Jumanne, 28 Shawwal 1445 | 2024/05/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan

H.  13 Rajab 1445 Na: 1445 / 31
M.  Alhamisi, 25 Januari 2024

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Kuongezeka kwa Misimamo Mikali ya Hindutva ni Matokeo ya Moja kwa Moja ya Sera ya Kisekula ya Kigeni ya Pakistan! Khilafah Itapitisha Sera ya Kigeni, iliyojengwa juu ya Msingi wa Kubeba Ujumbe wa Kiislamu wa Tawhid kwa Ulimwengu Mzima

(Imetafsiriwa)

Mnamo tarehe 22 Januari 2024, Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi, alizindua Ram Mandir maarufu, kwa shangwe na sherehe nyingi. Likiwa katika mji wa Ayodhya, hekalu hilo la Kibaniani lilijengwa juu ya magofu ya Msikiti wa Babri, nembo kuu ya utawala wa Waislamu juu ya bara hilo dogo, ambao ulivunjwa na makundi ya Mabaniani mwaka wa 1992. Fikra ya Hindutva ya BJP inafafanuliwa na chuki yake dhidi ya Uislamu na Waislamu. Mradi wake wa kisiasa ni ule wa kuushinda Uislamu kama fikra ya kisiasa, na kuondoa athari zote za hadhara ya Kiislamu kutoka India, na Bara Hindi Dogo. Hivyo Ram Mandir na ujenzi wake ulikuwa wa umuhimu kisiasa na kitamaduni kwa Modi na BJP. Kupitia uzinduzi wa Ram Mandir, Modi alitangaza ushindi wa Mabaniani na Hindutva dhidi ya Waislamu na Uislamu.

Kuibuka kwa Modi, BJP na itikadi kali ya Hindutva, madarakani nchini India, ni matokeo ya moja kwa moja ya watawala wa Pakistan kupitisha sera ya kigeni ya kisekula, na kutabanni kitambulisho cha kisekula kwa Pakistan. Tangu kukwea kwa Jenerali Musharaf madarakani, majenerali wa kijeshi wa Pakistan wamejaribu kudhoofisha kitambulisho cha Kiislamu cha Pakistan, ili kuwaridhisha mabwana zao wa kisiasa na kimfumo jijini Washington. Uongozi wa kijeshi wa Pakistan ulitupilia mbali itikadi ya Jihad kama itikadi ya utendakazi wa Jeshi la Pakistan, ambayo ni fikra msingi na motisha kuu ya jeshi lolote la Kiislamu. Jeshi la Kiislamu linapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu (swt), likiinua Neno la Mwenyezi Mungu (swt) kuwa juu kabisa, huku likibeba Ujumbe wa Kiislamu wa Tawhid kwa ulimwengu mzima.

Badala ya jeshi lililokuwa mfano wa majeshi ya kihistoria ya Khilafah, ambayo yalifungua Bara dogo la India kwa Uislamu, au kukomboa sehemu kubwa ya Milki ya Kirumi katika enzi ya Uthmaniya, uongozi wa kijeshi wa Pakistan umejaribu kufafanua upya ruwaza ya Jeshi la Pakistan mbali na ruwaza kuu ya kupigana kwa ajili ya utukufu wa Uislamu na Waislamu. Badala yake, viongozi wa kijeshi wa Pakistan wamejaribu kuidunisha ruwaza ya Jeshi la Pakista hadi kuwa jeshi la kujihami, la kitaifa, ambalo limefungwa na mipaka ya dola ya kitaifa. Kwa hakika inasikitisha kusikia hasira za mkuu wa jeshi la Pakistan kwa mauaji ya Mpakistani mmoja, na kuitishia Afghanistan kwa majibu ya kijeshi, kwa upande mmoja, wakati kwa upande mwingine, zaidi ya Waislamu 25,000 wameuawa kwa kuchinjwa na umbile la Kiyahudi nchini Palestina, pasi na risasi iliyofyatuliwa na viongozi wa kijeshi wa Pakistan, au hata tishio moja la kimaneno la jibu la kijeshi lililotolewa.

Kukua kwa fikra ya Hindutva ni matokeo ya moja kwa moja ya itikadi mpya ya kijeshi ya Pakistan. Viongozi wa kijeshi wa Pakistan waliiondoa India kama tishio la kijeshi kutoka kwa itikadi yao ya kijeshi. Badala yake, katika kipindi cha miongo miwili iliyopita uongozi wa kijeshi wa Pakistan umejaribu kuligeuza Jeshi la Pakistan kuwa jeshi la kitaifa, la kukabiliana na ugaidi. Ruwaza hii ya Jeshi la Pakistan inakinzana moja kwa moja na ruwaza ya makamanda wakuu wa kijeshi wa Kiislamu kama Muhammad bin Qasim, Mahmood Ghaznavi, Shahabudin Ghauri na Qutb ud-Din Aibak ambao walianzisha utawala wa Uislamu juu ya Bara Ndogo la India, kuanzia 712 hadi 1757 M. Zaidi ya hayo, ruwaza finyo ya kitaifa, kwa jeshi la Waislamu inagongana moja kwa moja na hukmu za Shariah, na ruwaza ya Kiislamu kwa jeshi la Waislamu.

Enyi Maafisa wa Jeshi la Pakistan! Mwenyezi Mungu (swt) amekuamrisheni kupigana katika Njia yake mpaka Dini yake (swt) itawale. Mwenyezi Mungu (swt) asema katika Quran Tukufu,

[قَاتِلُوا الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَلَا بِالْيَوْمِ الْآخِرِ وَلَا يُحَرِّمُونَ مَا حَرَّمَ اللَّهُ وَرَسُولُهُ]

“Piganeni na wasio muamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho, wala hawaharimishi alivyo harimisha Mwenyezi Mungu na Mtume.” [Surah At-Tawbah 9:29].

Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema, «وَاعْلَمُوا أَنَّ الْجَنَّةَ تَحْتَ ظِلاَلِ السُّيُوفِ» “Na jueni kuwa Pepo (Jannah) iko chini ya vivuli vya panga.” (Bukhari na Muslim). Ipeni Nusrah yenu Hizb ut Tahrir, chini ya Amiri wake, mwanachuoni mkubwa na mtawala, Sheikh Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, kwa ajili ya kusimamisha tena Khilafah Rashida ya Pili kwa Njia ya Utume. Khilafah itakurudisheni kwenye njia ya watangulizi wenu katika silaha, makamanda wakubwa wa kijeshi wa Kiislamu waliopigania utukufu na ushindi wa Uislamu. Simamisheni Khilafah na mtoe pigo la kifo kwa Modi na itikadi yake ya Hindutva. Kisha mupate heshima na ujira wa kupandisha bendera za Liwaa’ na Rayah za Khilafah juu ya Srinagar na Al-Qudsi.

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan
Address & Website
Tel: 
https://bit.ly/3hNz70q

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu