Jumatano, 16 Safar 1446 | 2024/08/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Serikali ya Jordan Kuanzisha Afisi ya NATO ni Uhalifu dhidi ya Palestina na Gaza na Usaliti kwa Umma wa Kiislamu

Huku Wamagharibi wakikata tamaa ya uwezo wa tawala vibaraka katika nchi za Kiislamu kuendelea kudhibiti na kutawala mambo, na uhakika wake kwamba Ummah unakaribia kuzifagilia mbali tawala hizi na kuziondoa, na hivyo kuondoa uwepo wao katika nchi zetu; kwa kuzingatia haya yote, hatua hii ilitoka kwa NATO, ili wao wenyewe waweze kusimamia utekelezaji wa mipango yao na kulinda maslahi yao katika ardhi zetu, na kulinda umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Kwa Shangwe na Nderemo ya Hali ya Juu, Bunge la Marekani Lilimkaribisha Muuaji wa Gaza!

Baada ya miezi kumi ya mauaji ya kila siku dhidi ya watu wa Gaza, ambayo yanatangazwa muda baada ya muda kwa sauti na picha za hali ya juu, kwa idadi, takwimu, ushuhuda na hukumu za mahakama... baada ya yote hayo, Bunge la Congress lilimpokea kiongozi wa Baraza la Vita huko Gaza, Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi Netanyahu, kwa karamu ya nderemo na shangwe kana kwamba yeye ni mmoja wa mashujaa wa watu wao. Sauti yao ya ndani ikisema: Tunataka kukupa ujira, Netanyahu, kwa kuwaua Waislamu wa Gaza kwa niaba yetu.

Soma zaidi...

Uchaguzi nchini Marekani na Uingereza Unashindana katika Kulenga Uislamu na Waislamu

Katikati ya uungaji mkono wa Marekani na Uingereza kwa mauaji yanayofanywa na umbile la Kiyahudi, ambalo liliasisiwa na Himaya ya Uingereza yenyewe, na baada ya zaidi ya miezi tisa ya uungaji mkono wao kwa umwagaji damu wa Waislamu mjini Gaza, kampeni za uchaguzi wa rais na chama zinaendelea hivi sasa nchini Marekani na Uingereza.

Soma zaidi...

Utawala wa Mirziyoyev nchini Uzbekistan Unafuata Nyayo za Karimov Aliyekufa, katika Kuwatesa Mashababu wa Hizb ut Tahrir na Kukabiliana na Uislamu

Vyombo vya usalama nchini Uzbekistan vimewakamata tena wanachama 23 wa Hizb ut Tahrir na kuendelea na taratibu za kesi zao Mei 9 2024 kwa mashtaka yale yale waliyoshtakiwa wakati wa enzi ya dhalimu aliyefariki Karimov. Mashababu hao tayari walikuwa washatumia karibu miaka 20 jela na mateso tangu 1999 - 2000 M.

Soma zaidi...

Kuwekwa Kizuizini kwa Sababu ya Majadiliano Tu ya Hadhara kuhusu Kanuni za Shariah ya Kiislamu katika Demokrasia Kubwa Zaidi Duniani

Mamlaka za polisi kutoka jimbo la Tamil Nadu nchini India zimeripoti kuzuiliwa kwa Waislamu sita kwa kufanya amali za Hizb ut Tahrir (HT). Watu hao waliokamatwa ni pamoja na Dkt Hameed Hussain, ambaye ana shahada ya uzamifu ya Uhandisi Mitambo, Baba yake Hussain Ahmed Mansoor na kaka yake Abdul Rehman ambaye ni Msomi wa Kiislamu na wengine watatu, Mohammed Maurice, Khader Nawaz Sherif na Ahmed Ali.

Soma zaidi...

Pongezi za Idd Al-Adha Iliyobarikiwa 1445 H

Hizb ut Tahrir inatoa pongezi na baraka zake za dhati kwa Umma wa Kiislamu, wenye kulemewa na majeraha na kustahamili shinikizo la moja kwa moja na lisilo la moja kwa moja la kikoloni. Kwa mnasaba huu, tunawataja makhsusi watu wetu wenye subira mjini Gaza Hashim na kwa jumla katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, tukimuomba Mwenyezi Mungu azifanye siku za Idd hii kuwa chanzo cha utulivu wa nyoyo zao.

Soma zaidi...

Tangazo la Matokeo ya Kuutafuta Mwandamo wa Mwezi wa Shawwal 1445 H Pongezi kwa Idd Al-Fitr Al-Mubarak

Baada ya kuutafuta mwandamo wa mwezi wa Shawwal katika mkesha huu uliobarikiwa wa Jumanne, mwandamo wa mwezi mpya haujathibitishwa kulingana na mahitaji ya Shariah. Kwa hivyo, kesho Jumanne ni kukamilika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan, Mwenyezi Mungu akipenda, na siku inayofuata kesho Jumatano, itakuwa siku ya kwanza ya mwezi wa Shawwal na siku ya kwanza ya Idd al-Fitr iliyobarikiwa.

Soma zaidi...

Tarehe 28 Rajab Mwaka huu ni Ukumbusho Mkubwa kuliko Miaka Yote Iliyopita kwamba Kuregea kwa Khilafah ni Hitajio la Haraka

Kumbukumbu ya kuanguka kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab inakuja mwaka huu ikiwa na athari zaidi ya kukumbukwa kuliko miaka iliyotangulia. Inakuja na jeraha la Palestina linalotiririka damu nyingi zaidi kuliko hapo awali, na kutukumbusha kwamba suala la kupotea kwa Palestina lilikuwa na bado lina uhusiano wa karibu na kuanguka kwa Khilafah.

Soma zaidi...

Serikali ya Rishi Sunak Yaipiga Marufuku Hizb ut Tahrir na Kuisingizia Uongo, Kuibandika Upanga wa "Kuchukia Mayahudi" dhidi ya wale Wanaopinga Mauaji Yanayofanywa na umbile la Kiyahudi huko Gaza

Alhamisi iliyopita, Januari 18, 2024, serikali ya Uingereza ilipigia kura Bungeni ombi la kupiga marufuku Hizb ut Tahrir, ambapo marufuku hiyo iliidhinishwa na wabunge wachache waliokuwepo kwenye kikao hicho.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu