Jumapili, 11 Dhu al-Qi'dah 1445 | 2024/05/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan

H.  15 Shawwal 1445 Na: 1445 / 43
M.  Jumatano, 24 Aprili 2024

Enyi Waislamu wa Pakistan! Waislamu Jasiri wa Gaza Wanasimama Kidete Mbele ya Umbile la Kiyahudi, Hivyo Musikate Tamaa. Washajiisheni Ndugu Zenu na Watoto Wenu katika Vikosi vya Jeshi la Pakistan Kutangaza Jihad kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina

#ArmiesToAqsa

(Imetafsiriwa)

Enyi Waislamu wa Pakistan! Mayahudi, kwa msaada wa watetezi wao wa Marekani, wanafanya ukatili usioelezeka juu ya Waislamu katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina. Waislamu elfu thelathini na nne wameuawa. Waislamu zaidi ya mia moja wamejeruhiwa. Zaidi ya nusu ya mashahidi ni wanawake na watoto. Mtoto mmoja anauawa kila dakika kumi. Kuna wahasiriwa wengi wa njaa, huku nyumba zikivunjwa. Idadi hiyo inaongezeka kila uchao. Mayahudi wamewakamata Waislamu wengi kutoka Ukingo wa Magharibi, na hata zaidi kutoka Gaza, ambao wanakabiliwa na uhalifu wa kikatili katika magereza. Katika wakati ambapo mauaji ya halaiki ya Waislamu yanaendelea huko Gaza, Ukingo wa Magharibi na maeneo mengine, watawala wa Pakistan wanakataa kabisa kuhamasisha vikosi vya jeshi la Pakistan kwa ajili ya ukombozi wa Palestina. Badala yake, watawala hawa wanatabanni msimamo wa Marekani juu ya Palestina, ambao huanza kwa wito wa kusitisha mapigano na kumalizikia na suluhisho la dola mbili, ambalo linasalimisha Palestina nyingi zaidi kwa uvamizi huo.

Enyi Waislamu wa Pakistan! Sasa, ni juu yetu kutimiza jukumu letu kuelekea Palestina, haswa Waislamu wa Gaza. Hatupaswi kujifunga tu na kuomba Dua kwa ajili ya Palestina na kususia bidhaa za Marekani na Magharibi. Ingawa hatua hizi zimejaa kheri na thawabu, sio suluhisho kamili ya tatizo hili. Ni jukumu letu kuwalazimisha watawala hawa kujisalimisha kwa amri ya Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume wake (saw), na kuhamasisha vikosi vya Pakistan katika Jihad kwa ajili ya ukombozi wa Palestina. Hatupaswi kufikiria kuwa sisi, kama watu binafsi, au kama familia, au kama jamaa na marafiki, ni watu wachache tu, ambao wana athari ndogo kwa jamii. Badala yake, lazima tuamini Nusra ya Mwenyezi Mungu (swt) tunapotimiza wajibu wetu wa Kisharia kwa Waislamu wa Palestina. Majeshi yetu lazima yapigane na lazima tuwaamshe ili kupigana. Mwenyezi Mungu (swt) alimuamuru Mtume wake (saw) kwamba,

[يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ حَرِّضِ الْمُؤْمِنِينَ عَلَى الْقِتَالِ]

“Ewe Nabii! Wahimize Waumini wende vitani.” [Surah Al-Anfal 8:65].

Enyi Waislamu wa Pakistan! Sote tunaweza kuchangia katika kampeni ya kimataifa ya #ArmiesToAqsa  kwa njia tano zifuatazo: Kwanza, kupitia akaunti zetu za mitandao ya kijamii kama Facebook, WhatsApp, Twitter, Tiktok na Instagram, tunaweza kuitisha uhamasishwaji wa vikosi vya jeshi la Pakistan kwa ajili ya Jihad. Pili, tunaweza kumtaka Imam wa Msikiti wa eneo letu kuelezea wajibu wa Jihad kwa vikosi vya jeshi la Pakistan, kunusuru Gaza na Palestina. Tatu, tunaweza kuitisha kwamba wanaharakati wa kisiasa na kijamii miongoni mwa jamaa na marafiki zetu kutabanni matakwa ya kuhamasishwa vikosi vya Pakistan kwa ajili ya jihad. Nne, tunaweza kukutana na jamaa zetu na marafiki katika vikosi vya Pakistan na kunataka waweze kuhamasika katika kuinusuru Palestina. Tano, tunaweza kueneza utambuzi wa wito wa kuhamasisha vikosi vya jeshi la Pakistan katika Jihad kwa ajili ya ukombozi wa Palestina, katika afisi zetu, shule, vyuo na mikusanyiko ya kibinafsi, na pia miongoni mwa watu wenye ushawishi katika duara zetu za jamaa na marafiki.

Enyi Waislamu wa vikosi vya jeshi la Pakistan! Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema, «مَا تَرَكَ قَوْمٌ الْجِهَادَ إِلَّا عَمَّهُمُ اللَّهُ بِالْعَذَابِ» “Watu hawatawacha Jihad isipokuwa Mwenyezi Mungu atawajumuisha katika adhabu.” [At-Tabarani katika Al-Mujam Al-Awsat]. Kupuuza kwenu jihad kumesukuma Ummah ndani ya shimo la kukata tamaa, udhalilifu na fedheha. Ummah mzima unangojea msimamo wenu wa maamuzi. Ummah mzima una hamu ya nyinyi kusonga kwa ajili ya Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, kuingia Al-Masjid Al-Aqsa, kama washindi, mkipiga Takbira. Kunyanyuka! Kuwapindua watawala ambao wamekufungieni kwenye kambi zenu. Kuwapindua wale ambao hunyonya nguvu yenu kuwakanyaga wapinzani wao wa kisiasa, na kurefusha muda wa utawala wao. Ipeni Nusrah yenu Hizb ut Tahrir kwa ajili ya kusimamisha Khilafah Rashida, ili muweze kusonga chini ya Khalifa Rashid kwa ajili ya ukombozi wa Palestina yote, kutoka mto wake hadi bahari yake. Mwenyezi Mungu (swt) alisema,

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ اسْتَجِيبُواْ لِلّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُم لِمَا يُحْيِيكُمْ]

“Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele.” [Surah Al-Anfal 8:24].

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan
Address & Website
Tel: 
https://bit.ly/3hNz70q

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu