Jumatano, 29 Shawwal 1445 | 2024/05/08
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Je, Watawala wamefanya nini hasa, zaidi ya Kuruhusu Tuchuruzike Damu?

(Imetafsiriwa)

Matukio ya kutisha huko Gaza yameifanya dunia nzima kuamka na kufikiria. Kwa mara ya kwanza, inaonekana kuna utambuzi wa kimataifa wa ukweli kwamba watawala ndani ya mfumo huu wametufelisha sisi sote. Wamejaribu kutuambia kwamba wajibu wa watawala ni kulinda maslahi ya raia wao, kufuata utawala wa sheria na kuhakikisha kuwa sauti yetu inabebwa kupitia sera za serikali - lakini huu ni uwongo waziwazi.

Na tukitazama matukio ya mwaka uliopita inatuonyesha ni kwa kiasi gani watawala watakwenda kulinda maslahi yao wenyewe na yale ya wafuasi wao. Wanakwenda mbali na kupuuza umwagikaji wa damu wakati mauaji ya halaiki yanafanyika mbele yao, wanashindwa kuwalinda watu wao kote ulimwenguni. Hata wakati machaguo yao yanagongana nayo, au kuonyesha kupuuza waziwazi, maadili na kanuni walizotumia kupata uhalali na ambazo ndizo zilizowaingiza madarakani.

Damu ya Waislamu inamwagwa.

Kote katika nchi za Kiislamu, watu wanateseka kwa namna moja au nyingine. Utawala wa Ubepari wa kisekula, katika ardhi zilizowahi kutawaliwa na Uislamu umewaacha watu kwenye huruma ya michezo ya kisiasa. Kwa hiyo wanaishi katika hali ya kutokuwa na usalama mara kwa mara, huku damu yao ikimwagwa katika mashambulizi mara kwa mara. Mifano michache tu ya mwaka huu, mbali na Gaza ni pamoja na;

- Hali nchini Myanmar ni ya kabla ya 2023. Mzozo katika eneo hilo ulianza tangu Vita vya Pili vya Dunia, lakini mapinduzi ya kijeshi ya hivi majuzi mnamo 2021 yalisababisha “mchakato wa kimfumo” wa kuwaondoa mamia ya maelfu ya Warohingya kutoka Myanmar “kupitia vitendo vya mara kwa mara vya udhalilishaji na unyanyasaji”.

- Nchini India, kumekuwa na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya Waislamu - Shirika la Hindutva Watch liliripoti kwamba zaidi ya matukio 250 ya chuki dhidi ya Waislamu yalitekelezwa nchini India katika nusu ya kwanza ya 2023.

- Halafu huko Kashmir, kuna uvamizi unaoendelea wa vikosi vya India. Mwaka huu, kulitokea makabiliano kati ya vikosi vya usalama vya India na wanamgambo katika wilaya ya Anantnag ya Jammu na Kashmir, India.

Lakini je, ni Waislamu pekee wanaoteseka?

Hapana, sivyo. Hakika kuna ajenda ya kuwakandamiza Waislamu na Uislamu. Lakini Mfumo wa Kibepari unafichuliwa kote ulimwenguni.

Katika Ulimwengu wa Magharibi, watawala wamejaribu kutumia kanuni kama vile ‘haki ya kupiga kura’, ‘haki ya kuandamana’, ‘Vyombo vya habari, vya uwazi na uhuru’ ili kuwafurahisha wananchi wake. Kuwaambia kwamba wakifanya kazi ndani ya mfumo, sauti zao zitasikika na matatizo ndani ya mfumo yatatatuliwa. Matukio ya mwaka uliopita yanaonyesha jinsi hili ni uwongo.

• Nchini Marekani, ghasia za bunduki ni suala kubwa. Mwaka wa 2023 ulikuwa katika kasi ya kuvunja rekodi ya mauaji ya watu wengi. Licha ya maandamano na harakati, kundi la kushawishi bunduki bado halijawajibishwa.

• Vurugu za polisi ziliendelea nchini Marekani. Mnamo 2023, polisi waliwaua zaidi ya watu 1,200.

• Nchini Ufaransa, pindi watu walipofanya maandamano na kukutana na bunduki za maji na mabomu ya machozi kwa nyakati tofauti.

• Kufuatia migomo kote Uingereza, serikali ilipitisha sheria ya kupinga mgomo.

Hii ni mifano michache tu ya matatizo katika Ulimwengu wa Magharibi, kuna mengi zaidi hasa yanayohusiana na uchumi. Katika sehemu nyingine za dunia, tunaweza kuona matatizo ambayo yamejitokeza kama matokeo ya moja kwa moja ya matatizo ya mfumo ambayo yanawaathiri Waislamu pamoja na nchi zisizo za Kiislamu.

Kumeenea Ukosefu wa Utulivu wa Kisiasa.

Baada ya miaka ya arubaini, wazo la kujitawala na utawala wa kidemokrasia likawa kipengele kinachofafanua serikali kote ulimwenguni. Lakini urithi wa ukoloni wa gawanya utawale, pamoja na kuendelea kuingiliwa na mamlaka ya ukoloni mamboleo, kumezua hali ambapo migogoro na ukosefu wa utulivu ni jambo la kawaida katika idadi ya nchi duniani kote. Makundi katika nchi mbalimbali yanagombea madaraka na utawala, bila kujali madhara kwa wananchi.

Mwaka huu tu, tunayo mifano kadhaa ikijumuisha:

• Vurugu za hivi majuzi za kisiasa nchini Nigeria kati ya wanamgambo wa eneo hilo.

• Vurugu za kisiasa za uhalifu nchini Mexico, wakati ushajiishaji wa sheria unajaribu kuzuia vurugu zinazohusiana na dawa za kulevya kati ya mashirika ya uhalifu na vikosi vya serikali.

• Ukosefu wa serikali kuu nchini Haiti, huku magenge yakidhibiti sehemu kubwa ya mji mkuu wa Port-au-Prince. Wanateseka kutokana na mambo kadhaa ya chakula na afya.

• Mzozo unaoendelea wa mpaka kati ya Armenia na Azberjan, ulioanza mwaka wa 2021, kuhusu eneo linalozozaniwa.

• Vifo na kuhamishwa kwa raia katika jimbo la Blue Nile kusini mashariki mwa Sudan, kutokana na migogoro ya ardhi.

• Kulikuwa na mapigano kuhusu eneo linalozozaniwa la Abyei nchini Sudan Kusini kati ya Twic Dinka na wanamgambo wa Misseriya dhidi ya wanamgambo wa Ngok Dinka. Huku mzozo ukiwa umemalizika rasmi, bado kungali na mashambulizi ambayo hutokea mara kwa mara.

• Mgogoro unaoendelea kati ya Jeshi la Kitaifa la Somaliland na vikosi vya SSC-Khatumo vya Dhulbahante huko Las Anod, mji mkuu wa eneo la Sool. Mapigano yalizuka Februari 6 baada ya vikosi vya usalama vya Somaliland kufanya msako mkali dhidi ya maandamano ya raia. Siku 2 baadaye, Garad mkuu wa Dhulbahante, alitangaza nia ya kujitenga na kuungana tena na Serikali ya Shirikisho ya Somalia.

• Shambulizi la droni la Wanajeshi wa Nigeria lilipiga kijiji kimakosa, na kuua takriban raia 88. Walidhani walikuwa wanalenga majambazi.

Hakuna wa kuwazuia raia kuwa katika huruma ya michezo ya Kimataifa Tunawatazama watawala wakikaa pamoja na kubishana juu ya kile ‘wanachoamini kuwa ni sahihi’, wakisikiliza huku wakijaribu kuwaaminisha raia wao kwamba wanatimiza ‘wajibu wa kimaadili’ wa kuilinda dunia dhidi ya ‘magaidi’. Lakini michezo ya kimataifa juu ya rasilimali na maslahi ya kimkakati ni sehemu inayojulikana, inayokubalika ya mfumo huu. Na watawala wanatumia tu maneno kama ‘majukumu ya kimaadili’ na ‘ugaidi’ kuhalalisha kwa nini raia ndio wanaolipa gharama za michezo kwa miili na mali zao. - Ukrainia Tunajua kuhusu Vita vya Ukraini-Urusi, na matokeo yake yanaonekana kote ulimwenguni. Ilikuwa ni vita ambayo ilipiganwa juu ya utawala wa Marekani katika eneo hilo, na hofu ya Magharibi ya kupoteza ufikiaji wao wa eneo ambalo lilikuwa na manufaa ya kimkakati na rasilimali. - Yemen Mapigano kati ya waasi wa Houthi na muungano wa Saudia unaounga mkono serikali ya Yemen inayotambulika kimataifa yamesababisha theluthi mbili ya watu, au Wayemeni milioni 21.6, kuhitaji msaada. Milioni tano wako katika hatari ya njaa, na mlipuko wa kipindupindu umeathiri zaidi ya watu milioni moja. - Syria Vita nchini Syria ni endelevu, ikisema zaidi ya muongo mmoja uliopita. Ingawa inarejelewa kuwa vita vya wenyewe kwa wenyewe, kumekuwa na ushiriki mkubwa kutoka kwa mataifa ya kigeni - hapo awali kutoka NATO na GCC, Iran na Urusi. Hivi sasa, kuna ushiriki mkubwa kutoka Uturuki katika eneo hilo. Na wakati vita vya wenyewe kwa wenyewe vilisemekana kuzuka dhidi ya Bashar al-Assad- bado yuko madarakani. Na matokeo yake, kuna Wasyria milioni 13 waliokimbia makazi yao, na zaidi ya watu elfu 500 wa Syria walikufa. - Guyana Kuna hali inayotengenezwa huko - Akiba kubwa ya mafuta iligunduliwa baharini mnamo 2010 na kisha, Guyana ikatoa leseni za kuchimba visima katika maji yanayozozaniwa mwaka huu. Kwa upande wake, Venezuela ilitangaza nia ya kuchukua udhibiti wa eneo hilo, kufanya kura ya maoni na kuchukua hatua za kushinikiza madai yake juu ya eneo hilo. Katika kukabiliana na hatua za Venezuela, nchi nyingine ziliunga mkono msimamo wa Guyana ikiwa ni pamoja na Brazil, Uingereza na Marekani. Brazil ilituma wanajeshi kwenye mpaka wake na eneo hilo na Marekani ilifanya mazoezi ya kijeshi na Guyana. - Gaza Kisha bila shaka, tuna mambo ya kutisha ambayo yanajitokeza huko Gaza na Ukingo wa Magharibi. Kwa kukubalika na kuungwa mkono kimataifa kwa uvamizi haramu wa Israeli, vitendo vyao vya mauaji ya halaiki, na habari za mpango mpya wa IMEC.

Hakuna wa kuwazuia raia kuwa katika huruma ya michezo ya Kimataifa

Tunawatazama watawala wakikaa pamoja na kubishana juu ya kile ‘wanachoamini kuwa ni sahihi’, wakisikiliza huku wakijaribu kuwakinaisha raia wao kwamba wanatimiza ‘wajibu wa kimaadili’ wa kuilinda dunia dhidi ya ‘magaidi’. Lakini michezo ya kimataifa juu ya rasilimali na maslahi ya kimkakati ni sehemu inayojulikana, inayokubalika ya mfumo huu. Na watawala wanatumia tu maneno kama ‘majukumu ya kimaadili’ na ‘ugaidi’ kuhalalisha kwa nini raia ndio wanaolipa gharama za michezo kwa miili na mali zao.

- Ukraine Tunajua kuhusu Vita vya Ukraine-Urusi, na matokeo yake yanaonekana kote ulimwenguni. Ilikuwa ni vita wazi ambavyo vilipiganwa juu ya utawala wa Marekani katika eneo hilo, na hofu ya Magharibi ya kupoteza njia yao ya eneo ambalo lilikuwa na manufaa ya kimkakati na rasilimali.

- Yemen Mapigano kati ya waasi wa Houthi na muungano wa Saudia unaounga mkono serikali ya Yemen inayotambulika kimataifa yamesababisha thuluthi mbili ya watu, au Wayemeni milioni 21.6, kuhitaji msaada. Milioni tano wako katika hatari ya njaa, na mlipuko wa kipindupindu umeathiri zaidi ya watu milioni moja.

- Syria Vita nchini Syria ni endelevu, kwa zaidi ya muongo mmoja uliopita. Huku vikiitwa kuwa ni vita vya wenyewe kwa wenyewe, kumekuwa na ushiriki mkubwa kutoka kwa dola za kigeni - hapo awali kutoka NATO na GCC, Iran na Urusi. Hivi sasa, kuna ushiriki mkubwa kutoka Uturuki katika eneo hilo. Na huku vita vya wenyewe kwa wenyewe vikisemekana kuzuka dhidi ya Bashar al-Assad- bado angali madarakani. Na matokeo yake, kuna Wasyria milioni 13 waliokimbia makaazi yao, na zaidi ya watu elfu 500 wa Syria walikufa.

- Guyana Kuna hali inayotengenezwa huko - Akiba kubwa za mafuta iligunduliwa baharini mnamo 2010 na kisha, Guyana ikatoa leseni za kuchimba visima katika maji yanayozozaniwa mwaka huu. Kwa upande wake, Venezuela ilitangaza nia ya kuchukua udhibiti wa eneo hilo, kufanya kura ya maoni na kuchukua hatua za kushinikiza madai yake juu ya eneo hilo. Katika kukabiliana na hatua za Venezuela, nchi nyingine ziliunga mkono msimamo wa Guyana ikiwa ni pamoja na Brazil, Uingereza na Marekani. Brazil ilituma wanajeshi kwenye mpaka wake na eneo hilo na Marekani ilifanya mazoezi ya kijeshi na Guyana.

- Gaza Kisha bila shaka, tuna mambo ya kutisha ambayo yanajitokeza huko Gaza na Ukingo wa Magharibi. Kwa kukubalika na kuungwa mkono kimataifa kwa uvamizi haramu wa Israel, vitendo vyao vya mauaji ya halaiki, na habari za mpango mpya wa IMEC.

Hakuna mtu wa kuchukua jukumu wazi na kuwalinda waliohamishwa

Pamoja na mizozo na michezo ya kimataifa, kunakuja kuenea kwa watu wengi waliokosa. Na bado haijulikani ni nani anayepaswa kuwajibika kwa raia. Ikiwa uhamishwaji huo wa makao ni wa ndani, serikali itasema kwamba ni kwa sababu ya ukosefu wa rasilimali za kuwahudumia. Ikiwa uhamishwaji huo makao ni wa nje, mataifa mengine hayako tayari kuwajibikia kwa muda mrefu. Ingawa kuna mjadala wa haki za wakimbizi, hakuna dola hata moja inayowajibika kuwatunza wakimbizi.

Kulingana na makadirio ya UNHCR, watu milioni 117.2 watalazimika kuyahama makaazi yao kwa lazima au kutokuwa na utaifa mnamo 2023.

Baadhi ya mifano maalum ya serikali ni pamoja na:

- Wakimbizi wa Afghanistan wakati serikali ya Pakistan ilipoamua kuwafukuza wakimbizi wanaoishi ndani ya mipaka yao na Afghanistan ilisema kuwa hawakuwa na rasilimali za kuwatunza zaidi ya wakimbizi milioni 1 ambao walikuwa wakirudishwa kwao kwa nguvu.

- Zaidi ya Waeritrea elfu 500 - karibu 15% ya idadi ya watu nchini - wamehamishwa nje ya nchi kwa sababu ya ghasia zinazoendelea na ukosefu wa utulivu wa kisiasa.

- Mgogoro unaoendelea nchini CAR umesababisha zaidi ya wakimbizi 750 elfu kusajiliwa mwaka wa 2023.

- Kulikuwa na ongezeko la wakimbizi wa Somalia mwaka huu - na zaidi ya wakimbizi 814 elfu kurekodiwa kufikia katikati ya 2023.

- Congo ina idadi kubwa zaidi ya watu waliokimbia makao yao barani Afrika.

- Kuna zaidi ya Waislamu milioni 1 wa Rohingya wasio na utaifa.

- Kuna zaidi ya Wasudan Kusini milioni 4 ambao wamelazimika kutoka makwao.

Ulimwengu unaoendeshwa na Ubepari wa kisekula, ni mahali pabaya sana pa kuishi. Vurugu za kisiasa, matatizo ya kiuchumi, machafuko ya kijamii ni jambo la kawaida. Tumeanza kuamka lakini tunatakiwa kukesha. Watawala kote ulimwenguni wamejionyesha kuwa waongo tena na tena. Ni mara ngapi tutajiruhusu kudanganywa ili tuwaamini?

Yanayotokea Gaza yameleta mshtuko kote ulimwenguni. Na sasa wanajaribu kusafisha sura zao.

- kwa ‘misaada’ wanayotuma kwa Wapalestina, licha ya kuruhusu 80% ya miundombinu ya Gaza kubomolewa.

- Kwa mazungumzo 'yaliyovuja' ambayo yanashajiisha suluhisho la dola mbili.

- Huku simulizi za vyombo vya habari zikijaribu kuweka bayana mashambulizi yote dhidi ya Nethanyahu na serikali yake, matukio ya Gaza, matukio duniani kote, yalitokea kwa sababu watawala waliruhusu yatendeke. Kubadilisha sura moja katika uchaguzi- uchaguzi wowote-hakutabadilisha kitu. Kubadilisha sheria moja haitabadilisha chochote.

Mfumo mzima ndio tatizo. Tusipoubadilisha, dunia nzima itaendelea kuteseka. Khilafah haitawalinda Waislamu tu, katika muda wote wa utakaosimama Uislamu hapa duniani, pia itawalinda na kuwajali raia wasio Waislamu kwa namna ambayo Mfumo wa Kibepari haujaweza kufanya.

Amesema Mtume (saw):

«إِنَّمَا الْإِمَامُ جُنَّةٌ يُقَاتَلُ مِنْ وَرَائِهِ وَيُتَّقَى بِهِ فَإِنْ أَمَرَ بِتَقْوَى اللَّهِ وَعَدَلَ فَإِنَّ لَهُ بِذَلِكَ أَجْراً وَإِنْ أَمَرَ بِغَيْرِهِ فَإِنَّ عَلَيْهِ وِزْراً»

“Hakika Imam ni ngao (ulinzi) watu hupigana nyuma yake, na hujihami kwake. Akiamrisha uchaMungu na akafanya uadilifu basi kwake katika hilo ana ujira na akiamrisha kwa lisilokuwa hilo atabeba mzigo dhidi yake.”

Imeandikwa kwa Ajili ya Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir na
Fatima Musab
Mwanachama wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu