Ijumaa, 24 Shawwal 1445 | 2024/05/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan

H.  23 Sha'aban 1445 Na: 1445 / 35
M.  Jumatatu, 04 Machi 2024

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Njaa ya Kulazimishwa ya Mamia ya Maelfu ya Waislamu huko Rafah, Gaza, ni Kwa sababu ya Utepetevu wa Maafisa wa Kijeshi na Askari, Wanaosubiri Amri Ambazo Kamwe Hazitatoka

(Imetafsiriwa)

Enyi Maafisa na Askari wa Jeshi la Pakistan! Kumekuwa na vilio vya kutosha vya kuomba kutoka Gaza hadi kwenu! Kumekuwa na vilio vya kutosha kwa wale ambao wana masikio yanayosikia na nyoyo zinayohisi. Katika miezi hii mirefu, yenye uchungu na isiyotulia, tumesikia visingizio vyenu vyote vya kutokuchukua hatua. Hakuna udhuru wenu hata mmoja unaokubalika, kwa mujibu wa Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume wake (saw). Umma wa Kiislamu haukubali udhuru wenu wowote. Makumi ya maelfu ya Waislamu huko Gaza miili yao imepondwa na kusagwa na mabomu. Viumbe waoga zaidi ya watu wote wanabuni njia mpya za kuua kishahidi, kujeruhi na kukatwa vipande vipande. Mwenyezi Mungu (swt) amekuwajibisheni kwa Jihad, kuwanusuru Waislamu na ukombozi wa Ardhi Iliyobarikiwa. Mwenyezi Mungu (swt) hakuiweka faradhi yenu sharti la amri kutoka kwa vibaraka wa wakoloni. Amri kama hizo kamwe hazitakuja. Mwenyezi Mungu (swt) hakuiweka faradhi yenu sharti juu ya mipaka ya dola ya kitaifa, iliyochorwa na wakoloni ili kuugawanya na kuudhoofisha Umma wa Kiislamu.

Mwenyezi Mungu (swt) hatakubali visingizio vyenu vya kutochukua hatua, hali miili ya kaka zenu, dada zenu na watoto wenu imesagwa chini ya vifusi! Mwenyezi Mungu (swt) hatakubali udhuru kutoka kwenu, wakati njaa ya kulazimishwa iliwekwa kwa mamia ya maelfu ya kaka na dada zenu Waislamu. Wanakufa kwa njaa mitaani. Wanatafuta chakula kilichooza kwenye takataka chafu. Wanakusanya nyasi kupika ili kushibisha njaa. Wanalilia afueni kwa vijana na wazee wao. Wanazimia kwa njaa. Kwa hivyo, muitiko wenu umekuwa ni nini hadi sasa? Kutoa machozi, kutishia kujiuzulu, kupanga kustaafu na kuwalaani makamanda wenu! Kutochukua hatua kwenu kunakufanyeni washirika katika uhalifu wa uongozi wenu. Utiifu wenu wa wale wanaomuasi Mwenyezi Mungu (swt) unakupelekeeni kwenye adhabu yenu tu katika Moto wa Jahannam. Amesema Mwenyezi Mungu (swt):

[وَقَالُوا رَبَّنَا إِنَّا أَطَعْنَا سَادَتَنَا وَكُبَرَاءنَا فَأَضَلُّونَا السَّبِيلَا]

“Na watasema: Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tuliwat'ii bwana zetu na wakubwa wetu; nao ndio walio tupoteza njia.” [Surah Al-Ahzab 33:67].

Enyi Maafisa na Wanajeshi wa Jeshi la Pakistan! Hakika hawa watawala wa Waislamu na makamanda wa kijeshi ndio wahalifu wabaya zaidi kuliko wote. Wao ndio vinara wa nchi za Magharibi katika vita vyake vya msalaba dhidi ya Uislamu na Waislamu. Hao ndio wabadilishanaji wa Kibla cha Kwanza, Al-Masjid Al-Aqsa uliobarikiwa, ili kuokoa viti vyao vibovu vya enzi. Ama nyinyi ni walinzi na wasaidizi wa watawala hawa na makamanda wa kijeshi. Ni kutokuchukua hatua kwenu ndiko kulikowezesha makamanda wenu wa kijeshi kushirikiana na Wamarekani, kuwapa uhuru Mayahudi kwa miezi yote hii. Kwa nini adui zenu hawakuogopini? Wasaliti wanawezaje kukutegemeeni? Je, hamuna hata baadhi ya uanaume wa yule askari kafiri wa Marekani, aliyejichoma moto, akipinga uongozi wake wa kijeshi? Je, mpaka lini mtapuuza amri ya Mwenyezi Mungu (swt) ambaye kwa neema Yake mnapumua, mnakunywa na kula? Mwenyezi Mungu (swt) anasema,

[وَمِنَ النَّاسِ مَن يَعْبُدُ اللَّهَ عَلَى حَرْفٍ فَإِنْ أَصَابَهُ خَيْرٌ اطْمَأَنَّ بِهِ وَإِنْ أَصَابَتْهُ فِتْنَةٌ انقَلَبَ عَلَى وَجْهِهِ خَسِرَ الدُّنْيَا وَالْآخِرَةَ ذَلِكَ هُوَ الْخُسْرَانُ الْمُبِينُ]

“Na katika watu wapo wanao muabudu Mwenyezi Mungu kwa ukingoni. Ikimfikia kheri hutulia kwayo, na ukimfikia msukosuko hugeuza uso wake. Amekhasiri dunia na Akhera; hiyo ndiyo khasara iliyo wazi.” [Surah Al-Hajj 22:11].

Mpaka lini tutakusikieni mkijitetea kwa kusema, “Nifanye nini peke yangu?” Mnawezaje kusema hivyo, wakati maafisa na askari wengi waaminifu walio karibu nanyi, wote wanakubaliana nanyi? Vipi mtasema hivyo, wakati nanyi ni watoto wa Waislamu wanaompenda Mwenyezi Mungu (swt), Mtume wake (saw) na Waumini? Kwa hiyo, basi, ni jinsi gani kikundi kidogo cha makamanda wafisadi na wasaliti waweza kukuzuieni kujikusanya kwa ajili ya ushindi na shahada? Je, hamtapanga na kuratibu pamoja na Waislamu waaminifu, kuondoa vikwazo vyote katika njia ya utiifu kwa Mwenyezi Mungu (swt)? Je, mmetanguliza maisha ya dunia kuliko maisha ya Akhera, kama walivyofanya hao makamanda wasaliti mnaowalaani? Basi onyweni kwamba Mwenyezi Mungu (swt) amesema:

[قُلْ إِن كَانَ آبَاؤُكُمْ وَأَبْنَآؤُكُمْ وَإِخْوَانُكُمْ وَأَزْوَاجُكُمْ وَعَشِيرَتُكُمْ وَأَمْوَالٌ اقْتَرَفْتُمُوهَا وَتِجَارَةٌ تَخْشَوْنَ كَسَادَهَا وَمَسَاكِنُ تَرْضَوْنَهَا أَحَبَّ إِلَيْكُم مِّنَ اللّهِ وَرَسُولِهِ وَجِهَادٍ فِي سَبِيلِهِ فَتَرَبَّصُواْ حَتَّى يَأْتِيَ اللّهُ بِأَمْرِهِ وَاللّهُ لاَ يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ]

“Sema: Ikiwa baba zenu, na wenenu, na ndugu zenu, na wake zenu, na jamaa zenu, na mali mliyo yachuma, na biashara mnazo ogopa kuharibika, na majumba mnayo yapenda, ni vipenzi zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Jihadi katika Njia yake, basi ngojeni mpaka Mwenyezi Mungu alete amri yake. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wapotovu.” [Surah At-Tauba 9:24]

Enyi Maafisa na Wanajeshi wa Jeshi la Pakistan! Umma umesimama kwenye njia panda. Ima kuwe na adhabu kali kutoka kwa Mola wetu Mlezi (swt), au mvua nyingi ya baraka za Mwenyezi Mungu (swt). Inategemea matendo yenu, juu ya wengine wote. Amesema Mwenyezi Mungu (swt) amesema:

[إِلاَّ تَنفِرُواْ يُعَذِّبْكُمْ عَذَابًا أَلِيمًا وَيَسْتَبْدِلْ قَوْمًا غَيْرَكُمْ وَلاَ تَضُرُّوهُ شَيْئًا وَاللّهُ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ]

“Kama hamwendi atakuadhibuni adhabu chungu, na atawaleta watu wengine, wala nyinyi hamtamdhuru chochote. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.” [At-Tauba, 9:39]. Nyinyi ndio mnaoweza kuwafundisha wanyama hawa wa Kizayuni funzo ambalo wao wala wakoloni wanaowaunga mkono hawatasahau. Nyinyi ndio mnaoweza kulipizia kisasi watoto, dada na kaka wasio na hatia na kutia hofu katika moyo wa kila dhalimu. Nyinyi ndio mnaoweza kuitakasa Ardhi Iliyobarikiwa kutokana na uchafu wa umbile la Kiyahudi.

Jeshi lenu lote, au hata sehemu yake, linatosha kutwaa heshima ya kuikomboa Palestina. Ummah wote utasimama nyuma yenu. Wanaume wote wa Kiislamu wenye uwezo watasimama karibu nanyi. Basi mtangulizeni Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume Wake (saw) mbele yenu. Viti vya watawala, mikono miovu ya Marekani katika ardhi zetu, vitang'olewa. Kwa kukatwa mikono yake, Marekani basi itaweza kutazama bila msaada kutoka mbali, ikitenganishwa na bahari. Marekani ina hofu kwamba kampeni ya Mayahudi ya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu ndani ya Ramadhan itasababisha kupinduliwa kwa watawala hawa. Igeuzeni hofu hii kuwa uhalisia, ili macho yao yakodoke kwa hofu. Ipeni Nusrah yenu Hizb ut Tahrir kwa ajili ya kusimamisha tena Khilafah kwa Njia ya Utume. Hizb ut Tahrir inangojea majibu yenu, ikiwa imejiandaa kikamilifu na mradi kamili wa kisiasa. Je, mtaikaribisha Ghadhabu ya Mwenyezi Mungu (swt) ikutembeleeni kwa kutochukua hatua zaidi, au mtajitahidi kupata baraka zake katika Dunia hii na kesho Aakhira?

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Pakistan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan
Address & Website
Tel: 
https://bit.ly/3hNz70q

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu