Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 495
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Enyi Waislamu: Inatosha sasa. Ukatili unaofanywa na Mayahudi kwa watu, miti na mawe hauhesabiki! Sasa wanavamia kivuko cha Rafah, ambacho utawala wa Misri ulikichulia kuwa mstari mwekundu ambao haungekaa kimya kuhusu uvamizi dhidi yake.
Maelfu walishiriki katika matembezi makubwa yaliyoitishwa na Hizb ut Tahrir katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) na watu mashuhuri wa mji wa Hebron (Al-Khalil) kuinusuru Rafah na kuokoa kile kilichobaki cha Gaza.
Kutekwa nyara kwa Naveed Butt tangu tarehe 11 Mei 2012, ni dhambi kubwa na ukiukaji wa wazi wa haki za binadamu. Hakuna kesi ya ugaidi, uasi au uhaini iliyosajiliwa dhidi ya Naveed Butt. Zaidi ya hayo, hakuna kesi hata ya kumdhuru nzi, au kung'oa jani kutoka kwa mti, ya Naveed Butt mwenye huruma na mkarimu.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Enyi Waislamu wa Vikosi vya Jeshi la Pakistan! Kuweni Upande wa Ummah dhidi ya watawala wasaliti ili kulinda Dini na Akhera yenu!
Hizb ut Tahrir / Amerika: Maoni juu ya Maandamano ya Vyuo Vikuu!
Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia inaendeleza kuinusuru kwake Gaza ambapo mpaka sasa imeandaa matembezi 33 tangu kuzinduliwa cheche ya Kimbunga cha Al-Aqsa, na ina nia ya kuuamsha Umma na majeshi yake hadi wasimamishe dola la Uislamu aliyowafaradhishia juu yao Mwenyezi Mungu.
Enyi Waislamu wa Pakistan! Sasa, ni juu yetu kutimiza jukumu letu kwa Palestina, haswa Waislamu wa Gaza!