Matukio ya Kisiasa ya Hivi Majuzi nchini Yemen Yanaonyesha Nini?
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo Alhamisi, 28 Agosti, Waziri Mkuu wa Wizara ya Mabadiliko na Ujenzi, Ahmed Ghaleb Al-Rahwi, aliuawa, pamoja na mawaziri wengine tisa: Waziri wa Sheria na Haki za Binadamu Mujahid Ahmed Abdullah Ali; Waziri wa Uchumi, Viwanda na Uwekezaji Moeen Hashim Ahmed Al-Mahaqri; Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Rasilimali za Maji Radwan Ali Ali Al-Rubai; Waziri wa Mambo ya Nje na Wageni Jamal Ahmed Ali Amer; Waziri wa Umeme, Nishati na Maji Ali Seif Mohammed Hassan; Waziri wa Utamaduni na Utalii Ali Qasim Hussein Al-Yafei; Waziri wa Masuala ya Jamii na Leba Samir Mohammed Ahmed Bajaala; Waziri wa Habari Hashim Ahmed Abdul Rahman Sharaf Al-Din; na Waziri wa Vijana na Michezo Mohammed Ali Ahmed Al-Mawlid. Mawaziri wengine kadhaa bado wako katika hali mbaya na ya wastani, akiwemo Jalal Al-Ruwaishan, Naibu Waziri Mkuu wa Masuala ya Ulinzi na Usalama. Umbile la Kiyahudi limeeleza kuwa lilifanya shambulizi hilo, likiwalenga Waziri wa Ulinzi Mohammed Al-Atifi na Mkuu wa Majeshi Mohammed Abdul Karim Al-Ghamari.



