Iwapo Kuanguka kwa ‘Jamhuri’ Hakukupelekea Kusimamishwa kwa Khilafah, Ni lazima Kutumike kama Hatua ya Mpito kuelekea Khilafah Rashida
- Imepeperushwa katika Afghanistan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kuporomoka kwa serikali ya Jamhuri nchini Afghanistan ni moja ya matukio muhimu zaidi kwa watu wa Afghanistan na Umma mpana wa Kiislamu katika karne ya 21. Serikali hii sio tu kwamba haikuwa na mizizi yoyote katika itikadi ya Kiislamu, bali ilikuwa ni zao la muundo wa ukoloni mamboleo - mfumo ulioagizwa kutoka nje uliojengwa ili kurasimisha ufisadi, utegemezi, na dhulma. Kuanguka kwake lilikuwa ni mwisho wa kimaumbile na usioepukika wa mfumo ambao, tangu kuanzishwa kwake, ulikuwa ngeni kwa kitambulisho cha Kiislamu na kupingana na maadili ya Uislamu.