Jumapili, 11 Dhu al-Qi'dah 1445 | 2024/05/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Iraq

H.  9 Muharram 1444 Na: 1444 / 01
M.  Jumapili, 07 Agosti 2022

 Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi
(Imetafsiriwa)

(وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ الَّذِينَ إِذَا أَصَابَتْهُمْ مُصِيبَةٌ قَالُوا إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ)

“Na wabashirie wanao subiri * Wale ambao ukiwasibu msiba husema: Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea.” [Al-Baqarah :155-156]

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Iraq inatoa rambirambi zake za dhati kwa familia ya marehemu mheshimiwa Ndugu Khader Issa Al-Jubouri, aliyefariki mnamo Jumapili jioni, tarehe 9 Muharram 1444 H sawia na Agosti 7, 2022 M, baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Yeye, Mwenyezi Mungu amrehemu, alikuwa mmoja wa wabebaji da’wah wachangamfu tangu miaka ya sabiini. Alifungwa gerezani kwa miaka kadhaa, lakini aliendelea kufanya kazi ya kusimamisha sheria ya Mwenyezi Mungu hadi kifo chake, licha ya maradhi yake katika miaka ya hivi karibuni.

Na tunapotoa rambirambi zetu kwa familia za marehemu, pia tunatoa rambirambi zetu kwa wabebaji da’wah wote tukimuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu amfinike kwa Rehma zake Pana na ammiminie radhi zake na msamaha wake na adumu ndani ya Mabustani yake makubwa pamoja na Manabii, wakweli, mashahidi na watu wema, na hilo ndilo kundi tukufu, na tunamuomba Mwenyezi Mungu atujaalie sisi, familia yake na jamaa zake subira na faraja na asitunyime katika ujira wake na wala asitupotoshe baada yake, Amin.

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Iraq

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Iraq
Address & Website
Tel: 

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu