Alhamisi, 30 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/10/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Sudan

H.  27 Rabi' I 1446 Na: HTS 1446 / 11
M.  Jumatatu, 30 Septemba 2024

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Masuala ya Ummah
(Imetafsiriwa)

Tunafuraha kutangaza kwamba Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan itaanzisha tena kikao cha kila mwezi, Jukwaa la Masuala ya Ummah, ambalo linajadili masuala ya Ummah na kuwasilisha masuluhisho ya kimsingi kwa kuzingatia imani ya Ummah, itikadi tukufu ya Kiislamu. Tunayo heshima kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wale wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria, kushiriki, na kuchangia kwa maoni na mawazo yao. Jukwaa la mwezi huu litaanza na mada:

Mapambano ya Kimataifa ya Ushawishi nchini Sudan na Mbinu za Ukombozi

Wazungumzaji kwenye kikao:

1. Ustadh Nasser Reza – Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan.

2. Ustadh Ibrahim Othman (Abu Khalil) – Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan.

3. Mwendesha kikao: Ustadh Yaqoub Ibrahim – Mjumbe wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan.

Tarehe: Jumamosi, 2 Rabi' al-Akhir 1446 H, sawia na tarehe 5 Oktoba 2024 saa saba mchana (1:00 PM)

Mahali: Afisi ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan katika mji wa Port Sudan – mtaa wa Al-Azhama - Barabara ya Stadium - Mashariki mwa Stadium.

Kuhudhuria kwako kunaakisi hamu yako kwa masuala ya Ummah wako.

Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Sudan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
Address & Website
Tel: 0912240143- 0912377707
http://www.hizb-sudan.org/
E-Mail: Spokman_sd@dbzmail.com

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu