Ijumaa, 24 Shawwal 1445 | 2024/05/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Hizb ut Tahrir / Uholanzi:

Kongamano la Khilafah la kila Mwaka “Kulenga Familia ya Kiislamu katika nchi za Magharibi”

 

Hizb ut Tahrir / Uholanzi yaandaa Kongamano la Khilafah la kila mwaka chini ya kichwa:

“Kulenga familia ya Kiislamu katika nchi za Magharibi”

Na hilo ni kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 102 ya kuvunjwa kwa Dola ya Kiislamu (Khilafah).

Jumapili, 13 Shaaban 1444 H - 05 Machi 2023 M

Familia katika nchi za Magharibi inakabiliwa na changamoto nyingi. Ulimwengu huu ambao urasilimali unatawala pamoja na fikra na fahamu zake, unatishia mfumo wa jadi wa familia na dori iliyopewa wanaume na wanawake katika kuianzisha na kuichunga. Hata hivyo Waislamu wana uongozi wa kifikra wa Kiislamu unaowafanya waweze kukabiliana na changamoto na matishio haya, na kuwasilisha mtazamo wa Kiislamu kwa Jamii, kama suluhisho msingi na lenye mafanikio kwa matatizo ya mwanadamu!

Hivyo basi je mtazamo huu ni upi? Je, familia tutailinda vipi?

Je, dola ijayo ya Khilafah itakuwa na dori ya kiulimwengu katika suala hili?

Tunakualikeni muhudhurie kongamano hili la kila mwaka, ambapo maswali haya yatajibiwa, na changamoto na masuluhisho yatajadiliwa, kwa idhini ya Mwenyezi Mungu (swt).

Kwa maelezo Zaidi tafadhali zuru mitandao ya Hizb ut Tahrir / Uholanzi:

Tovuti Rasmi ya Hizb ut Tahrir / Uholanzi

Facebook: Hizb ut Tahrir / Uholanzi

Akaunti ya Twitter: Hizb ut Tahrir / Uholanzi

Instagram: Hizb ut Tahrir / Uholanzi

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu