Jumamosi, 25 Shawwal 1445 | 2024/05/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Ardhi ya Baraka-Palestina

H.  14 Safar 1445 Na: BN/S 1445 / 01
M.  Jumatano, 30 Agosti 2023

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mtume (saw) amesema, «‌مَنْ ‌حَمَلَ عَلَيْنَا السِّلَاحَ فَلَيْسَ مِنَّا» “Yeyote atakayebeba silaha dhidi yetu, si katika sisi.”
Chini ya Kisingizio cha Usumbufu, Mamlaka ya Palestina Inashirikiana na Mvamizi katika Uchokozi dhidi ya Watu wa Palestina!
(Imetafsiriwa)

Mamlaka ya Palestina (PA) ilifanya uhalifu wa kinyama zaidi Jumatano hii asubuhi kwa kumuua kijana Abdulqader Zaqdah, ambaye alijeruhiwa wakati wa uvamizi wao kwenye kambi ya Tulkarm. Wengine kadhaa pia walijeruhiwa. Uvamizi huu unafanywa kwa kisingizio cha kuondoa 'usumbufu' kwenye barabara ya umma, udhuru ule ule wanaoutumia kila wakati (kama walivyofanya katika Kambi ya Balata huko Nablus) kutengua vizuizi vilivyowekwa na vijana ili kuzuia uvamizi wa vikosi vya uvamizi, na hivyo kuwezesha kuingia kwao kwenye kambi!

Uvamizi huu na uchokozi mkubwa unakusudia kufichua, kwa mtu yeyote aliye na macho mawili, ule unaoitwa mradi wa kitaifa unaowakilishwa na mamlaka. Inasisitiza waziwazi kuwa sio chochote ila ni mradi wa usalama kutumikia umbile la Kiyahudi na jeshi tekelezi ambalo hufanya kazi dhidi ya watu wa Palestina. Ni mradi ambao hufanywa tu na wale wanaomsaliti Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na watu na Ummah wao wenyewe.

Kile PA ilichofanya katika kambi ya Tulkarm leo hakitofautiani na dori yake tangu siku ya kwanza, na hakitengani na kile ambacho imekuwa ikikifanya hivi karibuni huko Jenin na kambi yake, na vile vile katika Nablus na kambi zake. Kinafanana sambamba na kile kile uvamizi hufanya kwa usahihi, ikiwemo ukamataji, kufukuza, na mauaji inapolazimu. Sio tofauti na mikutano katika Aqaba na Sharm el-sheikh pia. Yote hii inakusudia kuzuia na kuimaliza kila nafsi na sauti ya jihad ya watu wa Palestina. Kwa kutumia nyudhuru kuondoa usumbufu kwa kupitiliza, kwa kweli ni jinai, matumizi ya nguvu hayaangazi ukweli wa uhalifu. Badala yake, inazua swali la kimaumbile linalojirudia rudia: Je! Mawakala hawa walikuwa wapi wakati wa usumbufu wa vikosi vya umbile la Kiyahudi kwenye kambi, kusababisha sokomoko, vifo, na uharibifu? Je! Walijiandaa vipi kuwalinda watu na kuondoa madhara na uchokozi wa umbile la Kiyahudi kutoka kwao? Je! Kuondoa vizuizi vya saruji kunahitaji mauaji? Au ni ujumbe kwa watu wa Palestina kwamba mamlaka haitasita kuwafyatulia risasi, kuwaua, na kwamba haitilii maanani yoyote kwa "amani ya raia", na kwamba je damu sio mstari mwekundu? Au ni ishara ya maumbile ya dori yake ya baadaye na kile watu wa Palestina wanaweza kutarajia kutoka kwake ikiwa watakaa kimya juu ya uhalifu wake dhidi yao?

Ewe watu wetu katika Ardhi Iliyobarikiwa, Mamlaka ya Palestina, pamoja na uhalifu na uratibu wake kwa uvamizi huo, inakusukumeni nyinyi na Mujahidina kulenga mambo ya mamlaka ya usalama na mauaji katika kujilinda. Hili litakuwa na athari kubwa kwenu, na inaambatana na kile walowezi wanatafuta kuweka hali halisi katika Ukingo wa Magharibi. Mamlaka ya wasaliti inawaandama Mujahidina na kutekeleza sera za Marekani na maadui wa Uislamu kukufanya muwe makombo matamu kwa umbile la Kiyahudi. Mnajua kuwa walowezi katika Ukingo wa Magharibi wasingefanikiwa kufanikisha kile walichofanya lau si kwa kushirikiana mamlaka hayo na utoaji wake wa kifiniko kwa idadi ya madalali wa ardhi ambao huvujisha mali na ardhi kwa walowezi.

Hatari halisi inayotishia kuishi kwenu ni kwamba mamlaka ya Palestina inashirikiana na uvamizi huo kuwasha moto wa ugomvi na vita kati yenu. Hiki ndicho umbile la Kiyahudi inachotafuta, kama ilivyo kwa mtazamo wao, nyinyi ni watu ambao mnaweza kuuawa, kufukuzwa nchi, au kulazimishwa kuishi katika udhalilifu chini ya utawala wao bila ya upinzani wowote.

Enyi Waislamu, azimio la kadhia ya Palestina na kuondoa ukandamizaji kutoka kwa watu wake kunaweza kupatikana tu kupitia suluhisho moja, ambalo ni kuling’oa umbile la Kiyahudi kutoka kwa mizizi yake na kukataa kila kitu kinachohusiana nalo, iwe ni mipango ya ndani au ya kimataifa, au masuluhisho ambayo hutumika tu kuliimarisha na kulilinda. Lengo letu limefunganishwa na Uislamu na kwenu, na kwa msingi huu, lazima isuluhishwe. Kwa nusra na nguvu ya Mwenyezi Mungu, utawala wa Kiislamu utaanzishwa, na Khilafah (ukhalifa) kwa njia ya utume itasimama. Majeshi ya Waislamu yataingia katika ardhi iliyobarikiwa ili kuikomboa kutoka kwa umbile la Kiyahudi.

[وَاللهُ غَالِبٌ عَلَى أَمْرِهِ وَلَكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ]

“Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kushinda katika jambo lake, lakini watu wengi hawajui.” [Yusuf:21]

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina)

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Ardhi ya Baraka-Palestina
Address & Website
Tel: 

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu