mwenyezi Mungu na anayeiogopa Siku ya Mwisho?!

Enyi Ummah wa mashahidi kwa wanadamu...Enyi Umma wa Muhammad (saw):

Wajibu wenu kwa Uislamu unawajibisha kuinuka katika Dini ya Mwenyezi Mungu kwa utukufu, bila kuogopa lawama ya mwenye kulaumu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Inakuwajibisheni kuwahutubia watoto wenu katika jeshi ili watekeleze wajibu wao kwa Dini yao, Ummah wao, na Masra ya Mtume wao.

Jukumu lenu kwa ulimwengu ni jukumu kubwa la kuutoa katika giza la ubepari na ukandamizaji wake hadi kwenye nuru na uadilifu wa Uislamu, na mtaulizwa kuhusu hilo siku ya kuwasilishwa mbele ya Mwenyezi Mungu (swt). Hili linahitaji nguvu za Umma wa Kiislamu kufanya kazi kwa nguvu zao zote ili kusimamisha Dini ya Mwenyezi Mungu duniani, kupindua tawala dhalimu, na kuunganisha Ummah chini ya bendera moja.

Umma wa Muhammad (saw), ni Ummah uliochaguliwa na Mwenyezi Mungu (swt) ili kusimamisha Dini Yake na kubeba Wahyi na ujumbe Wake kwa watu wote. Kwa fadhila hii ulistahiki hadhi ya mitume na manabii kutoka miongoni mwa watu wao, hivyo ukawa ni mashahidi kwa watu, na maneno ya Mwenyezi Mungu (swt) yanakutoshelezeni katika hili:

[وَجَاهِدُوا فِي اللهِ حَقَّ جِهَادِهِ هُوَ اجْتَبَاكُمْ وَمَا جَعَلَ عَلَيْكُمْ فِي الدِّينِ مِنْ حَرَجٍ مِلَّةَ أَبِيكُمْ إِبْرَاهِيمَ هُوَ سَمَّاكُمُ الْمُسْلِمِينَ مِنْ قَبْلُ وَفِي هَذَا لِيَكُونَ الرَّسُولُ شَهِيداً عَلَيْكُمْ وَتَكُونُوا ‌شُهَدَاءَ ‌عَلَى النَّاسِ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَاعْتَصِمُوا بِاللهِ هُوَ مَوْلَاكُمْ فَنِعْمَ الْمَوْلَى وَنِعْمَ النَّصِيرُ]

“Na fanyeni juhudi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kama inavyo stahiki jihadi yake. Yeye amekuteueni. Wala hakuweka juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila ya baba yenu Ibrahim. Yeye (Mwenyezi Mungu) alikuiteni Waislamu tangu zamani, na katika hii (Qur'ani) pia, ili awe Mtume shahidi juu yenu, na nyinyi muwe mashahidi kwa watu. Basi shikeni Sala na toeni Zaka na shikamaneni na Mwenyezi Mungu. Yeye ndiye Mlinzi wenu, Mlinzi bora kabisa, na Msaidizi bora kabisa.” [Al-Hajj: 78].

Kwa kumalizia: Hili ndilo tulilotaka kuuhutubia Ummah wetu kwalo katika kumbukumbu ya Al-Isra' Wal Mi'raj na siku ya kuvunjwa kwa Khilafah, tukikumbusheni Surat Al-Isra, na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) akiwaongoza Mitume katika Swala katika Msikiti wa Al-Aqsa, ambao una bishara njema na dalili ya utawala wa Uislamu juu ya kila kitu chengine, na kwamba nafasi ya Umma wa Kiislamu ni nafasi ya uimamu na uongozi. Pia kukumbusheni juu ya wajibu wenu kwa Uislamu na watu wote, na kuyataka majeshi yenu yatekeleze wajibu wao katika kumnusuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kuandamana hadi Al-Quds, kwa kuiletea utukufu na ukombozi, mahali pa kutua Khilafah ambayo itaijaza ardhi usawa na uadilifu, Mwenyezi Mungu akipenda.

Sisi katika Hizb ut Tahrir tunatazamia ushindi wa Mwenyezi Mungu na Khilafah Rashida kwa njia ya Utume ambayo itapanga upya mahusiano ya kimataifa kwa msingi mmoja, ambao ni kuueneza Uislamu hadi ufikie kule ambako usiku na mchana unafika, katika uthibitisho wa yale ambayo Al-Bayhaqi na wengineo walivyosimulia kwa upokezi ulio sahihi kutoka kwa Tamim Al-Dari, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, ambaye amesema: Nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) akisema:

«لَيَبْلُغَنَّ هَذَا الْأَمْرُ مَا بَلَغَ اللَّيْلُ وَالنَّهَارُ، وَلَا يَتْرُكُ اللهُ بَيْتَ مَدَرٍ وَلَا وَبَرٍ إِلَّا أَدْخَلَهُ اللهُ هَذَا الدِّينَ بِعِزِّ عَزِيزٍ أَوْ بِذُلِّ ذَلِيلٍ، عِزّاً يُعِزُّ اللهُ بِهِ الْإِسْلَامَ، وَذُلّاً يُذِلُّ اللهُ بِهِ الْكُفْرَ»

“Kwa yakini jambo hili litafika kule ambako usiku na mchana unafika. Na Mwenyezi Mungu hataacha nyumba wala makaazi isipokuwa Mwenyezi Mungu aitaingiza Dini hii kwa izza ya mwenye izza au kwa udhalilifu wa mdhalilifu. Kwa izza ambayo Mwenyezi Mungu ataupa Uislamu, na udhalilifu ambao Mwenyezi Mungu ataudhalilisha ukafiri.”

Hatimaye, tafakarini maneno ya Mwenyezi Mungu (swt):

[وَقُلْنَا مِنْ بَعْدِهِ لِبَنِي إِسْرَائِيلَ اسْكُنُوا الْأَرْضَ فَإِذَا جَاءَ وَعْدُ الْآخِرَةِ جِئْنَا بِكُمْ لَفِيفاً * وَبِالْحَقِّ أَنْزَلْنَاهُ وَبِالْحَقِّ نَزَلَ وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا مُبَشِّراً وَنَذِيراً]

“Na tukawaambia baada yake Wana wa Israili: Kaeni katika nchi. Itapo kuja ahadi ya Akhera tutakuleteni nyote pamoja. * Na kwa Haki tumeiteremsha, na kwa Haki imeteremka. Na hatukukutuma ila uwe mbashiri na mwonyaji.” [Al-Isra’: 104-105].

H. 27 Rajab 1445
M. : Alhamisi, 08 Februari 2024

Hizb-ut-Tahrir
Ardhi ya Baraka-Palestina

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu