Jumamosi, 10 Dhu al-Qi'dah 1445 | 2024/05/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Wito kutoka Ardhi Iliyobarikiwa kwenda kwa Ummah wa Kiislamu na Majeshi Yake

(Imetafsiriwa)

Enyi Majeshi ya Kiislamu, Majenerali, Maafisa na Askari:

Kutoka Msikiti wa Al-Aqsa na katikati ya vifusi vya Gaza Hashem, tunakuiteni kwa wito wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

  [يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَا لَكُمْ إِذَا قِيلَ لَكُمُ ‌انْفِرُوا فِي سَبِيلِ اللهِ اثَّاقَلْتُمْ إِلَى الْأَرْضِ أَرَضِيتُمْ بِالْحَيَاةِ الدُّنْيَا مِنَ الْآخِرَةِ فَمَا مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فِي الْآخِرَةِ إِلَّا قَلِيلٌ]   

“Enyi mlio amini! Mna nini mnapo ambiwa: Nendeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu, mnajitia uzito katika ardhi? Je, mmeridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera? Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha na ya Akhera ni chache.” [Surat At-Tawba:38].

Na tunakuonyeni kwa maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[إِلَّا تَنْفِرُوا يُعَذِّبْكُمْ عَذَاباً أَلِيماً وَيَسْتَبْدِلْ قَوْماً غَيْرَكُمْ وَلَا تَضُرُّوهُ شَيْئاً وَاللهُ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ]

“Kama hamwendi atakuadhibuni adhabu chungu, na atawaleta watu wengine, wala nyinyi hamtamdhuru chochote. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.” [Surat At-Tawba:39]. Mujahidina madhubuti wanapigana kwenye uwanja wa vita kwa dhamira na azma, huku adui muoga akishambulia kutoka mbali kwa ndege zao na mizinga, wakiharibu nyumba, wakiwa na nia ya kuua wanawake, watoto, na vikongwe. Mnasubiri nini?

Tuambieni, kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ni kipi kinachokuchocheeni shauku ya jihad katika njia ya Mwenyezi Mungu?

Tuambieni, kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ni lini tutaviona vikosi na majeshi yenu katika nyua za Msikiti wa Al-Aqsa?!

Watawala wahalifu, wasaliti wanasisitiza kugeuza matendo ya Mujahidina kuwa udhalilifu, usaliti na kushindwa. Ushujaa wa jeshi la Misri katika mwezi wa Ramadhan (Oktoba) uligeuzwa na msaliti Sadat kuwa uhaini mkubwa. Ikiwa majeshi ya Waislamu yatapuuza katika kunusuru Msikiti wa Al-Aqsa na mujahidina katika Ardhi Iliyobarikiwa, ni khiyana iliyopitiliza. Ni msaada wa moja kwa moja kwa umbile la Kiyahudi na kuwapa tamkini wasaliti kugeuza ushujaa kuwa khiyana mpya dhidi ya utakatifu wa Safari ya Usiku ya Mtume (saw) (Isra na Mi'raj). Je, mtawaacha mujahidina uwanjani peke yao na kubakia ndani ya kambi zenu huku mkiwa mumeshindwa na kujisalimisha?

Waharibifu wametangaza kizuizi kamili na kukata maji, mafuta, chakula na vifaa vya matibabu kutoka Ukanda wa Gaza, kwa hivyo mnafanya nini?

Je, mtawaacha watu wa Gaza peke yao katika makabiliano haya ya kishujaa na kuwa washirika wa Mayahudi katika kuwaua?! Au mtaitikia wito wa kifahari wa kumnusuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake, ili msiache jiwe juu ya jiwe kwa ajili ya umbile la Kiyahudi?

Mujahidina katika njia ya Mwenyezi Mungu wanataraji moja ya matokeo mema mawili: ushindi au kufa kishahidi (Shahada). Yeyote anayeuawa shahidi hakika amepata ushindi mkubwa, na watu wa Palestina wana mashahidi (shuhada’) wengi, lakini kinachokosekana ni nusra kutoka kwa majeshi ya Waislamu. Wallahi hili ndio mama wa maovu yote."

[Vipande vya kisimamo cha Hizb katika mji wa Ramallah - 12/10/2023]

Ewe Ummah wa Ahmad, Ummah bora kabisa ulioletwa kwa ajili ya Wanadamu:

Tunakuombeni huku uchungu ukitulemea nyoyoni mwetu. Je! haujafika wakati nyoyo zenu zinyenyekee mbele ya kumkumbuka Mwenyezi Mungu? Je, sio wakati sasa wa masikio yenu kusikia wito wetu? Je! haujafika wakati kwa majeshi yenu kuitikia wito wa Mwenyezi Mungu? Je! haujafika wakati kwenu kumnusuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake? Umbile hili katili litatoweka ndani ya saa moja ya siku. Mnasubiri nini?

Umbile hili bovu linaloendelea kuwepo katika Ardhi Iliyobarikiwa linadumishwa na watawala vibaraka wanaokufungeni na kukuzuieni kuikomboa Bayt Al-Maqdis. Je, mtafanya nini?

Enyi Majeshi ya Kiislamu... Enyi Makamanda, Maafisa na Askari:

Ukombozi wa Masra (kupaa) kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) ni heshima kubwa ambayo haipatikani na waoga au wanyonge. Ni heshima kubwa iliyohifadhiwa kwa ajili ya wanyoofu na watu wema pekee. Je, mtalivua vazi la fedheha na kuvaa vazi la heshima? Je, mtasimama, mkiwa mumeimarishwa na Dini yenu, ili kurudisha heshima ya Umma wa Kiislamu, au mtaendelea kudhalilika chini ya nira ya watawala vibaraka wanaokutiisheni na Ummah wenu kwenye aina mbalimbali za udhalilifu na uduni?"

Tunaomba nusra yenu ili kusimamisha Uislamu, kusimamisha Khilafah, na kuikomboa Bayt Al-Maqdis. Mkiitikia wito wa Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na Waumini, hakika mtapata ushindi mkubwa. Lakini mkiyumba, na mkaogopa, na mkashikamana na ardhi, basi mtafeli, na ni haki tu kwa Mwenyezi Mungu kukubadilisheni kwa watu wasiokuwa kama nyinyi.

[وَإِنْ تَتَوَلَّوْا يَسْتَبْدِلْ قَوْماً غَيْرَكُمْ ثُمَّ لَا يَكُونُوا ‌أَمْثَالَكُمْ]

“Na mkigeuka atawaleta watu wengine badala yenu, nao hawatakuwa kama nyinyi.” [Surah Muhammad:38].

Sisi, katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, tutabaki imara kwenye njia ya Haqq (Ukweli), hata kama madhalimu na makafiri watatuzunguka kutoka kila upande. Tunaubeba Uislamu, na nyoyo zetu zina amani na Iman. Wasio na maadili wanaweza kudhani sisi ni wanyonge, hatuna msaada wala nguvu, lakini wajue kwamba tunakabiliana nao kwa nguvu zisizo na kikomo, nguvu za Aziz Al-Qahhar (Mwenye Nguvu, Mwenye kushinda). Ama maadui zetu, hata nguvu zao zionekane ni kubwa kiasi gani, daima zitakuwa na mipaka na zitaporomoka mbele yetu kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu na uwezo wake.

Wacha Marekani ilete vyombo vyake vya kubebea ndege, na nchi zote za kikafiri zilete meli zao ili kulinda umbile la Kiyahudi. Kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu hawatawafaa kitu. Je, hamuamini maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu?

[إِنْ يَنْصُرْكُمُ اللهُ ‌فَلَا ‌غَالِبَ ‌لَكُمْ وَإِنْ يَخْذُلْكُمْ فَمَنْ ذَا الَّذِي يَنْصُرُكُمْ مِنْ بَعْدِهِ وَعَلَى اللهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ]

“Akikunusuruni Mwenyezi Mungu hapana wa kukushindeni, na akikutupeni ni nani, basi, baada yake Yeye ataye kunusuruni? Na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu.” [Aal-i-Imran:160]?!

Ndio, pindi Mwenyezi Mungu anapotunusuru, hakuna kushindwa kwetu. Vita hivi ni moja tu kati ya vingi, na hatujui ni kheri gani aliyotuandikia Mwenyezi Mungu. Hata hivyo, tuna uhakika kwamba Ardhi Iliyobarikiwa imekusudiwa ushindi wa wazi - Khilafah kwa njia ya Utume, pamoja na askari wake kushuka juu ya Bayt Al-Maqdis, kulipiza kisasi cha damu ya Mayahudi, kutekeleza ahadi ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na bishara njema za Mtume Wake (saw). Hakika Imam al-Bukhari amepokea kutoka kwa Abdullah bin Umar (radhi za Allah ziwe juu yao) kwamba amesema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) akisema...'"«تُقَاتِلُكُمْ الْيَهُودُ فَتُسَلَّطُونَ عَلَيْهِمْ، ثُمَّ يَقُولُ الْحَجَرُ: يَا مُسْلِمُ، هَذَا يَهُودِيٌّ وَرَائِي فَاقْتُلْهُ» “Mayahudi watapigana na nyinyi, nanyi mtapewa ushindi juu yao mpaka jiwe litasema: Ewe Muislamu, huyu hapa Yahudi (amejificha nyuma yangu); basi muuwe.” Kisha ardhi itaangazwa kwa nuru ya Uislamu na ushindi wa Mwenyezi Mungu Al-Qawee Al-Aziz Al-Hakeem (Mwingi wa Nguvu, Mwindi wa Uwezo, Mwingi wa Hekima).

Ewe Mwenyezi Mungu, ifanye kheri hii ujulikane kupitia kwetu, na uzipanue nyoyo za Waislamu kwayo. Utujalie mamlaka kutoka Kwako, ambayo tunaweza kuyatumia kuinusuru Dini Yako na kuinua neno lako. Sisi ni waja Wako na askari Wako, basi tujaalie tuwe miongoni mwa waja wako bora uliowateuwa kwa ajili ya kuinusuru Dini Yako na kunyanyua neno lako. Mwenyezi Mungu anatutosha, na hakika Yeye ndiye Mlinzi bora. Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote.

H. 25 Rabi' I 1445
M. : Jumanne, 10 Oktoba 2023

Hizb-ut-Tahrir
Ardhi ya Baraka-Palestina

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu