Jumamosi, 14 Muharram 1446 | 2024/07/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Vichwa vya Habari 07/12/2022

Vichwa vya Habari:

Indonesia Yapitisha Kanuni ya Jinai Kupiga Marufuku Ngono Nje ya Ndoa

Wasiwasi wa Ulaya Juu ya Sheria ya Marekani ya Kupunguza Mfumko wa Bei

Maelezo:

Indonesia Yapitisha Kanuni ya Jinai Kupiga Marufuku Ngono Nje ya Ndoa

Indonesia imepitisha kanuni mpya ya jinai yenye ubishani inayojumuisha kupiga marufuku kuishi kinyumba na ngono nje ya ndoa, katika mabadiliko ambayo wakosoaji wanashindana yanaweza kuhujumu uhuru katika taifa hilo la Asia ya Kusini. Sheria hizo mpya zinahusu watu wa Indonesia na wageni na pia zinaregesha marufuku ya kumtusi rais, taasisi za serikali au mfumo wa kitaifa wa Indonesia unaojulikana kama Pancasila. Kanuni hiyo iliyopangwa ilisababisha maandamano kote nchini yaliyoongozwa na wanafunzi wakati rasimu kamili ilipotolewa mnamo Septemba 2019, huku kukiwa na hofu ingepunguza uhuru wa kibinafsi. Ngono kabla ya ndoa pamoja na uzinzi yataadhibiwa hadi mwaka mmoja gerezani au faini chini ya kanuni hiyo. Kuishi kinyumba kutaadhibiwa kwa miezi sita gerezani au faini, ingawa ikiwa tu itaripotiwa kwa polisi na wazazi, watoto, au mwenza.

Makundi ya kutetea haki yanasema mapendekezo hayo yanasisitiza kuongezeka kwa uhafidhina kwa nchi ambayo kwa muda mrefu imesifiwa kwa uvumilivu wake wa kidini, huku usekula ukishamiri katika katiba yake. Tangu kuanguka kwa mrithi Suharto - ambaye alikandamiza makundi ya kisiasa ya Kiislamu - kumekuwa na uhamasishaji wa maadili ya Kiislamu, hisia kwamba Uislamu unatishiwa na ushawishi wa nje katika maeneo mengi ya kisiwa cha Java, ambapo zaidi ya nusu ya watu wa Indonesia wanaishi. Jibu la vyombo vya habari vya kilimwenguni limekuwa hasi, vimewasilisha hatua hii kama hatua ya kurudi nyuma katika ulimwengu wa kisasa.

Wasiwasi wa Ulaya Juu ya Sheria ya Marekani ya Kupunguza Mfumko wa Bei

Ziara ya Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ya hivi karibuni nchini Amerika mnamo Novemba 29 ambapo alikutana na Rais Joe Biden na kujadili Sheria ya Kupunguza Mfumko wa bei ya hivi karibuni (IRA). Hatua hiyo ni pamoja na $370 bilioni katika ruzuku na mapumziko ya ushuru kwa uwekezaji salama kwa mazingira. Lakini sharti kuu la hili ni kuwa silsila nyingi za usambazaji wa bidhaa zinazofuzu kwa mahitaji ya bidhaa ziwe Amerika Kaskazini. Lakini Ulaya, Ufaransa ikiwa mstari wa mbele, imeiunda sheria hiyo kama juhudi haramu ya kupora viwanda vyenye weledi na mkakati wa hali ya juu vya Ulaya wakati bara hilo liko katika mazingira magumu zaidi. Maafisa wa Ulaya wanaitishia Washington kwa vita vya kibiashara na kesi mbele ya Shirika la Biashara Ulimwenguni ikiwa haitavipa viwanda vyao manufaa sawia na yale yanayopatikana Canada na Mexico. Kwa miongo kadhaa Amerika ilikuza biashara ya huria ya kilimwengu ili kuunda agizo ambalo litatumikia ajenda yake. Lakini baada ya miaka mlipa ushuru wa Amerika iliona nafasi za kazi na viwanda vikihamia nje ya nchi na kampuni za kigeni zikipata fursa nzuri katika soko la Amerika, kwa gharama ya kampuni za nyumbani za Amerika. Siku za utandawazi sasa zinabadilishwa na uchumi wa utaifa na kurudishwa biashara ndani ya nchi badala ya kutolewa nje.

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu