Jumatatu, 27 Shawwal 1445 | 2024/05/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Enyi Watawala katika Ardhi za Waislamu ... Sikizeni na Muzingatie...


(Imetafsiriwa)

Kuna vita vya kikatili vinavyofanywa dhidi ya Gaza na kukosekana uingiliaji kati wa majeshi ya Waislamu, haswa yale yanayoizunguka Palestina, licha ya mauaji yote yanayofanywa na umbile la Kiyahudi, mchana na usiku. Vita hivi vya kikatili sasa vimeambatana na taarifa zinazofuatana kutoka kwa wakoloni wa makafiri, haswa Marekani na Uingereza, kuhusu suluhisho la dola mbili kwa Palestina. Suluhisho hili ni dola ya Mayahudi katika sehemu kubwa ya Palestina, na baadhi yake ni imeondolewa nguvu ya kijeshi ambayo Wapalestina wamehifadhiwa! Suluhisho hili limetajwa mara nyingi, midomoni mwa watawala katika ardhi za Waislamu, haswa nchi za Kiarabu zinazoizunguka Palestina, huku mamlaka ya Palestina ikiwa mstari wa mbele wa wito huu ...

Kisha, kukawa na mwendelezo wa uvamizi wa kikatili kwa karibu siku hamsini. Halafu, mkataba wa kusitisha vita wa wiki nzima uliidhinishwa na umbile la Mayahudi, kisha kuubatilisha, na kuendelea na hata ukatili mkubwa zaidi na bila ya uingiliaji kati wa majeshi. Yote haya ni kuonyesha kana kwamba umbile la Mayahudi ni nguvu kubwa, kiasi kwamba majeshi ya Waislamu hayawezi kupigana nao. Kwa hivyo, yote yanaleta mazingira ya kujadiliana nalo juu ya mradi muovu, suluhisho la dola mbili, ambalo ni usaliti kwa Mwenyezi Mungu, Mtume wake, na waumini.

Enyi watawala katika Ardhi za Waislamu:

Umbile la Kiyahudi sio watu wa vita na ushindi, badala yake ni kama Mwenyezi Mungu (swt) alivyosema,

[لَنْ يَضُرُّوكُمْ إِلَّا أَذًى وَإِنْ يُقَاتِلُوكُمْ يُوَلُّوكُمُ الْأَدْبَارَ ثُمَّ لَا يُنْصَرُونَ]

Maadui hawatakudhuruni ila ni maudhi tu. Na wakipigana nanyi watakupeni mgongo, na tena hawatanusuriwa. [Surah Aali Imran 3:111]. Kama munavyoona, waumini wachanga wanapigana na Mayahudi, kwa idadi ndogo na uwezo mdogo kuliko umbile la Kiyahudi, na bado umbile hili halijafanikiwa ushindi mpaka wa leo. Kwa hivyo, ikiwa majeshi ya Waislamu yatasonga, sio hata majeshi yote ya Waislamu, bali yale tu yanaoizunguka Palestina, au hata baadhi yake, basi umbile la Kiyahudi halingebakia hata athari yake kuonekana.

Palestina ni ardhi ya Kiislamu .. Umar al-Farooq (ra) aliifungua .. Salahudin Al-Ayubi akaikomboa .. na Abdul Hameed II akailinda. Sio ya kuuzwa. Haikubali kugawanywa kati ya watu wake, na wale awanaoikalia kimabavu, kuwafukuza watu wake kutoka kwake. Suluhisho lake sio suluhisho la dola mbili. Badala yake, suluhisho lake ni kama Mwenyezi Mungu Al-Aziz, Al-Jabbar alivyosema, na maneno Yake (swt) ndio suluhisho la kweli,

[وَاقْتُلُوهُمْ حَيْثُ ثَقِفْتُمُوهُمْ وَأَخْرِجُوهُمْ مِنْ حَيْثُ أَخْرَجُوكُمْ] “Na wauweni popote mwakutapo, na muwatoe popote walipo kutoeni.” [Surah Al-Baqarah 2:191].

Enyi Watawala katika Ardhi za Waislamu:

Je! Kuuwawa shahidi na kujeruhiwa kwa Waislamu elfu sitini huko Gaza haitoshi kwenu kuhamasisha majeshi kwa ajili ya kuwanusuru?! Mwenyezi Mungu (swt) amesema,

[وَإِنِ اسْتَنْصَرُوكُمْ فِي الدِّينِ فَعَلَيْكُمُ النَّصْرُ] “Lakini wakiomba msaada kwenu katika Dini, basi ni juu yenu kuwasaidia.” [Surah Al-Anfal 8:72].

Je! Kelele za watoto wa Gaza, vilio vya kina mama, uchungu wa waliofiwa, na vilio vya wanaume na wanawake wakongwe, havitoshi kwenu, kuhamasisha majeshi, katika kuwanusuru?!!

Je! Muendelezo wa mauaji, kunyofolewa kwa miili, na miguu, ya mashahidi, na umwagaji damu ya mashahidi na majeruhi kutoka chini ya vifusi na magofu, haitoshi kwenu kuwanusuru watu wa Gaza?!!

Je! Hamuoni? Je! Hamusikii? Je! Damu haichemki mishipa mwenu, kiasi kwamba muinusuru Gaza Hashim?!!

Je! Hamuoni aibu mbele ya Mwenyezi Mungu, Mtume wake, na waumini, kiasi kwamba msikataa kutoa Nusrah (kuwanusuru)? Hakika, Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema ukweli katika Hadith iliyopokewa na Al-Bukhari, ambaye alisema kwamba Adam alisimulia, kwamba Shu'bah kutoka kwa Mansour, ambaye alisema, nilimsikia Rab'i bin Hiraash akizungumza kutoka kwa Abu Masoud, kwamba Mtume (saw) amesema,

«إِنَّ مِمَّا أَدْرَكَ النَّاسُ مِنْ كَلَامِ النُّبُوَّةِ إِذَا لَمْ تَسْتَحْيِ فَاصْنَعْ مَا شِئْتَ» Hakika katika miongoni mwa waliyoyapata watu kutoka kwa maneno ya Mitume (as) ni, ‘ikiwa huoni haya basi fanya unavyotaka.’”  

Enyi Watawala katika Ardhi za Waislamu:

Tunatambua kuwa uaminifu wenu kwa wakoloni wa makafiri, haswa Marekani, na utiifu wenu kwao ndio unaokuzuieni kuinusuru Gaza na watu wake ili kuhifadhi viti vyenu vibovu. Mumesahau, au mumejisahaulisha, kwamba kwa kufanya hivyo hamupotezi tu Akhera yenu, munapoteza hata maisha ya dunia hii. Hakika, wakoloni makafiri watakutupeni kama konde za tende, na kuvunja viti vyenu, pindi wakimaliza kufikia malengo yao kupitia nyinyi. Kilichowatokea watangulizi wenu hapo awali, ni funzo kwenu, ikiwa tu mutatambua hilo.

Hakika, Mwenyezi Mungu Al-Qawwi, Al-Aziz, amesema kweli,

[أَفَلَمْ يَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَتَكُونَ لَهُمْ قُلُوبٌ يَعْقِلُونَ بِهَا أَوْ آذَانٌ يَسْمَعُونَ بِهَا فَإِنَّهَا لَا تَعْمَى الْأَبْصَارُ وَلَكِنْ تَعْمَى الْقُلُوبُ الَّتِي فِي الصُّدُورِ]

Je! Hawatembei katika ardhi ili wapate kuwa na nyoyo zao za kuzingatia, au masikio ya kusikilia? Kwani hakika si macho yanayo pofuka, lakini zinazo pofuka ni nyoyo ziliomo vifuani.” [Surah Al-Hajj 22:46].

Enyi Askari katika Majeshi ya Waislamu:

Imekuwa takriban miezi miwili tangu uvamizi wa kikatili wa Mayahudi ulipoanza dhidi ya watu wenu huko Gaza ... na licha ya mauaji ambayo umbile la Kiyahudi limeyafanya, na bado wanayafanya, ambayo wanawake, watoto, 'ulema na wazee waliuawa shahidi ... na licha ya uharibifu wa nyumba, mahospitali, Misikiti na taasisi, watawala wanakuzuieni kuwanusuru ndugu zenu huko Gaza, mukikaa na kunyamaza kimya! Je! Hamuogopi kukaa tuli, kiasi kwamba Ghadhabu kutoka kwa Mola wenu (swt) iwashukie juu yenu?

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَا لَكُمْ إِذَا قِيلَ لَكُمُ انْفِرُوا فِي سَبِيلِ اللهِ اثَّاقَلْتُمْ إِلَى الْأَرْضِ أَرَضِيتُمْ بِالْحَيَاةِ الدُّنْيَا مِنَ الْآخِرَةِ فَمَا مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فِي الْآخِرَةِ إِلَّا قَلِيلٌ * إِلَّا تَنْفِرُوا يُعَذِّبْكُمْ عَذَاباً أَلِيماً وَيَسْتَبْدِلْ قَوْماً غَيْرَكُمْ وَلَا تَضُرُّوهُ شَيْئاً وَاللهُ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ]

Enyi mlio amini! Mna nini mnapo ambiwa: Nendeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu, mnajitia uzito katika ardhi? Je, mmeridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera? Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha na ya Akhera ni chache (38). Kama hamwendi atakuadhibuni adhabu chungu, na atawaleta watu wengine, wala nyinyi hamtamdhuru chochote. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu (39).” [Surah At-Tawbah 9:38-39].

Je, hamutamani moja ya matendo mema mawili [ushindi au shahada]?

[يَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَيُدْخِلْكُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِنْ تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ وَمَسَاكِنَ طَيِّبَةً فِي جَنَّاتِ عَدْنٍ ذَلِكَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ * وَأُخْرَى تُحِبُّونَهَا نَصْرٌ مِنَ اللهِ وَفَتْحٌ قَرِيبٌ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ]

Atakusameheni dhambi zenu, na atakutieni katika Mabustani yapitiwayo na mito kati yake, na maskani nzuri nzuri katika Bustani za milele. Huko ndio kufuzu kukubwa. (12) Na kinginecho mkipendacho, nacho ni nusura itokayo kwa Mwenyezi Mungu, na ushindi ulio karibu! Na wabashirieni Waumini! (13).” [Surah As-Saf 61:12-13]. Je hamutamani hadhi katika dunia hii na kesho Akhera?

Enyi Askari katika Majeshi ya Waislamu:

Kimbilieni kuwanusuru ndugu zenu huko Gaza. Endapo watawala watasimama dhidi yenu, basi wakamateni kwa kila njia inayowezekana. Wanusuruni ndugu zenu katika Ardhi Iliyobarikiwa, na mufanye kuwe ni kushindwa kukubwa kwa umbile la Mayahudi kama vile kulivyokuwa kushindwa kukubwa kwa Makruseda huko Al-Quds Ash-Sharif, na pia kushindwa kukubwa kwa Wamongolia huko Ain Jalut ... na hivyo Palestina irudi kwa ujumla wake, kuwa makaazi ya Uislamu, kama ilivyokuwa hapo awali. Itapambwa tena kwa bendera ya Rayah ya Khilafah, bendera ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), kwani ni ardhi ya Isra'a na Miraj ... Ardhi Iliyobarikiwa na vilivyobariki viunga vyake .

[سُبْحَانَ الَّذِي أَسْرَى بِعَبْدِهِ لَيْلاً مِنَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ إِلَى الْمَسْجِدِ الْأَقْصَى الَّذِي بَارَكْنَا حَوْلَهُ لِنُرِيَهُ مِنْ آيَاتِنَا إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ]

“SUBHANA, Ametakasika aliye mchukua mja wake usiku mmoja kutoka Msikiti Mtukufu mpaka Msikiti wa Mbali, ambao tumevibariki vilivyo uzunguka, ili tumuonyeshe baadhi ya Ishara zetu. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia na Mwenye kuona.” [Surah Al-Israa 17:1].

Jitokezeni, Enyi Askari, muwanusuru ndugu zenu huko Gaza Hashim. Mnusuruni Mwenyezi Mungu (swt), Naye atakunusuruni.

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنْ تَنْصُرُوا اللهَ يَنْصُرْكُمْ وَيُثَبِّتْ أَقْدَامَكُمْ * وَالَّذِينَ كَفَرُوا فَتَعْساً لَهُمْ وَأَضَلَّ أَعْمَالَهُمْ * ذَلِكَ بِأَنَّهُمْ كَرِهُوا مَا أَنْزَلَ اللهُ فَأَحْبَطَ أَعْمَالَهُمْ]

“Enyi mlio amini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu naye atakunusuruni na ataithibitisha miguu yenu. Na walio kufuru, basi kwao ni maangamizo, na atavipoteza vitendo vyao. Hayo ni kwa sababu waliyachukia aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, basi akaviangusha vitendo vyao.” [Surah Muhammad 47:7-9].

H. 20 Jumada I 1445
M. : Jumatatu, 04 Disemba 2023

Hizb-ut-Tahrir

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu