Jumapili, 17 Sha'aban 1446 | 2025/02/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Amali Kubwa: “Ni Nani atamzuia Trump?!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) ambayo yanayofanywa na umbile nyakuzi la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina), na kwa kuzingatia matakwa ya adui wa Mwenyezi Mungu, Trump, kuwahamisha Waislamu wasio na ulinzi kutoka Ukanda wa Gaza, Hizb ut Tahrir/Wilayah Uturuki inaandaa amali za halaiki kote nchini Uturuki chini ya kichwa: “Ni Nani atamzuia Trump?!”

Soma zaidi...

Umbile la Kigaidi la Kizayuni Limeufanya Ukingo wa Magharibi kuwa Makaburi ya Watoto kama vile Gaza, Huku Majeshi ya Nchi za Waislamu Yakitazama

Mnamo tarehe 7 Februari, shirika la ‘Save the Children’ liliripoti kwamba watoto wasiopungua 224 wameuawa katika Ukingo wa Magharibi na wanajeshi au walowezi wa Kizayuni tangu Januari 2023, mdogo zaidi akiwa na umri wa miaka 2 pekee. Kulingana na Umoja wa Mataifa, watoto 171 waliuawa katika Ukingo wa Magharibi tangu tarehe 7 Oktoba 2023 - sawia na karibu 1 kila siku. Hakuna mwanajeshi wa Kizayuni aliyefunguliwa mashtaka au kuwajibika kwa mauaji haya. Afisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu ilisema kuwa kumekuwa na ongezeko la mara 20 la idadi ya watoto wa Kipalestina waliouawa na mashambulizi ya anga ya umbile la Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi katika miaka ya hivi karibuni.

Soma zaidi...

Vitisho vya Kutojali vya Trump Vitasambaratishwa dhidi ya Mwamba wa Ustahamilivu wa Gaza

Mara tu Trump alipotwaa urais wa Marekani, alianza kutoa vitisho kushoto na kulia. La kukasirisha zaidi kati ya haya lilikuwa ni tangazo lake la nia yake ya kuwahamisha kwa nguvu watu wa Gaza. Alisisitiza tena uungaji mkono wake wa kufukuzwa kwa kudumu kwa Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza hadi nchi nyingine wakati wa mkutano wake na Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi mnamo Jumanne, 4 Februari 2025. Hata alitangaza nia yake ya kununua ardhi ya Gaza na kuigeuza kuwa mradi wa uwekezaji!

Soma zaidi...

Trump asingeweza Kututawala kama Tungekuwa na Khalifa, na Umbile la Kiyahudi Lisingekuwepo bila Usaliti wa Watawala wetu

Viongozi wa ukafiri nchini Amerika na Ulaya, pamoja na chombo chao, umbile la Kiyahudi, wanajua kwamba misimamo ya watawala wa Waislamu, duara zao za kisiasa, na wapambe wao—wanaowatukuza—hawawakilishi wengi wa Waislamu, wala hawaakisi matumaini yaliyo ndani ya nyoyo zao kwa ajili ya kuregeshwa kwa mamlaka yao. Ukitaka kuelewa msimamo wao wa kweli na jibu lao kwa maamrisho ya Mwenyezi Mungu mbele ya chuki kwenu na kuwaua duniani kote, na kusubutu kwenu kutishia kukalia ardhi zao zaidi na kupora mali zao, musiangalie zaidi ya kiburi cha kiongozi wenu Trump. Kwa kutokuwa na haya mbele ya ulimwengu, ameonyesha kiburi cha Amerika kafiri na msaada wake kwa wale walioshukiwa na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...

Urusi Yajaribu Kubandika Shtaka la Ugaidi kwa Chama Kinachoheshimika zaidi cha Kisiasa ili Kuhalalisha Ukandamizaji na Kufilisika kwake!

Chini ya kichwa cha habari: "Huduma ya Usalama ya Urusi yakamata seli ya kigaidi yenye uhusiano na Hizb ut Tahrir," Russia Today ilichapisha ripoti mnamo 5 Februari 2025, ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya kigaidi yenye uhusiano na Hizb ut Tahrir huko Crimea na kuwakamata watu watano ambao walikuwa wakisajili wafuasi wa chama hicho, ambacho kimepigwa marufuku nchini Urusi." Video ilionyeshwa inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba.

Soma zaidi...

Maamuzi ya Mikutano ya Mawaziri wa Kiarabu ni Matupu na Hayatapita zaidi ya Maandishi kwenye Karatasi

Mkutano wa Mawaziri wa Pande Sita wa Kiarabu jijini Cairo mnamo Jumamosi, 1 Februari 2025, kuhusu Gaza na Kadhia ya Palestina ambayo ni pamoja na Jordan, Imarati, Saudi Arabia, Qatar, na Misri, pamoja na Katibu wa Kamati ya Utendaji ya Jumuiya ya Ukombozi wa Palestina na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu - walithibitisha katika taarifa yao kile walichokiita "uungaji mkono wao kamili wa watu wa Palestina juu ya ardhi yao na kuzingatia haki zao halali kwa mujibu wa sheria ya kimataifa."

Soma zaidi...

Kuanguka kwa Khilafah Kunaashiria Wito wa Kuhuishwa Kwake

Mnamo tarehe 3 Machi 1924, sawia na 28 Rajab 1342 H, kikundi kidogo cha wasaliti wa Kituruki, wakiongozwa na Mustafa Kemal, walivunja urithi wa zaidi ya karne 13 za umoja wa Waislamu. Kuanzia wakati huo na kuendelea, Waislamu walipoteza paa lao juu ya vichwa vyao na wakawa mayatima. Leo, miaka 104 ya hijria imepita tangu tukio hili la kusikitisha. Baada ya kuanguka kwa Khilafah, makafiri waligawanya ulimwengu wa Kiislamu katika maeneo madogo yaliyojitenga. Waliweka vikwazo vya usafiri kati ya maeneo haya, yakihitaji pasipoti na visa, na kuharibu majeshi yetu, silaha, rasilimali, ardhi, uwezo wa binadamu, na teknolojia-kila kitu.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu