Ijumaa, 24 Shawwal 1445 | 2024/05/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Uhakiki wa Habari 19/07/2023

Urusi Yaachana na Mkataba wa Nafaka wa Bahari Nyeusi

Mnamo Julai 17, wizara ya mambo ya nje ya Urusi ilitangaza kuwa nchi hiyo itaondoka kwenye makubaliano ya Mkataba wa Nafaka wa Bahari Nyeusi ambao umesaidia kuleta nafaka za Ukraine katika masoko ya dunia katika mwaka uliopita. Kama sehemu ya kujiondoa katika mpango huo, Urusi ilisema haitadhamini tena usalama wa meli zinazopita kwenye ukanda wa bahari wa misaada ya kibinadamu katika Bahari Nyeusi. Wizara hiyo pia ilitangaza kuwa Kituo cha Uratibu wa Pamoja, ambacho kimekuwa kikifuatilia utekelezaji wa mpango huo kutoka Istanbul, kitavunjwa. Urusi ilidai iliamua kuondoka kwa sababu matakwa yake ya kuongeza muda wa makubaliano hayo hayajatekelezwa. Lakini tangazo hilo lilikuja saa chache baada ya shambulizi la droni ndege la baharini kuharibu daraja la Kerch Strait linalounganisha Urusi na Crimea. Katibu wa Vyombo vya Habari wa Kremlin Dmitry Peskov alikanusha kisa hicho ambacho kilihusishwa na uamuzi wa Moscow. Uamuzi wa Urusi kujiondoa katika Mkataba wa Nafaka wa Bahari Nyeusi mwaka mmoja baada ya kutiwa saini utadhoofisha uhusiano wake na Uturuki na kuhatarisha uchumi wa Ukraine uliokumbwa na vita pamoja na kupandisha bei ya vyakula duniani. Mnamo Julai 2022, maafisa wa Urusi na Ukraine walitia saini makubaliano tofauti na Uturuki na UN ambayo yaliruhusu usafirishaji wa nafaka kutoka bandari zilizochaguliwa za Ukraine kwenye Bahari Nyeusi, kwa badali ya mkataba wa maelewano yaliyolenga kuwezesha usafirishaji wa nafaka na mbolea kutoka Urusi kwenda kwa masoko ya dunia. Urusi imekuwa ikielekeza matatizo kadhaa ya kimfumo yanayohitaji kutatuliwa ili kuruhusu kuendelea kwa mpango huo wa nafaka. Hizi ni pamoja na kurudisha Benki ya Kilimo ya Urusi (Rosselkhozbank) kwenye mfumo wa malipo wa SWIFT; kuanza tena kwa usambazaji wa mashine za kilimo na vipuri kwa Urusi kati ya mambo mengine. Kujiondoa kwa Moscow katika mkataba huo wa nafaka kutafanya nchi za Magharibi zipunguze uwezekano wa kuwezesha mauzo ya nje ya kilimo nchini Urusi, na kulazimisha Moscow kuzingatia operesheni zisizovutia za kijeshi ili kuizuia Ukraine kusafirisha nafaka zake yenyewe. Kumalizika kwa nafaka kunaweza kuzua hofu ya uhaba wa nafaka na hofu kutoka kwa waagizaji wa nafaka, ambayo inaweza kudhuru uhusiano wa Urusi na mataifa kama vile Uturuki.

Makumi ya Wanachama wa PTI Waunda Chama Kipya

Wanachama 57 wa chama cha Waziri Mkuu wa zamani Imran Khan cha Pakistan Tehreek-e-Insaf (PTI) walitangaza kwamba wanajiondoa katika chama hicho ili kuunda chama chao kinachoitwa Chama cha Wabunge cha Pakistan Tehreek-e-Insaf. Wengi wa wanachama wa chama hicho kipya wanatoka jimbo la Khyber Pakhtunkhwa, ambalo kwa muda mrefu limekuwa ngome ya PTI, akiwemo kiongozi wa chama kipya, Pervez Khattak, ambaye awali aliwahi kuwa waziri wa ulinzi wa Pakistan na waziri mkuu wa Khyber Pakhtunkhwa. Mamlaka zimefanya msako wa PTI kufuatia ghasia zilizofanywa na wafuasi wa PTI baada ya kukamatwa kwa Imran Khan Mei 9. Msako huo wa mamlaka za kijeshi umeshuhudia kundi kubwa la watu muhimu wa PTI wakijiondoa kwenye chama hicho na kukemea ghasia hizo katika wiki za hivi karibuni. Chama kipya, ambacho kina watu hao hao wa zamani kinakabiliwa na mvutano mkali na migawanyiko ya ndani na umaarufu wa kudumu wa Imran Khan. Ndani ya saa moja baada ya kutangazwa kuanzishwa kwa chama kipya, angalau watu tisa wanaohusishwa na chama kipya walikataa ripoti za madai ya kuhama kwao PTI na kusisitiza uaminifu wao kwa Khan.

Uturuki Yatia Saini Mkataba Mkubwa Zaidi wa Ulinzi na Saudi Arabia

Saudi Arabia ilikubali kununua droni za Uturuki, ambazo pia zitajumuisha uhamishaji wa teknolojia na uzalishaji wa pamoja, katika kandarasi kubwa zaidi ya ulinzi na usafiri wa anga katika historia ya Uturuki. Saudi Arabia na Uturuki zilifikia makubaliano hayo wakati wa ziara ya Erdogan jijini Riyadh kama sehemu ya ziara yake ya baada ya kuchaguliwa tena katika Ghuba ya Kiarabu. Erdogan pia alisafiri hadi Qatar na Imarati. Erdogan alishinda uchaguzi wa hivi majuzi katikati ya changamoto kubwa za kiuchumi, nyingi alizofanya mwenyewe. Mikataba hiyo ya mauzo ya nje inampa Erdogan uwekezaji unaohitajika sana na fedha huku uchumi wa Uturuki ukiyumba kutokana na mfumko wa bei na deni la taifa linalokua. Kwa Saudi Arabia, mpango huo utarahisisha matarajio ya nchi hiyo kujenga ujuzi wake wa teknolojia ya ulinzi, na faida ya ziada ya kutohatarisha kuvuruga uhusiano wa Marekani na Saudi Arabia kwa sababu Saudi Arabia itakuwa ikiagiza silaha kutoka Uturuki, ambayo ina uhusiano wa karibu wa kisiasa na kimkakati na Marekani.

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu