Jumanne, 28 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/10/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Iraq

H.  24 Rabi' I 1446 Na: 1446 / 02
M.  Ijumaa, 27 Septemba 2024

Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Viumbe Vioga zaidi vya Mwenyezi Mungu Vinaonyesha Ujasiri baada ya Mashujaa Kuzika Vichwa vyao kwenye Mchanga!
(Imetafsiriwa)

Operesheni Kimbunga cha Aqsa “Tufan Al-Aqsa” kwa hakika imezifichua na kuzidhihirisha tawala za khiyana katika ardhi za Waislamu na watawala wao wasaliti. Vile vile imewasilisha hoja ya wazi kwa watu wenye nguvu na ushawishi katika Ummah, hususan majeshi yake, na hatimaye, imefichua uwongo na udanganyifu wa kile kinachoitwa “Mhimili wa Upinzani.”

Kwa takriban mwaka mzima, umbile la Kiyahudi limekuwa likiwaletea watu wa Gaza mambo ya kuogofya, uhalifu dhidi ya watoto, wanawake, majengo na hospitali, uhalifu unaopelekea mtu kutetemeka kwa hofu kali. Na bado, Gaza yenye fahari, baada ya karibu mwaka mmoja, inasalia kuasi dhidi ya umbile la Kiyahudi. Hawajafikia malengo yao yoyote: sio kuimaliza Hamas wala kurudi kwa wafungwa. Katikati ya matukio haya yote mazito, yote ambayo tumesikia kutoka kwa Mhimili wa Upinzani ni kelele tu au majibu ya aibu ya kuziokoa nyuso!

Hata hivyo, kwa kuaibishwa na uthabiti wa Gaza yenye fahari, wametafuta ushindi ili kuutangazia ulimwengu hivi: “Sisi si waoga wala hatushindwi.” Walipatiliza fursa ya mashambulizi ya vyombo vya habari yaliyoratibiwa na chama cha Iran nchini Lebanon kuonyesha nguvu zao dhidi ya wanamgambo muhimu zaidi wa Iran katika suala la mamlaka na eneo la kijiografia. Walifanya mashambulizi makali dhidi ya chama cha Iran nchini Lebanon kwa kupenyeza vifaa vya pagers na kuwalipua, wakifanya mauaji makubwa miongoni mwa uongozi wake wa kijeshi, na kulipua vikali maeneo ya kusini mwa Lebanon, na kupelekea kulengwa kwa kiongozi wa chama hicho mwenyewe.

Kwa kujibu, tunaona kimya kamili kutoka kwa Iran huku ikitazama, kwa macho yake yenyewe, jinsi chama chake nchini Lebanon kinavyoporomoka, bila kuchukua hatua. Kinyume chake, inaendelea kuchunguza uwezekano wa mazungumzo na Marekani! Je, Iran imekipa mgongo chama chake nchini Lebanon kama ilivyokuwa mjini Gaza hapo awali?

Je, makundi haya yanatambua kwamba hayana mamlaka ya kweli na kwamba maamuzi yao ya kisiasa yapo mikononi mwa wale wanaoyafadhili na kuwalipa mishahara wapiganaji wao?

Je, makundi mengine yatajifunza somo kutokana na tukio hili, au siku itakuja watakapoomboleza, “Nililiwa siku ile ng’ombe mweupe alipoliwa”?

Enyi Waislamu na Majeshi ya Ummah: umbile la Kiyahudi linajivunia nguvu zake mbele ya ulimwengu, hata kufikia kutishia kwamba lina nyingi zaidi ilizoziweka akiba kudhihirisha uwezo wake kwa ulimwengu, kama wanavyodai. Hata hivyo, sisi tunaujua kwa yakini uoga wa kweli wa Mayahudi, kama Mwenyezi Mungu alivyosema kweli pindi aliposema:

[وضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الذِّلَّةُ أَيْنَ مَا ثُقِفُوا إِلَّا بِحَبْلٍ مِّنَ اللهِ وَحَبْلٍ مِّنَ النَّاسِ وَبَاءُوا بِغَضَبٍ مِّنَ اللهِ وَضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الْمَسْكَنَةُ]

“Wamepigwa na udhalili popote wanapo kutikana, isipo kuwa wakishika kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu. Na wakastahiki ghadhabu ya Mwenyezi Mungu, na wamepigwa na unyonge.” [Surat Aal-i-Imran:112] Na Mayahudi wamesema uongo.

Maonyesho haya ya kiburi yanawezekana tu kutokana na kimya chenu, hasa kimya cha majeshi ya Waislamu. Ni ukweli ulioje wa maneno ya mshairi aliyesema: “Ni desturi ya watu kuabudu masanamu, sio kutokana na ukuu wa masanamu hayo, bali kutokana uduni wa watu hao.”

Kwa hiyo kwa heshima ya dunia na furaha ya Akhera, Hizb ut Tahrir inakuombeni, enyi majeshi ya Waislamu, kuondoa udhalilifu kutoka mabegani mwenu na muinue vichwa vyenu kutoka kwenye mchanga. Zipindueni tawala za fedheha, na tangazeni jihad katika njia ya Mwenyezi Mungu ili kuikomboa Al-Aqsa na maeneo mengine ya ardhi za Waislamu. Hapo ndipo Mayahudi watatambua saizi yao halisi, watakapojikinga nyuma ya mawe na miti, kwa kutimiza bishara njema ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw):

«لا تَقُومُ السَّاعَةُ حتَّى تُقاتِلُوا اليَهُودَ، حتَّى يَقُولَ الحَجَرُ وراءَهُ اليَهُودِيُّ: يا مُسْلِمُ، هذا يَهُودِيٌّ وَرائي فاقْتُلْهُ»

“Kiyama hakitosimama mpaka mupigane na Mayahudi, mpaka jiwe ambalo nyuma yake amejificha Yahudi litasema: “ewe Muislamu huyu hapa Yahudi nyuma yangu, basi muuwe.”

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Iraq

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Iraq
Address & Website
Tel: 
E-Mail: hutiraq@yahoo.com

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu