Jumatano, 16 Safar 1446 | 2024/08/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

  Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan:

Ripoti ya Habari 08/04/2022

Katika muendelezo wa amali za umma zilizoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan, ili kuuamsha Umma wa Kiislamu na kuimarisha azma yake ya kusimamisha Dola ya Khilafah Rashida ya pili, kwa kuunda rai jumla inayofahamu hukmu za Uislamu na masuluhisho yake, Hizb imefanya amali mbalimbali za umma katika majimbo na mikoa mbalimbali ya nchi.

Ambapo Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan walitoa hotuba kubwa ya umma katika mji wa El Obeid yenye kichwa: "Demokrasia ni nidhamu ya Kikafiri Haram, kuichukua, kuitabikisha, au kuilingania," mnamo Machi 17, 2022, mbele ya ukumbi wa Gold Soir Musalah, ambapo Ustadh Muhammad Al-Amin Dafa Allah alizungumza akielezea ufisadi wa fikra ya Demokrasia jinsi ilivyotokana na akili ya mwanadamu iliyo dhaifu na isiyokamilika ambayo haina uwezo wa kujua kipi kina madhara na kipi ni kizuri kwa ajili yake. Pia alionyesha ufisadi wa msingi ambao demokrasia imejengwa juu yake.

Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan katika mji wa Gedaref walifanya mkao wao wa mara kwa mara, kwa anwani: "Mawimbi ya bei ya juu na dalili za kuporomoka." Je, kuna mwangaza ndani ya handaki? Waraka wa kwanza uliowasilishwa na Ustadh Suleiman Ad-Dasis ilishughulikia mawimbi mfululizo ya bei ya juu ambayo yaliongeza mateso ya watu na kuwachosha, kama sababu nzuri zaidi za kutabikisha mfumo wa kirasilimali unaowakilishwa katika kuunganisha sarafu na dolari, ambayo kwa kweli ni karatasi ambayo thamani yake tu ni wino ambao kwao ilichapishwa, iliyolazimishwa na Amerika kwa watu wa ulimwengu ili kupora utajiri wao.

Waraka wa pili, iliowasilishwa na Mhandisi Al-Bashir Ahmed, pia ilishughulikia masuluhisho kutoka kwa msingi wa Uislamu mtukufu yanayo hakikisha maisha ya utu sio tu kwa Waislamu; Bali, kwa watu wote, alipoanza hotuba yake kwamba Sudan, pamoja na rasilimali zake ambazo Mwenyezi Mungu ameijaalia, inaifanya kustahiki kuwa kapu la chakula duniani. Kisha akagusia dolari na uharamu wa kuichukua kama msingi wa pesa. Kanuni katika Uislamu ni kwamba dhahabu na fedha ndio msingi wa fedha taslimu. Dola ya Khilafah Rashida ya pili, kwa njia ya Utume, itatengeneza dinari za dhahabu na dirham za fedha ili kukomesha kiburi na utawala mkubwa wa fedha za watu.

Katika muktadha wa kupanda kwa bei na kuongezeka kwa bei, Mashababu wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan walifanya hotuba kubwa ya hadhara katika mji wa El Obeid mnamo tarehe 24 Machi 2022 mbele ya ukumbi wa swala wa Soar al-Zahab, ambayo Ustadh al-Nazir Muhammad Hussein alizungumza akielezea sababu na vyanzo vya kupanda mara kwa mara kwa bei ya mafuta, ambayo ilisababisha kupanda kwa bei katika kila kitu.

"Ramadhan ni mwezi wa ufunguzi na ushindi wa majeshi ya Kiislamu." chini ya mada hii, mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan walifanya hotuba kubwa ya hadhara katika mji wa El Obeid mnamo Machi 30, 2022 mbele ya ukumbi wa salwa wa Siwar al-Dahab, ambapo Ustadh Muhammad Qoni alizungumza, akielezea jinsi Waislamu walivyoshinda Vita vya Badr na jinsi walivyoiteka Makka kwa sababu tu Washirikina wa Maquraish waliwashambulia washirika wa Mtume (saw), ni nani atawasaidia Waislamu wanaodhulumiwa nchini Syria, Palestina, Iraq, Yemen na Kashmir? Nani atashinda kwa dalili za Waislamu? Je, sio wajib kufanya kazi ya kulinyanyua neno la Mwenyezi Mungu?

Mjumbe wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu