Jumanne, 26 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

DVD “Amali za Kimataifa za Hizb ut Tahrir katika Kuinusuru Gaza!”

Kwa kuzingatia matendo ya kishujaa ya mujahidina katika ardhi iliyobarikiwa ya Palestina mnamo 7 Oktoba 2023, chini ya kauli mbiu ya “Kimbunga cha Al-Aqsa,” dhidi ya umbile nyakuzi la Kizayuni, ambalo limeendelea katika uvamizi wake dhidi ya Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa na kuzingirwa kwake na mashambulizi ya mabomu yanayoendelea ya Ukanda wa Gaza kwa zaidi ya miaka 19, umbile hilo limefichuliwa jinsi lilivyo: umbile la kuchukiza, msingi wake ni dhaifu kuliko utandu wa buibui.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi Miongoni mwa Mashababu wa Hizb ut Tahrir Mwalimu Ustadh Ahmad Muhammad Al-Saharin (Abu Khalid)

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir/Wilayah Jordan inaomboleza kifo cha mwalimu mtukufu, Ustadh Ahmad Muhammad Al-Saharin (Abu Khalid), mwanachama wa Hizb ut Tahrir, aliyefariki Jumatano, 10 Disemba 2025, akiwa na umri wa miaka 79. Alikuwa miongoni mwa wabebaji da’wah wa muda mrefu na anayejulikana sana huko Tafila.

Soma zaidi...

Licha ya Serikali ya Jordan Kuwaangusha Watu wa Gaza na Kujisalimisha Kwake kwa Mpango wa Trump, Vyombo Vyake vya Usalama Vyamkamata Mmoja wa Wanachama wa Hizb ut Tahrir

Serikali ya Jordan inaendelea kwa kiburi katika dhambi na uvamizi, licha ya kuwaangusha watu wa Gaza, na kwa hakika ushirikiano wake na umbile la Kiyahudi katika vita vya mauaji ya halaiki ambavyo imepigana katika Ukanda wa Gaza, kwa kulipatia njia za uwezeshaji na uhai. Haikusita kumbariki Trump mhalifu katika kuifilisi kadhia ya Palestina kwa kuhudhuria kile kinachoitwa “Baraza la Amani” ili kuwa shahidi wa uongo wa mpango wa Trump wa udhibiti juu ya ardhi za Waislamu na kwa kupotea kwa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Amali ya Umma “Moto mjini Gaza Hautazima, na Dhulma Haitakwisha!!

Katika kukabiliana na mauaji ya kikatili yanayoendelea (mauaji ya halaiki) yaliyofanywa na umbile halifu la Kizayuni dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi, kujeruhiwa, na kutoweka kwa Waislamu zaidi ya 220,000 hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki iliandaa usomaji wa taarifa kwa vyombo vya habari katika miji kumi mikubwa chini ya kichwa: “Moto Hautazima Gaza, na Dhulma Haitakwisha!”

Soma zaidi...

Shambulizi la Muafghani jijini Washington na Maeneo Yaliyofichwa ya Siasa

Shambulizi la silaha jijini Washington, D.C. wiki moja iliyopita—ambapo Rahmanullah Lakanwal, raia wa Afghanistan, anatuhumiwa kuwafyatulia risasi Walinzi wawili wa Kitaifa wa Marekani—lilitokea karibu na kituo cha Metro cha Farragut Magharibi, mita mia chache tu kutoka Ikulu ya White House, eneo ambalo kwa kawaida linalindwa na baadhi ya tabaka kali zaidi za usalama. Kutokana na ufyatuaji risasi huo, Sarah Bäckström, mlinzi wa Kitaifa wa miaka 20, aliuawa na Andrew Wolf alijeruhiwa vibaya.

Soma zaidi...

Utawala wa Sharaa nchini Syria Haujui Mipaka Katika Kujisalimisha Kwake kwa Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump alituma barua iliyoandikwa kwa mkono kwa kiongozi wa Syria Ahmed Sharaa, akisisitiza uungaji mkono wake na kuahidi msaada wa Marekani. Barua hiyo iliwasilishwa Damascus kupitia Tom Barrack, mmoja wa washirika wa karibu wa Trump na mfanyibiashara wa kimataifa. Picha ya wakati Trump alipokutana na Sharaa katika Afisi ya Oval iliambatanishwa na barua hiyo. Trump aliandika barua ifuatayo kwenye picha hiyo kwa mwandiko wake mwenyewe: “Ahmed, utakuwa kiongozi mzuri, na Amerika itasaidia!” (Mashirika, 3 Disemba 2025)

Soma zaidi...

Kukamatwa Kupya kwa Wanachama wa Hizb ut Tahrir nchini Yemen na Mahouthi Je, kauli mbiu “Kifo kwa Amerika” inawezaje kuishi sambamba na Kutetea Mpango wa Trump kuhusu Gaza?!

Mnamo Alhamisi, 27/11/2025, vikosi vya usalama vya Mahouthi vilimkamata Saddam Ali Qa’id al-Mukirdi, mwenye umri wa miaka 28, kutoka wilaya ya Ṣabr al-Mawadim katika Mkoa wa Taiz ulio chini ya udhibiti wa Mahouthi katikati mwa Yemen. Kukamatwa huku ni kwa pili, kufuatia kukamatwa kwa ndugu Osama na Mohammad Mas’ad Al-Wurafi katika Mkoa wa Ibb mnamo 21/11/2025, baada ya kugawanya toleo lenye kichwa: “Trump Awaongoza Wafuasi Wake Miongoni mwa Watawala katika Ardhi za Waislamu kwenye Mpango wa Fedheha na Aibu, Wanaosujudu Vichwa Vyao Nyuma Yake kwa Kuiweka Gaza ya Hashim Chini ya Udhamini na Ukoloni.”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu