Jumatano, 05 Safar 1447 | 2025/07/30
Saa hii ni: 17:51:35 (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ewe Hamasa ya Uislamu ndani ya Umma wa Muhammad (saw) Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema: “Si Muumini anayelala ameshiba na hali jirani yake ana njaa.”

Miti na mawe yamelia kutokana na hofu iliyotusibu. Vifua vyetu vinatoa damu na maumivu, watoto wetu wanasisimka kutokana na njaa na kiu, wanawake wetu wanalia ili kuchochea wivu wa ulinzi wa waumini. Asiyeuawa kwa kupigwa mabomu hufa kwa njaa na kiu. Lakini maumivu ya usaliti ni mazito juu yetu kuliko milipuko ya mabomu, njaa, na kiu. Kaka na dada zenu mjini Gaza wanatangatanga bila malengo, bila makaazi, sauti zao zimenyamazishwa na udhaifu ulioletwa na njaa na kiu, baada ya kutoweka matumaini yote kwamba yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu atakuja kuwasaidia. Wanapiga kelele: Uko wapi Umma wa Uislamu? Iko wapi hamasa ya Dini? Uko wapi msaada wa Waumini?

Soma zaidi...

Uhamisho au Ukombozi, enyi Umma wa Kiislamu?

Dhalimu wa Marekani, Trump, alisema katika mkutano na waandishi wa habari pamoja na mhalifu Netanyahu jioni ya Jumanne, 4 Februari 2025: "Marekani itachukua Ukanda wa Gaza, na tutafanya kazi nayo pia" Aliongeza, "Tutageuza Ukanda wa Gaza ulioharibiwa kuwa Riviera ya Mashariki ya Kati." Alizungumzia juu ya umiliki wake wa muda mrefu wa Gaza na alisisitiza taarifa yake ya awali kuhusu kuwahamisha watu wa Gaza, ambapo alisisitiza kutiishwa kwa watawala wa Misri na Jordan na wasaidizi wao, akisema: "Misri na Jordan zilisema hazitapokea wakaazi kutoka Gaza, na mimi nasema lazima watapokea." Hapo ndio watawala watiifu, wasaliti.

Soma zaidi...

[شَهْرُ ‌رَمَضَانَ الَّذِي أُنْزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ] “Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur'ani kuwa ni uwongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi.” [Surah Al-B

Mwezi wa Furqan umekujieni. Unawajibisha kutofautisha baina ya haki na batili. Basi kuweni watiifu kwa Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume wake (saw), na jiepushe na ukafiri, makafiri, unafiki na wanafiki. Hakuna hukmu inayostahili kutawala isipokuwa ya Mwenyezi Mungu (swt).

Soma zaidi...

“SUBHANA, Ametakasika aliye mchukua mja wake usiku mmoja kutoka Msikiti Mtukufu mpaka Msikiti wa Mbali, ambao tumevibariki vilivyo uzunguka, ili tumuonyeshe baadhi ya Ishara zetu. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia na Mwenye kuona.” [Al-Isra’: 1]

Safari ya Usiku na Kupaa, Al-Isra’ Wal Mi’raj, ni muujiza mkubwa ambapo Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), aliona moja ya alama kuu za Mola wake. Ambapo milango ya Bait al-Maqdis na milango ya mbinguni ilifunguliwa kwa ajili yake baada ya kukata tamaa na watu wa Makka na Taif.

Soma zaidi...

Enyi Ummah wa Muhammad (saw) Je! Ni Kufa Kifo cha Udhalilifu, au Utukufu, Ushindi na Tamkini?!

Enyi Ummah wa Muhammad (saw)! Watu wa Gaza wako baina ya kifo na kifo zaidi. Ikiwa hawatakufa kutokana na mabomu, watakufa kwa njaa, kiu, au watakufa kwa maradhi. Eneo la Kaskazini la Ukanda wa Gaza liko chini ya mzingiro mkali bila ya chakula, maji, au dawa. Kwa hivyo mutafanya nini, Enyi Waislamu?

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu