Chuo Kikuu cha Al-Quds Kinafanya Kongamano kwa Ufadhili wa Magharibi na Programu Iliyoundwa na Magharibi Chini ya Kauli Mbiu “Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake”
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo Jumanne, 2 Disemba 2025, Kitivo cha Sheria katika Chuo Kikuu cha Al-Quds – Abu Dis kilizindua kongamano la kimataifa lililopewa kichwa “Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake: Changamoto, Masuluhisho, na Mbinu Bora katika Eneo la Mediterania,” kwa ushirikiano na Wizara ya Masuala ya Wanawake ya Palestina, Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya Kupambana na Ukatili Dhidi ya Wanawake, Shirika la Idadi ya Watu la Umoja wa Mataifa (UNFPA), na Chuo Kikuu cha Perugia, Italia, kwa usaidizi wa ushirikiano wa Italia.



