Jumamosi, 14 Muharram 1446 | 2024/07/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Uhakiki wa Habari 05/11/2022

China na Ujerumani Zamuonya Putin Kutotumia Silaha za Nyuklia Nchini Ukraine

Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters:

Rais wa China Xi Jinping na Chansela wa Ujerumani Olaf Scholz mnamo Ijumaa walilaani vitisho vya kutumia silaha za nyuklia nchini Ukraine, huku Scholz akionya kwamba Urusi inakabiliwa na hatari ya "kuvuka mstari" katika jumuiya ya kimataifa kwa kutumia nguvu za kinyuklia.

Katika ziara ya kwanza ya kiongozi wa G7 nchini China tangu janga la COVID-19, Scholz alimshinikiza Xi kuidhibiti Urusi kukomesha uvamizi wake kwa Ukraine, akisema Beijing ina jukumu kama dola kubwa kufanya hivyo.

Xi alikubali kwamba viongozi wote wawili "wanapinga kwa pamoja matumizi au tishio la matumizi ya silaha za nyuklia" juu ya Ukraine, kulingana na taarifa ya shirika la habari la Xinhua, ingawa alijizuia kuikosoa Urusi au kuitaka Moscow iondoe vikosi vyake.

Scholz aliwasili jijini Beijing kwa ziara ya siku moja ambayo iliyapima maji kati ya China na Magharibi baada ya miaka ya mvutano unaoongezeka, huku mazungumzo yakigusia upatikanaji wa soko kati ya pande hizo mbili, mabadiliko ya tabianchi na chanjo za COVID-19.

Scholz alifanya safari hiyo huku akikabiliwa na ukosoaji kutoka ndani ya muungano wake kuhusu uhusiano na Beijing. Amejaribu kusawazisha kupata uwanja sawa kwa makampuni ya Ulaya na kuondoa utegemezi mkubwa wa Ujerumani kwenye soko la China.

Wakati wa chakula cha mchana na Scholz, Xi alisisitiza kuwa ni rahisi kuvunja uaminifu wa kisiasa lakini ni vigumu kuujenga upya, na pande zote mbili zinahitaji kuutunza, kulingana na Xinhua.

Hapo awali, alipokuwa akisalamia Scholz kwenye Ukumbi Mkuu wa Watu ulio katikati mwa Beijing, Xi alizitaka nchi hizo mbili kufanya kazi kwa karibu zaidi katika masuala ya kimataifa.

Kwa mara nyingine tena, uongozi wa China unaonyesha ubora wa ujuzi wake wa kisiasa ikilinganishwa na Urusi. Kumpokea Cansela Olaf Scholz wa Ujerumani kwa wakati huu ni mafanikio makubwa ya kisiasa kwa Rais wa China Xi Jinping, ambaye wiki iliyopita tu alithibitishwa kwa muhula wa tatu wa miaka mitano kama kiongozi wa China, akiwa mkuu wa kamati mpya ya kudumu ya politburo iliyoundwa na watiifu wake wa kibinafsi. Katika mihula yake miwili ya kwanza, Xi alilazimika kutembea kwa uangalifu kati ya makundi yanayoongozwa na watangulizi wake wawili, Hu Jintao na Jiang Zemin.

Zaidi ya hayo, Xi Jinping anaelewa kile ambacho Rais wa Urusi Vladimir Putin ameshindwa kukitambua. Magharibi yenyewe imegawanyika kwa uchungu. Marekani na Uingereza zinaogopa kuinuka kwa Ufaransa na Ujerumani, huku msuguano ukiwa pia kati ya Ufaransa na Ujerumani, na pia kati ya Marekani na Uingereza. Kwa kuivamia Ukraine bila kujali, Putin analazimisha kuunganishwa kwa dola hizi nne. Kwa miaka mingi, Ufaransa na Ujerumani zimejaribu aina fulani ya uhusiano na Urusi, lakini ziliendelea kukanushwa na rais wa Urusi mwenye kiburi cha kijinga ambaye alisisitiza kutambuliwa sawa kwa sawa na Amerika. kiburi  ni moja ya hatari kubwa katika siasa za kimataifa, kama ilivyo katika maisha ya kawaida pia. China, kwa upande mwingine, inapunguza nguvu yake na kuona thamani wakati huu katika kufikia Ujerumani, huku ikijitenga kidogo na Urusi.

Ni wajibu kwa wenye ufahamu wa kisiasa ndani ya Umma wa Kiislamu kufuatilia kwa makini maendeleo ya hali ya kimataifa ili kufahamu vyema mienendo ya dola kubwa. Uongozi wa Magharibi kafiri duniani umejaa ushindani, migogoro na mivutano ambayo inatoa fursa kwa Umma wa Kiislamu kuibuka kwa haraka kama dola kuu ya ulimwengu. Hili halitafanyika maadamu nchi za Kiislamu zitaendelea kutawaliwa na mabaki ya vibaraka na mifumo ya kikoloni. Lakini kwa idhini ya Mwenyezi Mungu (swt), Ummah wa Kiislamu utasimama hivi karibuni na kusimamisha tena Dola ya Kiislamu ya Khilafah kwa njia ya Mtume (saw) chini ya uongozi wenye ikhlasi, uwezo, ulio na utambuzi wa kisiasa ambao utaziunganisha tena ardhi za Waislamu, kukomboa maeneo yao yaliyokaliwa kimabavu, kutabikisha sharia ya Kiislamu, irudishe mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu, na kubeba nuru ya Uislamu kwa ulimwengu mzima. Dola ya Khilafah, karibu tangu kuanzishwa kwake, itaingia kwenye safu za dola kubwa kwa sababu ya ukubwa wa eneo lake, idadi kubwa ya watu wake wachangamfu, rasilimali zilizojaa, jografia isiyo na kifani na mfumo wa kipekee wa Kiislamu. Uhasimu mkali na migawanyiko ndani ya hali ya sasa ya kimataifa itaharakisha tu kuibuka kwake. Mwenyezi Mungu (swt) asema katika Qur’an Tukufu:

(تَحْسَبُهُمْ جَمِيعًا وَقُلُوبُهُمْ شَتَّى ذَلِكَ بِأَنَّهُمْ قَوْمٌ لَّا يَعْقِلُونَ)  

“Utawadhania kuwa wako pamoja, kumbe nyoyo zao ni mbali mbali. Hayo ni kwa kuwa wao ni watu wasio na akili.” [Al-Hashr: 14].

Netanyahu Aatarajiwa Kurudi kama Kiongozi wa Umbile Haramu la Kiyahudi

Gazeti la ‘New York Times’ wiki hii linaakisi juu ya mivutano inayotarajiwa katika ya Rais wa Marekani Joe Biden na Waziri Mkuu anayekuja Binyamin Netanyahu wa umbile haramu la Kiyahudi:

Na mnamo Alhamisi, Bw. Netanyahu alijihakikishia kurejea kwake madarakani kwa muungano mpya wa mrengo mkali wa kulia ambao kwa mara nyingine tena utamfanya kuwa waziri mkuu - uthibitisho wa mtindo ng’ang’anizi wa uongozi, ambao umekuwa ndio kitovu cha migongano wake na Bw. Biden na marais wengine wa Marekani kwa miaka mingi.

Viongozi hao wawili watajikuta katika nafasi ya kulumbana upya kuhusu masuala ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakisumbua uhusiano wao.

Ni mahusiano magumu zaidi ya yote, yenye kuyumba kati ya joto na mapambano, wakati mwingine kwa siku moja. Lakini Dennis Ross, mpatanishi wa zamani wa Mashariki ya Kati ambaye alizoea kuandamana na Bw. Biden, alipokuwa makamu wa rais, katika safari za kumuona Bw. Netanyahu, alibainisha katika mahojiano mnamo Alhamisi kwamba uhusiano ulikuwa bora kuliko ule kati ya Bw. Netanyahu na Rais Barack Obama.

"Mtazamo wa Bibi kuhusu Biden ni tofauti na mtazamo wa Bibi kuhusu Obama," Bw. Ross alisema, akitumia lakabu ya kawaida ya Bw. Netanyahu. "Bibi alikuwa na hakika kwamba Obama alikuwa akijaribu kumdhoofisha, na Obama alikuwa na hakika kwamba Bibi alikuwa akifanya kazi na Republican kumdhoofisha."

"Alimuona Biden kama mtu ambaye hangekubaliana naye, lakini moyo na hisia za Biden zote zilikuwa kwa Israel," alisema Dennis Ross, ambaye alisimamia diplomasia ya Mideast katika Baraza la Usalama la Kitaifa katika utawala wa Bw. Obama

Kutoelewana kunabakia. Rais anapendelea dola ya Palestina kutatua mzozo wa miongo kadhaa na Israel. Bw. Netanyahu hapendelei. Waziri mkuu wa Israel aliyataja mapatano ya nyuklia ya Iran ya mwaka 2015 kuwa maafa kwa Israel na eneo hilo. Bwana Biden alisema hiyo ndiyo njia bora ya kuizuia Iran isitengeneze silaha za nyuklia. Na watu hao wawili wamekuwa katika mzozo kwa miaka mingi juu ya ujenzi wa makaazi ya Waisraeli katika ardhi ya Palestina.

Mvutano kati ya umbile haramu la Kiyahudi na Marekani ni wa halisi. Lakini mivutano hii ni kama ile inayosababishwa na mbwa mwenye kichaa mwenye hasira anayejaribu kujitenga na kamba iliyoshikiliwa kwa nguvu na bwana wake. Marekani inataka umbile hilo haramu liwe kali na lichanganyikiwe kwa sababu Amerika inafahamu kwamba Mayahudi ni watu madhaifu sana, wachache katikati ya nchi zenye nguvu na kubwa za Kiislamu. Watawala vibaraka wa Magharibi katika nchi za Kiislamu wanapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kuwazuia Waislamu wao wanyoofu dhidi ya kupigana na kuwafurusha Mayahudi wahalifu wanaowakalia kwa mabavu. Marekani inajua kwamba ikiwa itaachilia kamba, basi mbwa mwenye wazimu atauliwa tu, akijaribu kwa ujinga kupambana na mpinzani mkubwa zaidi na mwenye nguvu zaidi yake. Abu Huraira (r.a.) amepokea kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) akisema:

«لَا تَقُومُ السَّاعَةُ حَتَّى يُقَاتِلَ الْمُسْلِمُونَ الْيَهُودَ فَيَقْتُلُهُمْ الْمُسْلِمُونَ حَتَّى يَخْتَبِئَ الْيَهُودِيُّ مِنْ وَرَاءِ الْحَجَرِ وَالشَّجَرِ فَيَقُولُ الْحَجَرُ أَوْ الشَّجَرُ يَا مُسْلِمُ يَا عَبْدَ اللَّهِ هَذَا يَهُودِيٌّ خَلْفِي فَتَعَالَ فَاقْتُلْهُ إِلَّا الْغَرْقَدَ فَإِنَّهُ مِنْ شَجَرِ الْيَهُودِ»‏

“Kiyama hakitasimam mpaka Waislamu wapigane na Mayahudi na Waislamu watawaua mpaka Mayahudi watajificha nyuma ya jiwe au mti na jiwe au mti useme: Ewe Muislamu au ewe mja wa Mwenyezi Mungu Yahudi huyu hapa nyuma yangu; basi njoo umuue; isipokuwa mti wa Gharqad, kwani ni katika mti wa Mayahudi.” [Sahih Muslim: 2922]

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu