Kichwa cha habari cha Fox News mnamo tarehe 22 Mei kilisema kwamba "Utawala wa Trump wasitisha mpango wa visa ya wanafunzi wa Harvard" na makala hayo yalimnukuu Waziri wa Elimu, Kristi Noem, akisema: "Utawala huu unaihisabu Harvard kwa kuendeleza vurugu, chuki dhidi ya Mayahudi, na kuratibiana na Chama cha Kikomunisti cha China kwenye chuo chake ... Ni fursa, sio haki, kwa vyuo vikuu kuchukua wanafunzi wa kigeni na kufaidika na malipo yao ya juu ya masomo ili kusaidia kulipa ruzuku zao za mabilioni ya dolari. Harvard ilikuwa na fursa nyingi za kufanya mambo kwa usahihi. Ilikataa. Wamepoteza cheti chao cha Mpango wa Wanafunzi na Ubadilishanaji wa Wageni (Student and Exchange Visitor Programme) kutokana na kushindwa kwao kuzingatia sheria. Hebu hili na liwe ni onyo kwa vyuo vikuu na taasisi zote za kielimu kote nchini."