Jumatatu, 27 Shawwal 1445 | 2024/05/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Hizb ut Tahrir Afisi Kuu ya Habari:

Kitengo cha Wanawake "Kampeni ya Kiulimwengu na Siku ya Wanawake ya Kuchukua Hatua kwa ajili ya Palestina"

Kampeni ya Kiulimwengu na Siku ya Wanawake Kuchukua Hatua Kuyaamsha Majeshi ya Waislamu na Wito kwao Kuwaokoa Wanawake wa Gaza na Watoto wake na Ukombozi Kamili wa Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina)

Pamoja na kuendelea kwa umbile halifu la Mayahudi (Wazayuni) katika upigaji mabomu wa kikatili na wa kihujma wa Gaza, wanawake na watoto ndio wanaopitia mauaji haya ya halaiki. Upigaji mabomu mpana umefanywa kwa majengo ya makaazi, maeneo ya wakimbizi, shule, hospitali, na vitongoji vyote vimeigeuza Gaza kuwa makaburi kwa wanawake na watoto. Kwa kuongezea, watoto wa Gaza wanakabiliwa na kifo kwa sababu ya njaa, ukame na magonjwa, huku umbile la Kiyahudi likitumia chakula, maji, dawa na mafuta kama silaha katika mzingiro wake wa kikatili kwa wakaazi.

Mbali na hilo, wakaazi wa Gaza milioni 1.5 ni wakimbizi tangu 7 Oktoba 2023 M. Wakati huo huo, umbile la (Kizayuni) la Kiyahudi linaendelea kuwatishia Waislamu katika Ukingo wa Magharibi, kuwatendea kikatili, kuwafunga na kuwaua lipendevyo na bila kihisabiwa au kuadhibiwa.

Kujibu mauaji haya ya halaiki na janga katika karne ya ishirini na moja, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir, kwa kushirikiana na Wanawake wa Hizb ut Tahrir kote ulimwenguni, kimezindua kampeni kubwa ya kiulimwengu ambayo itatangulia "Siku ya Kimataifa ya Wanawake ya Kuchukua Hatua kwa ajili Palestina" mnamo 26 Novemba 2023 M kuyataka majeshi ya Waislamu kutaharaki haraka ili kuwaokoa wanawake wa Gaza na watoto wake na kuikomboa Ardhi yote Iliyobarikiwa (Palestina) kutokana na saratani hii ya uvamizi, na kutoa nusra kwa Hizb ut Tahrir ili kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume ambayo itawapa utetezi wa kijeshi Waislamu wadhaifu kote ulimwenguni.

Siku ya kazi itajumuisha mabara matano na itajumuisha maandamano, semina na shughuli zengine kwa wanawake nchini Palestina, Uturuki, Indonesia, Tunisia, Lebanon, Malaysia, Kenya, Amerika, Australia, Denmark, Uholanzi, Ubelgiji na Uingereza. Tunatoa wito kwa Waislamu kuunga mkono kampeni hii muhimu, na tunawaalika wanawake wa Kiislamu kote ulimwenguni kuungana nasi kwenye Siku ya Kufanya Kazi ya Kimataifa ya Wanawake kwa ajili ya Palestina.

Dkt. Nazreen Nawaz

Mkurugenzi wa Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Ijumaa, 03 Jumada Al-Awwal 1445 H sawia na 17 Novemba 2023 M

Hotuba kutoka Semina ya Uingereza juu ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake Kuchukua Hatua kwa Ajili ya Palestina

Bonyeza Hapa

Angazo la Amali Hizi za Kimataifa

Jumapili, 12 Jumada al-Awwal 1445 H - 26 Novemba 2023 M

Dkt. Nazreen Nawaz, Mkurugenzi wa Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari

Amerika

Australia

Ubelgiji

Uingereza

Denmark

Indonesia

Kenya

Lebanon

Malaysia

Uholanzi

Ardhi Iliyobarikiwa - Palestina

Tunisia

Uturuki

Dondoo kutoka kwa Amali
"Siku ya Kimataifa ya Wanawake Kuchukua Hatua kwa ajili ya Palestina"

Jumapili, 12 Jumada al Awwal 1445 H sawia na 16 Novemba 2023 M

Video Fupi ya Ualishi

Kilio kutoka kwa Ardhi Iliyobarikiwa katika Siku ya Kimataifa ya Wanawake Kuchukua Hatua kwa ajili ya Palestina

Wito kutoka kwa Dada wa Kiislamu kutoka Uholanzi kwenda kwa Majeshi ya Waislamu Kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa

Wito kutoka kwa Dada wa Kiislamu kutoka Lebanon kwenda kwa Majeshi ya Waislamu Kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa

Wito kutoka kwa Dada wa Kiislamu kutoka Amerika kwenda kwa Majeshi ya Waislamu Kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa

Wito kutoka kwa Dada wa Kiislamu kutoka Ujerumani kwenda kwa Majeshi ya Waislamu Kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa

Wito kutoka kwa Dada kutoka Tunisia kwenda kwa Majeshi ya Waislamu Kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa

Wito kutoka kwa Dada kutoka Uturuki kwenda kwa Majeshi ya Waislamu Kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa

Wito kutoka kwa Dada katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina kwenda kwa Majeshi ya Waislamu Kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa

Wito wa Pili kutoka kwa Dada katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina kwenda kwa Majeshi ya Waislamu Kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa

Mikutano pamoja na Wanawake na Mabinti wa Umma wa Kiislamu katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina)

- Video ya Kwanza -

- Video ya Pili -

- Video ya Tatu -

- Video ya Nne -

Kalima ya Dkt. Nazreen Nawaz

Mkurugenzi wa Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Kwa Mnasaba wa Uzinduzi wa Kampeni ya Kiulimwengu

Ijumaa, 03 Jumada Al-Awwal 1445 H sawia na 17 Novemba 2023 M

Ili Kufuatilia Amali ya Kongamano la Kimataifa ambalo Limeandaliwa na

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Kwa Kichwa: "Je, Palestina Tutaikomboa Vipi?"

Ijumaa, 17 Jumada Al-Akhir 1445 H sawia na 30 Disemba 2023 M

Bonyeza Hapa


TUFANI YA TWITTER

Kusoma Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Kitengo cha Wanawake cha Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Lebanon cha Andaa Semina ndani ya Wigo wa Amali ya Wanawake ya Kiulimwengu kwa ajili ya Palestina

Jumapili, 12 Jumada Al-Awwal 1445 H sawia na 26 Novemba 2023 M

Bonyeza Hapa

Kusoma Taarifa ya Kitengo cha Wanawake

Iliyotangaza kuzinduliwa kwa kampeni yake ya ulimwengu, yenye kichwa:

"Kampeni ya Kimataifa na Siku ya Kufanya Kazi ya Kimataifa kwa ajili ya Palestina

Kwa ajili ya Kutoa Wito kwa Majeshi ya Waislamu Kuwaokoa Wanawake na Watoto wa Gaza na Kuikomboa Ardhi nzima ya Al-Aqsa”

Jumapili, 03 Jumada Al-Awwal 1445 H sawia na 17 Novemba 2023 M

Bonyeza hapa

- Alama Ishara za Kampeni -

#طوفان_الأقصى

#الجيوش_إلى_الأقصى

#الأقصى_يستصرخ_الجيوش

#AksaTufanı

#OrdularAksaya

#ArmiesToAqsa

#AqsaCallsArmies

Fuatilia kwa Lugha Nyenginezo

   
   
   

 

 

Imebadilishwa mara ya mwisho mnamoAlhamisi, 18 Januari 2024 09:19

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu