Jumamosi, 10 Dhu al-Qi'dah 1445 | 2024/05/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Umbile la Kiyahudi ni Dhaifu na Oga

Ukimya wa Majeshi Yetu ndio Unalipa Nguvu

(Imetafsiriwa)

Habari:

Idadi ya Waislamu wa Gaza waliokufa kutokana na mauaji, ukatili na mauaji ya halaiki yaliyofanywa na umbile la Kiyahudi linalokalia kwa mabavu huko Gaza katika muda wa siku 100 zilizopita tangu mafuriko ya Aqsa imezidi elfu 25.

Maoni:

Mbele ya mauaji ya halaiki yaliyofanywa na umbile la Kiyahudi linalokalia kwa mabavu huko Gaza, kwa nini sisi kama Umma wa Kiislamu tunashindwa kuzuia ukatili na dhambi hii kubwa huku tukiwa na uwezo wa kuizuia?

Baada ya zaidi ya karne tatu za kupigania haki na uhuru dhidi ya mawazo ya kikatili na ya kimwitu ya zama za kati, Magharibi kafiri mkoloni iligundua mapinduzi ya fikra na kufikia ubepari. Kisha, pamoja na Mapinduzi ya Viwanda, iligundua ukoloni. Kwa uwezo wa kiteknolojia na uzoefu ulioletwa na mapinduzi ya viwanda, ilikoloni Afrika, Amerika ya Kusini, Asia ya Mashariki ya Mbali na India. Ilivunja Dola ya Kiuthmani. Iliiondoa Khilafah. Iliteua serikali nyingi zilizohusishwa nayo kwenye ardhi ya Uthmani. Ilifanya serikali hizi kupigana na watu wao wenyewe. Mkoloni Kafiri Magharibi alisababisha uharibifu mkubwa katika ardhi hizi kupitia serikali hizi zilizowahudumia. Damu, machozi, njaa na taabu, kurudi nyuma, ugaidi, machafuko, vita vya wenyewe kwa wenyewe, migogoro ya kisiasa na kiuchumi imekuwa hatima ya nchi hizi.

Kafiri wa kikoloni hadhara ya Kimagharibi ilijidhihirisha kwetu kama kiwango cha ustaarabu wa kisasa. Ilidhalilisha historia yetu na maisha yetu ya nyuma yaliyojaa ushindi dhidi yao. Ilitufanya tuwaonee aibu mababu zetu. Kwa hivyo, ilichukua akili zetu. Ilitudhoofisha kwa kutukata na mizizi yetu ambayo tungepata nguvu. Imetufunga minyororo mikononi na miguuni mwetu.

Wameyazuia majeshi yetu kwa kuwapendelea wale wanaotutawala, ili tusiwazuie kuhamasisha majeshi yao kwa maslahi yao binafsi. Wameyafungia majeshi yetu kwenye kambi zao. Walifanya majeshi yetu yatumikie tu mipango na maslahi ya nchi za Magharibi. Waliharibu uhuru wetu. Imewatenga watawala wetu na majeshi yetu kutoka kwa watu wao na imani zao wenyewe na kuwageuza kuwa sehemu ya mfumo wa ulimwengu wa kikatili na wa kikoloni ambao wao wenyewe wameuweka, ambao umetulia juu ya wanadamu wote.

Hata hivyo, Waislamu wa nchi hizi walikuwa wametayarisha majeshi kuzuia haya yote yasitokee. Hawakula wenyewe bali waliwalisha, hawakuvaa wenyewe bali waliwavisha. Walikuwa wamewapa nafasi nzuri zaidi na kuwapa silaha bora zaidi. Walikuwa wamewapa mishahara bora kabisa na kuwafanya waishi kwenye nyumba bora zaidi. Kwa nini? Kulinda nchi zao, uhuru wao, maisha yao, mali zao, heshima na utu wao, imani yao, ambayo mkoloni kafiri Magharibi alitaka kuiangamiza kwa uadui wake wa kiburi na kichokozi.

Kwa bahati mbaya, mkoloni kafiri Magharibi ametupenyeza, akatuteka na kujaribu kuharibu matumaini ya Umma wa Kiislamu na wanadamu wote katika nafsi ya watawala na majeshi yetu.

Mauaji ya kikatili, ya kikatili, ya kikatili, ya kikatili, ya kiburi, ya kukiuka sheria na ya kinyama ya umbile la Kiyahudi linalowateka nyara wananchi wa Palestina kwa hakika ni shambulizi dhidi ya heshima na adhama ya majeshi ya nchi za Kiislamu na wananchi wote wa Kiislamu katika nafsi ya Wapalestina. Umbile la Kiyahudi limeyadharau majeshi ya Waislamu na kwa ufupi limeyapuuza tu.

Kwa sababu ni hakika. Ni hakika kwamba si jeshi la Uturuki, wala jeshi la Misri, wala jeshi la Jordan, wala jeshi la Arabia, wala jeshi lolote la Kiislamu litakalochukua hatua dhidi ya mashambulizi haya. Ni hakika kwamba majeshi yatabaki katika kambi zao. Haliyaogopi na halijiepushi na majeshi yetu, na haliyachukulii majeshi yetu kwa uzito. Ndiyo maana lina uwezo wa kutekeleza mashambulizi haya ya kikatili.

Iwapo watawala na majeshi ya Waislamu wanaweza kujinasua kutoka katika pingu na minyororo ambayo Kafiri Magharibi mkoloni ameziweka kwenye akili na nyoyo zao kwa kuregea kwenye imani na mizizi yao, na kuuregesha Umma wa Kiislamu kwenye nguvu zake kuu za zamani kwa kusimamisha Khilafah ambayo itawaunganisha Waislamu wote:

Basi hapo tu, wanaweza kuwa mashujaa wakubwa wanaouokoa Umma wa Kiislamu.

Hapo tu ndipo, wanapoweza kuokoa wanadamu wote kutokana na mfumo  wa kilimwengu wa makafiri wa kikoloni katili na wakali na kukomesha utawala wao.

Hapo tu, wataweza kutufanya turudishe heshima, utu na uhuru wetu ambao tulipoteza kitambo.

Hapo tu, wataweza tena kuwa tumaini la Umma wa Kiislamu na wanadamu wote.

Hapo ndipo wataweza kuitakasa Palestina kutokana na Mayahudi na kuutukuza Umma wa Kiislamu.

Hapo tu, ndipo Umma wa Kiislamu utainua kichwa chake ulichokiinamisha na kukumbatia majeshi yake.

]وَمَا لَكُمْ لَا تُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ وَالْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ الرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ وَالْوِلْدَانِ الَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا أَخْرِجْنَا مِنْ هَذِهِ الْقَرْيَةِ الظَّالِمِ أَهْلُهَا وَاجْعَل لَنَا مِنْ لَدُنْكَ وَلِيًّا وَاجْعَل لَنَا مِنْ لَدُنْكَ نَصِيرًا الَّذِينَ آَمَنُوا يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ وَالَّذِينَ كَفَرُوا يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ الطَّاغُوتِ فَقَاتِلُوا أَوْلِيَاءَ الشَّيْطَانِ إِنَّ كَيْدَ الشَّيْطَانِ كَانَ ضَعِيفًا[

“Na mna nini msipigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu na ya wale wanao onewa, wanaume na wanawake na watoto, ambao husema: Mola Mlezi wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhaalimu, na tujaalie tuwe na mlinzi anaye toka kwako, na tujaalie tuwe na wa kutunusuru anaye toka kwako. Walio amini wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na walio kufuru wanapiana katika njia ya upotofu. Basi piganeni na marafiki wa Shet'ani. Hakika hila za Shet'ani ni dhaifu.” [Surah An-Nisaa 75-76]

Imeandikwa kwa Ajili ya Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir na

Remzi Özer – Wilayah Uturuki

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu