Jumatatu, 12 Dhu al-Qi'dah 1445 | 2024/05/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Faini ya Kwanza ya Denmark kwa Wanawake Wanaovaa Niqab Itawasukuma Waislamu Kushikamana na Maadili ya Kiislamu Hata Zaidi!

Mnamo Agosti 4, 2018, shirika la habari la BBC liliripoti juu ya mwanamke wa kwanza wa Kiislamu kulipishwa faini nchini Denmark kwa ajili ya kuvaa niqab hadharani. “Bunge la Denmark liliidhinisha mswada mnamo Mei 2018 wa kumwadhibu yeyote anayevaa niqab kwa faini” (BBC, 31 Mei 2018). Kwa sasa sheria hiyo haitaji burka na niqab kwa majina, bali inaeleza, “Yeyote anayevaa nguo inayofinika uso hadharani ataadhibiwa kwa faini”. Marufuku hiyo ilipangwa kuanza utekelezwaji wake mnamo Agosti 2018. Mnamo Ijumaa 3 Agosti 2018 mwanamke wa Kiislamu mwenye umri wa miaka 28 aliyekuwa amevaa niqab katika soko kuu la hadhara mjini Horshom, km 25 (maili 15) kaskazini mwa Copenhagen, alishambuliwa kwa nguvu na mwanamke mwengine aliyepinga vazi lake na kuchukua hatua mikononi mwake kumvua kwa lazima vazi hilo la Kiislamu. Polisi waliitwa katika eneo hilo la “vita” na baada ya kuangalia kanda ya CCTV walimweleza mwanamke huyo wa Kiislamu kuwa angelipishwa faini ya kroner 1,000 ($155; £120) baada ya kukataa kuvua niqab hiyo kwa agizo la polisi. Kwa sasa faini hiyo imeongezeka mara kumi zaidi hadi kroner 10,000 ($1,500; £1,200) kwa wahalifu wanaorudia kosa.

Soma zaidi...

Kifungo cha Watoto Wahamiaji cha Trump Chadhihirisha Umbile la Kinyama Lisilokubalika la Nidhamu ya Kitaifa ya Kidemokrasia ya Amerika

Chini ya sera ovu ya uhamiaji ya ‘kutokuwa na hata chembe ya uvumilivu’ ya Raisi wa Amerika, takriban watoto 2000, wengine wao wakiwa na umri mdogo wa miaka 4 au 5, ni miongoni mwa wale walioorodheshwa kama ‘wahamiaji haramu’, wametenganishwa kwa nguvu kutoka kwa wazazi wao katika mpaka wa Amerika na Mexico katika kipindi cha wiki sita pekee. Wametiwa ndani ya vibanda vya seng’enge katika vituo vya vizuizi, ambavyo hali zake zimesifiwa kuwa ‘mithili ya gereza’. Mojawapo ya vituo hivi vya wahamiaji katika jimbo la Texas kimepewa lakabu ya La Perrera, “kibanda cha mbwa”, ambamo watoto wanalala chini sakafuni juu ya magodoro membamba na makaratasi ndio blanketi zao. Kanda ya sauti ya watoto walioathirika kimawazo na kulia imepatikana, wakililia wazazi wao. Idara zimetangaza mipango ya kujenga mahema yatakayobeba mamia zaidi ya watoto katika jangwa la Texas ambako viwango vya joto kawaida hufikia nyuzi 40.     

Soma zaidi...

Risasi Zimechukua Maisha ya Watu … Na Serikali Zinacheza Densi Juu ya Majeraha!

Kwa mujibu wa mashirika ya habari; mtoto wa miezi 8 Laila Al-Ghandour alifariki mnamo Jumanne asubuhi eneo la Mashariki mwa Gaza baada ya kuvuta gesi. Tukio hili linaongeza idadi ya mashuhadaa wa “Msafara wa Mkubwa wa Maregeo” na kufikia idadi ya 61, wakiwemo watoto 7 na majeruhi 2,800, wengi wao wakiwa ni kutokana na risasi na wengine wakiwa ni kutokana na vipande vya mabomu na gesi ya sumu wakati wa uzimaji msafara na majeshi ya umbile la Kiyahudi iliyoanza maeneo tofauti Mashariki mwa ukanda wa Gaza katika kumbukumbu ya miaka 70 ya Nakba, na ambayo ilipinga na kukataa kuhamishwa kwa ubalozi wa Amerika jijini Al-Quds (Jerusalem).

Soma zaidi...

Watoto wa Ardhi Tukufu (Palestina) Wanaendelea Kutolewa Kafara Kutokana na Uhaini na Utiifu wa Biladi (za Waislamu kwa makafiri)!

Katika ripoti iliyo chapishwa na kituo cha habari cha Al-Jazeera idhaa ya Kiingereza, maafisa wa Umoja wa Mataifa (UM) walishutumu kuendelea kukamatwa kiholela kwa watoto katika Ardhi Tukufu (Palestina) na umbile la Kiyahudi, ikisema kuwa “Unyimaji uhuru huu kwa watoto hawa ni wa kitaasisi, kinidhamu, na ulio enea pakubwa”. Msururu wa ripoti za UM zilizo wasilishwa katika lile linaloitwa Baraza la Haki za Kibinadamu zimeonyesha jinsi hali za maisha za watu wa ardhi tukufu ya Palestina na Ukingo wa Magharibi na Gaza zilivyo zidi kudorora kwa zaidi ya mwaka mmoja uliopita, na jinsi watoto wanavyo himili ukatili wa uvamizi wa umbile la Kiyahudi, kwa mujibu wa Kate Gilmore, Naibu Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa UM.

Soma zaidi...

Watoto wa Ghouta, Takwimu za Kimataifa Zazidi Kuongezeka

Tangu Februari 18, majeshi katili ya serikali ya Syria yakisaidiwa na jeshi la anga la Urusi yameendelea na mashambulizi yao makali dhidi ya eneo la Mashariki mwa Ghouta, baada ya kuligawanya kuwa sehemu tatu za kivita. Natija yake, yaliweza kudhibiti zaidi ya asilimia 80 ya eneo hili lililo karibu na mji mkuu wa Damascus, ambalo tangu mwaka wa 2012 limekuwa ngome kubwa zaidi na muhimu zaidi kwa makundi ya upinzani. 

Soma zaidi...

“Msafara Wenye Utu” Kwa Ajili ya Wanaodhulumiwa Syria na Wanawake Waliokamata Huku Viongozi na Majeshi ya Waislamu Wakiutelekeza Utu Wao kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali

Mnamo Jumanne, Machi 6, wanawake kutoka nchi 55 walitoka katika “msafara wenye utu” kuanzia Istanbul mpaka Hatay. Lengo lao likiwa ni kunyanyua rai jumla juu ya wanawake 6,736 wakiwemo wasichana 417 wanaoteseka katika magereza ya serikali ya Assad, wakisubiri kifo chini ya mateso na ubakaji wa kila siku. Magereza hayo yamejaa wanawake wazee, waja wazito na wanawake waliojifungua punde tu kabla ya vifungo vyao. Inajulikana kuwa wanawake wanaopitia uchungu wa ubakaji na mateso aghalabu hujiua wanapo pata fursa ya kufanya hivyo.

Soma zaidi...

Kwa Kukosekana Khilafah Wanawake Waheshimiwa wa Ash-Sham Wanakabiliwa na Kudhulumiwa Hata na Wale Wanaodai Kuwa Walinzi Wao!!!

Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa linalo shughulikia ufadhili wa watu (UNFPA) limesema kuwa wanawake katika kambi za wakimbizi nchini Syria wamekuwa wakidhulumiwa kimapenzi na wanaume wanaotoa misaada kwa niaba ya UM na mashirika ya kimisaada ya kimataifa. Ripoti hiyo, “Sauti kutoka Syria 2018”, ili eleza kwa kina namna wanawake wakimbizi wa Syria wanavyo lazimishwa kutoa ngono kama badali kwa chakula kutoka UM, na kwamba dhulma hii imeenea maeneo yote kusini mwa Syria.

Soma zaidi...

Watoto wa Mashariki Mwa Ghouta Wanaangamizwa! Ni Nani Atakaye Hifadhi Damu Zao?!!

Mnamo 22 Februari, shirika la Kiingereza la kuchunguza haki za kibinadamu za watu wa Syria lilisema kuwa zaidi ya watu 400 waliuwawa, ikiwemo watoto 150 katika shambulizi baya la mabomu lililopita la siku 5 Mashariki mwa Ghouta lililofanywa na majeshi katili ya Syria na Urusi, ambayo yanalenga kiholela nyumba za raia, maduka, mashule, mahospitali na masoko, yakiwaacha watoto wakiwa wamezikika katika vifusi vya majumba. Watoto wamelazimika kutafuta hifadhi katika mapango, mashimo au mivungu ya nyumba zao huku 'wakisubiri zamu yao kufa'.

Soma zaidi...

UN – Wanaotarajiwa Kuwa Walinzi Ndio Wauwaji!!

Gazeti la Uingereza la The Times, lilichapisha ripoti kwa kichwa "Wafanyikazi wa UM 'wanahusika na ubakaji 60000 kwa muda wa muongo mmoja'". Ripoti hii inajiri wakati ambapo kumetukia uenezaji mkubwa wa habari na gazeti hilo kuhusu kufichuka kwa kashfa hii iliyo yashtua mashirika ya "misaada"; ambapo lilichapisha katika ukurasa wake wa mbele ripoti inayofichua kuwa shirika la Oxfam lilikuwa limemteua Roland Van Hauwermeiren kama mkurugenzi wa tawi lake la Haiti, ambaye hatimaye alikuwa katikati ya kashfa ya kuhusika na makahaba wakati wa shughuli za uokozi za shirika hilo kwa waathiriwa wa tetemeko la ardhi nchini Haiti, miaka miwili baada ya kutimuliwa kutoka kwa shirika jengine la misaada la Kiingereza kwa madai ya kuwatumia makahaba vile vile!

Soma zaidi...

Makongamano ya Kimataifa, Mipango ya Amani, Pasi na Kukomesha Wala Kupunguza Mashambulizi ya Mabomu ya Urusi!

Matukio ya umwagikaji damu yanayojiri Mashariki mwa Ghouta na Idlib; Mtandao wa Kutetea Haki za Kibinadamu wa Syria umesema kwamba raia wapatao 370 wameuwawa Mashariki mwa Ghouta tangu mwanzoni mwa mwaka huu, ukitaja kuwa miongoni mwa wafu ni watoto 63 na wanawake 72. Katika eneo la Idlib, hususan mji wa Sarakib, ambao ndio uliolengwa kwa dhoruba hii tangu mnamo 25 Disemba, Warusi na serikali ya kihalifu ya Syria zimemwaga chuki zake dhidi yake, ikitangazwa na baraza lake la mji kuwa eneo lililo kabiliwa na janga, ambapo idadi ya vifo mwezi Januari ilikuwa ni watu wapatao 30 na zaidi ya raia 60 kujeruhiwa. Hii ni ikiongezewa na kulengwa kwa mashule na mahospitali, ambazo idadi yake kubwa haziendeshi tena shughuli zake.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu