Ijumaa, 09 Dhu al-Qi'dah 1445 | 2024/05/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Sudan

H.  5 Muharram 1445 Na: HTS 1445 / 02
M.  Jumapili, 23 Julai 2023

Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Wakutana na Mkuu wa Kabila la Bakr
(Imetafsiriwa)

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Ya Sudan ukiongozwa na Ustadh Muhammad al-Hassan Ahmad, Mwanachama wa Baraza la Hizb ut Tahrir  katika Wilayah ya Sudan, akiandamana na wanachama wa Hizb Ut Tahrir: Ndugu: Muhammad Mukhtar, Muntasir Karar, na Al-Samad al-Tayyib ulikutana na mkuu wa kabila la Bakr huko Gadharef, Ustadh Saif al-Dawla Haidar al-Taher Bakr, katika Baraza diwan (baraza) yake, kwa uwepo wa Ustadh Muhammad Fadl, mkuu wa Chama cha Kijamhuri huko Gadharef.

Baada ya kufahamiana, ujumbe huo ulifafanua mtazamo wa hizb kuhusu mzozo nchini Sudan, na kwamba sababu kiasili ilitokana na mvutano wa Marekani na Ulaya kwa ajili ya ushawishi nchini Sudan, na uporaji wa utajiri wake kupitia vibaraka wao. Hii ndio sababu mzozo umebakia unatokota kati ya majeshi ya Marekani (Jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka), na kati ya raia wa Ulaya, na kwamba vita hivi kati ya majeshi kwa kweli kwa ajili ya kuwaondoa wapambe wa Ulaya kutoka kwa mandhari ya kisiasa, au angalau kuzuia nguvu halisi kuwepo mikononi mwao.

Ujumbe huo ulieleza kuwa hakuna suluhisho kwa yale yanayotokea nchini Sudan, au katika nchi zengine za Kiislamu, isipokuwa kwa kusimamisha mfumo wa Kiislamu. Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, na kazi kubwa ya kuzuia vita, na (kulinda) utukufu wa damu ya Waislamu.

Mwisho wa mkutano, ujumbe huo ulimshukuru mkuu huyo kwa ukarimu na mapokezi mazuri.

Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Sudan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
Address & Website
Tel: 

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu