Jumatano, 16 Safar 1446 | 2024/08/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kama Umma Mmoja: Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa Kuangamizwa kwa Dhalimu Hasina na Tunawaombea Kuporomoka Madhalimu Wote Wanaoukandamiza Ummah

Baada ya majuma kadhaa ya ukandamizaji wa kikatili dhidi ya watu wa Bangladesh na dhalimu Hasina, genge la serikali yake, na wachungaji wake wa kigeni, alilazimishwa kidhalilifu kuikimbia nchi. Waislamu shupavu wa Bangladesh, wakiongozwa na wanafunzi jasiri, walivumilia ukatili usio na kifani na hatimaye kulazimisha kuondolewa kwake kupitia wimbi lisilozuilika la maandamano ambayo yalimshinda dikteta huyo.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yaandaa Maandamano mjini Al-Qadarif Kutaka Kukomeshwa kwa Vita na Umwagaji damu ya Waislamu

Mnamo siku ya Ijumaa, Agosti 2, 2024, Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan iliandaa maandamano katika mji wa Al-Qadarif baada swala ya Juma’a karibu na Jami’ Al-Atiq (Msikiti Mkongwe) katika Soko la Al-Qadarif. Maandamano hayo yalitaka kukomeshwa kwa vita na umwagaji damu ya Waislamu.

Soma zaidi...

Umbile la Mayahudi wa Kizayuni Linakiuka Matukufu Yetu Lipendavyo, Huku Watawala wa Waislamu Wakiyafungia Majeshi Yetu kwenye Kambi Zao

Mnamo asubuhi ya tarehe 31 Julai 2024, umbile la Kiyahudi lilimuua shahidi kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh katika shambulizi la kombora jijini Tehran, mji mkuu wa Iran. Siku moja kabla, umbile hilo la Kiyahudi lilimuua shahidi kamanda wa Hezbollah kwa kushambulia jengo la makaazi jijini Beirut, Lebanon. Hapo awali, umbile la Kiyahudi lilishambulia vituo mbalimbali katika bandari ya Hodeida nchini Yemen kwa ndege za kivita. Hii ni huku Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina ikiwa imegeuzwa kuwa magofu katika kipindi cha miezi kumi iliyopita.

Soma zaidi...

Umbile la Halifu la Mayahudi Kukiuka Nafasi za Ummah na Kuua Watu wake katika Miji Mikuu ni Uhalifu wa Tawala za Kioga mbele ya Umbile la Kiyahudi

Katika shambulizi la kiuhaini na lisilo na aibu, umbile halifu la Kiyahudi lilimuua mkuu wa afisi ya kisiasa ya Hamas jijiniTehran, ambapo Ndugu Ismail Haniyeh aliuawa shahidi alfajiri ya leo na adui wa Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na Umma. Tunamuomba Mwenyezi Mungu rehema na msamaha wake na amjaalie miongoni mwa mashahidi. Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na hakika kwake Yeye tutaregea.

Soma zaidi...

Serikali ya Jordan Kuanzisha Afisi ya NATO ni Uhalifu dhidi ya Palestina na Gaza na Usaliti kwa Umma wa Kiislamu

Huku Wamagharibi wakikata tamaa ya uwezo wa tawala vibaraka katika nchi za Kiislamu kuendelea kudhibiti na kutawala mambo, na uhakika wake kwamba Ummah unakaribia kuzifagilia mbali tawala hizi na kuziondoa, na hivyo kuondoa uwepo wao katika nchi zetu; kwa kuzingatia haya yote, hatua hii ilitoka kwa NATO, ili wao wenyewe waweze kusimamia utekelezaji wa mipango yao na kulinda maslahi yao katika ardhi zetu, na kulinda umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Wale Ambao Hawakufa kwa Risasi za Vita Walikufa ndani ya Makaazi ya Serikali!

Sudan Tribune iliripoti jana, Jumamosi, Julai 27, 2024, ikinukuu taarifa iliyotolewa na Kamati ya Maandalizi ya Umoja wa Madaktari wa Sudan, iliyosema: “Kamati ya Maandalizi ya Umoja wa Madaktari ilisema katika taarifa iliyopokelewa na Sudan Tribune kwamba watu waliokimbia makaazi yao mjini Kassala wanaishi kwenye mahema yaliyochakaa na kuzungukwa na maji kila upande, na watoto wao wanalia kwa njaa. Iliongeza kuwa hali imekuwa mbaya zaidi, kwani watoto wawili walikufa kwa shoti ya umeme, na kuna vifo kutokana na kuumwa na nyoka na kesi zingine zisizojulikana.”

Soma zaidi...

Tatizo la Umeme wa Ghali Halitatuliwi kwa Kupunguzwa kwa Malipo ya Nyuzi za Umeme na Majadiliano Mapya ya Mikataba Pekee. Suluhisho ni Kukomeshwa Kabisa kwa Ubinafsishaji katika Sekta ya Kawi, kwa mujibu wa Amri ya Mwenyezi Mungu (swt)

Kutolewa kwa data kuhusu malipo ya nyuzi za umeme kwa mitambo ya kuzalisha umeme na aliyekuwa waziri wa muda wa biashara, Gohar Ejaz, kumewashangaza watu. Muundo wa kandarasi za malipo ya nyuzi za umeme, ambao thamani yake ni zaidi ya rupia bilioni 2,000, umepangwa na mashirika ya wakoloni ya kimataifa, Benki ya Dunia na Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF).

Soma zaidi...

Kwa Shangwe na Nderemo ya Hali ya Juu, Bunge la Marekani Lilimkaribisha Muuaji wa Gaza!

Baada ya miezi kumi ya mauaji ya kila siku dhidi ya watu wa Gaza, ambayo yanatangazwa muda baada ya muda kwa sauti na picha za hali ya juu, kwa idadi, takwimu, ushuhuda na hukumu za mahakama... baada ya yote hayo, Bunge la Congress lilimpokea kiongozi wa Baraza la Vita huko Gaza, Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi Netanyahu, kwa karamu ya nderemo na shangwe kana kwamba yeye ni mmoja wa mashujaa wa watu wao. Sauti yao ya ndani ikisema: Tunataka kukupa ujira, Netanyahu, kwa kuwaua Waislamu wa Gaza kwa niaba yetu.

Soma zaidi...

Ajenda ya Mapinduzi ya Uislamu Kurekebisha Uchumi wa Pakistan, Baada ya Kuharibiwa kupitia Sera za Wakoloni

Utabikishaji wa sera za wakoloni umeharibu uchumi wa Pakistan, ambao una rasilimali nyingi sana. Kwa hatua na vipimo vyote, serikali na watu wa Pakistan wako kwenye ukingo wa kufilisika. Madeni ya mzunguko wa sekta ya nishati na bili za umeme haziwezi kumudika. Licha ya ongezeko la mara nne la ukusanyaji wa ushuru katika miaka tisa iliyopita, nakisi ya kifedha ya bajeti ya shirikisho, ya rupia bilioni nane na nusu, inazua maswali mazito kuhusu uwezo wa serikali.

Soma zaidi...

Mkono wa Umbile Halifu Wavamia nchi Yetu ya Yemen na ash-Sham chini ya Njama za Tawala na Kukosekana kwa Uzuiaji

Ndege za umbile halifu la Kiyahudi zilianzisha msururu wa mashambulizi ya kichokozi dhidi ya Yemen. Wakati wa mkutano wake jana, Baraza la Mawaziri la umbile hilo linalohusika na masuala ya usalama liliidhinisha shambulizi hilo dhidi ya Yemen, kwani uvamizi huo ulilenga vituo vya kuhifadhi mafuta na kituo cha umeme katika bandari ya Hodeidah.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu