Je, Mnaweza Kubadilisha hadi Mfumo wa Dhahabu na Fedha Badala ya Kujidanganya kwa Kubaki kwenye Mfumo wa Fedha wa Kulazimishwa? (Imetafsiriwa)
- Imepeperushwa katika Yemen
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo siku ya Jumamosi, tarehe 20 Ramadhan 1445 H, sawia na 30/3/2024 M, Gavana wa Benki Kuu jijini Sana'a, Hashim Ismail, alifanya mkutano na waandishi wa habari, ambapo alitangaza kutolewa kwa sarafu mpya ya riyal 100 kuchukua nafasi ya noti ya riyal 100 iliyoharibika iliyotolewa naye. Matumizi ya sarafu mpya yalianza kutumika mnamo Jumapili, Ramadhan 21, 1445 H.