Trump Aitishia Gaza kwa Uvamizi wa Moja kwa Moja na Kuwafukuza Watu Wake
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Jioni ya Jumanne, 4 Februari 2025, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza katika mkutano wake na Waziri Mkuu wa Kiyahudi kwamba "Wapalestina hawana chaguo zaidi ya kuondoka Ukanda wa Gaza. Nataka kuona Jordan na Misri zikipokea Wapalestina kutoka Gaza. Hakuna badali kwa wakaazi wa Gaza isipokuwa kuondoka." Aliongeza, "Jordan na Misri tayari zimekataa kuwapokea wakaazi kutoka Gaza, lakini baadhi ya watu wanakataa mambo isipokuwa hatimaye kukubaliana nayo."