Jumapili, 11 Dhu al-Qi'dah 1445 | 2024/05/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Katika Vita dhidi ya Hizb ut Tahrir, Urusi Imechukua Njia ya Uzbekistan

(Imetafsiriwa)

Kuokoa adhabu isiyo ya haki kwa kuulingania Uislamu pamoja na Hizb ut Tahrir, Hafizov Asgat aliongezewa miaka mengine 10 gerezani hadi kufikia miaka 19. Mnamo tarehe 05 Agosti 2021, Mahakama ya Kijeshi ya Wilaya ya Kati ilitangaza hukumu dhidi ya mwanachama wa Hizb ut Tahrir Hafizov Asgat, anayeshtakiwa kwa Sehemu ya 2 ya kifungu cha 205.5 na Sehemu ya 1 ya kifungu cha 205.1 cha Sheria ya Jinai kwa kuandaa shughuli na kushiriki katika shirika "Hizb ut Tahrir ”. Kwa miaka 13, ambayo bado ilibidi aondoke, mahakama iliongeza miaka mingine 10. Kwa jumla, pamoja na hukumu iliyotangulia, mfumo wa mahakama wa Urusi ulimhukumu kifungo cha miaka 29, ambayo tayari ametumikia miaka 6. Kwa hivyo, Urusi hutumia uzoefu wa huduma maalum za Uzbekistan - kila wakati kipindi cha awali kinapomalizika, huongeza kipya kwa wanachama wa Hizb ut Tahrir.

Kumbuka kwamba Asgat Khafizov alifungwa na kuzuiliwa kutoka 10/14/2014 kwa mashtaka ya uhalifu chini ya Sehemu ya 1 ya kifungu cha 205.5 na Sehemu ya 1 ya Kifungu cha 282.2 cha Kanuni ya Jinai ya Shirikisho la Urusi, kwa kuwa mratibu wa shughuli za shirika lenye msimamo mkali na shirika la kigaidi wakati huo huo, kisha, mnamo 08/12/2017 alihukumiwa na Mahakama ya Kijeshi ya Wilaya ya Privolzhsky miaka 19 na miezi 2 gerezani na kutumikia kifungo katika korokoro kali ya serikali.

Na hii ni mbali na kesi ya kwanza na sio kesi pekee ya ukiukaji sheria kama huo wa mashini ya ukandamizaji ya Urusi, inayowakilishwa na mahakama, vyombo vya upelelezi, na huduma maalum. Hili lilijaribiwa kwa mara ya kwanza mnamo 2017. Mwanachama wa Hizb ut Tahrir Rinat Galiullin, baada ya kutumikia kifungo cha miaka 5 gerezani kwa kesi ya jinai ya kuzuliwa, alipaswa kuachuliwa mnamo Julai 28, 2017 kutoka hospitali salama Nambari 3 ya jimbo la Saratov. Lakini wakati alipokuwa akiondoka korokoroni, aliwekwa kizuizini na FSB mbele ya mkewe na binti yake wa miaka 10. Ilibadilika kuwa kesi iliyofunguliwa dhidi yake chini ya Sehemu ya 2 ya kifungu cha 205.5 ya Kanuni ya Jinai (kushiriki katika shughuli za shirika la kigaidi). Uamuzi wa kuanzisha kesi ya jinai ulisema kwamba Galiullin, wakati alipokuwa kizuizini, alifanya "mazungumzo ya pamoja na ya mtu binafsi" na wafungwa na kujaribu kuwashirikisha katika shughuli za Hizb ut Tahrir.

Kwa hivyo, viongozi wa Urusi wanataka kukandamiza shughuli za shirika hili kwa kuwatishia wanachama wake na magereza, ambayo kwa wengi tayari yamekuwa ya maisha ya muda mrefu, wakijua kwamba chama na wanachama wake hawana uhusiano wowote na ugaidi, mashambulizi ya kigaidi au kitu chochote mithili yake. Idadi inayoongezeka ya mawakili na wanaharakati wa haki za binadamu, waandishi wa habari na wanasiasa wanafahamu kuwa marufuku ya Hizb ut Tahrir sio chochote ila uamuzi wa kisiasa tu, iliyo sababisha mnamo 2003 Mahakama Kuu ya Shirikisho la Urusi kuamua kulitambua shirika hili kama la kigaidi.

Mwenyezi Mungu (swt) katika Quran asema:

[يُرِيدُونَ لِيُطْفِئُوا نُورَ اللَّهِ بِأَفْوَاهِهِمْ وَاللَّهُ مُتِمُّ نُورِهِ وَلَوْ كَرِهَ الْكَافِرُونَ]

“Wanataka kuizima nuru ya Mwenyezi Mungu kwa vinywa vyao. Na Mwenyezi Mungu atakamilisha nuru yake ijapo kuwa makafiri watachukia.” [TMQ 61:8].

Imeandikwa kwa Ajili ya Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir na
Shaikhetdin Abdullah

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu