Jumatatu, 28 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/26
Saa hii ni: 02:57:02 (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kuanzia Mjumuiko wa “Matembezi kwa ajili ya Khilafah” yalioandaliwa na Hizb ut Tahrir, watu wanaopenda Uislamu wanawaita watoto wao wa kiume katika jeshi kujitokeza ili kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume; Na ili kuiridhisha Marekani na India, vib

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 101 tarehe 3 Machi, 2025, ya kuondolewa kwa Khilafah tukufu, Hizb ut Tahrir, Wilayah Bangladesh, iliandaa mjumuiko wa “Matembezi kwa ajili ya Khilafah” mnamo siku ya Ijumaa, Machi 7, 2025, baada ya Ijumaa, kutoka kwenye Lango la Kaskazini la Baitul, wakitaka kusimamishwa kwa Khilafah kwa njia ya Utume. Maelfu ya watu wanaopenda Uislamu kutoka matabaka mbalimbali walishiriki kwa hiari katika mjumuiko huu, wakipuuza vitisho vya vibaraka wa Marekani-India. Kutokana na mkusanyiko huu, watu wanaopenda Uislamu waliwaita watoto wao wanaotumikia jeshi kutoa nusrah (msaada wa kimada) kwa uongozi wa dhati wa Hizb ut Tahrir, katika kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Amerika Yala Sanamu Lake Yenyewe!

Katika Arabuni ya kabla ya Uislamu, baadhi ya Waarabu walikuwa wakitengeneza masanamu yao kutokana na tende; walipohisi njaa, wangekula miungu yao! Leo, historia inajirudia yenyewe, lakini kwa umbo gumu zaidi. Mfumo wa Kimagharibi ambao hapo awali uliinyanyua fahamu ya uhuru hadi kwenye hadhi takatifu—uhuru wa fikra, dhamiri, na dini; uhuru wa kuzungumza na kujieleza; uhuru wa kukongamana kwa amani; ushiriki wa kisiasa; ulinzi wa haki za walio wachache; na kukataza utesaji na kutendewa kikatili – sasa unasaliti maadili haya haya yanapokinzana na maslahi ya mabepari na kipote cha watawala.

Soma zaidi...

Watawala Vibaraka Wamefichua Udanganyifu wa Ubwana wa Kitaifa na Maslahi ya Kitaifa. Ni Hoja Gani iliyopo ya Kuzuia Kukomeshwa kwa Mfumo wa uliopo Sasa?

Mnamo tarehe 11 Februari 2025, taarifa kwa vyombo vya habari ilitolewa kwenye tovuti ya Mahakama ya Upeo ya Pakistan, ambayo ilifichua mabaki ya udanganyifu wa ubwana wa kitaifa. Taarifa hiyo kwa vyombo vya habari ilisema kuwa Jaji Mkuu na maafisa wengine wa mahakama walikutana na ujumbe wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) na kuwaeleza kuhusu masuala ya Mahakama ya Upeo. Katika taarifa hiyo, Jaji Mkuu alithibitisha kuwa Mahakama ya Upeo inakamilisha ajenda ya kikao cha Kamati ya Kitaifa ya Mahakama ya Utungaji Sera (NJPMC) katika wiki ya mwisho ya Februari. Hata aliwaalika wajumbe wa wakoloni pia kutoa mapendekezo yao katika suala hili.

Soma zaidi...

Mkutano wa Cairo, kama Watangulizi wake, Unadhihirisha Usaliti wa Watawala wa Kiarabu na Kuitelekeza kwao Gaza na Watu wake!

Gaza haihitaji mipango zaidi inayoiweka chini ya ukaliwaji kimabavu na udhibiti wa Mayahudi. Kinachohitaji kwa hakika ni hatua ya dhati kutoka kwa Ummah na majeshi yake ili kuinusuru na kuikomboa kutokana na mitego ya Mayahudi na Marekani. Bila haya, tutaendelea kuwahesabu mashahidi na majeruhi, tukishuhudia unajisi na kiburi cha Mayahudi—wakati wote huku watawala wa Waislamu wakiendelea kuusaliti Umma na utumwa wao kwa Amerika.

Soma zaidi...

Mkutano wa Cairo Unathibitisha Usaliti wa Watawala wa Kiarabu kwa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Mkutano huo wa dharura wa Waarabu ulifanyika jijini Cairo katikati ya mazingira machungu ambayo Umma wa Kiislamu unapitia, hasa hujuma za Kiyahudi mjini Gaza, na shinikizo la kimataifa linaloongezeka kuhusu kadhia ya Palestina. Kama ilivyotarajiwa, mkutano huo ulitoa taarifa ya mwisho ambayo ilikuwa na maneno ya kulaani na kukashifu, na kutaka masuluhisho ya viraka ambayo hayashughulikii mizizi ya mgogoro huo. Je, tunautazamaje mkutano huu? Na ni upi msimamo juu ya matokeo yake?

Soma zaidi...

Sudan imekua Jeraha jengine Chungu kwa Umma wa Kiislamu

Mnamo tarehe 18 Februari 2025, kikosi cha Rapid Support cha Sudan kilifanya mkutano katika jumba la mikutano ya kimataifa la Kenyatta (KICC) jijini Nairobi kuzungumza uundaji wa serikali ya umoja ya majimbo yanayodhibitiwa na kikosi hicho nchini Sudan. Utawala nchini Kenya unashikilia kudai kwamba kujihusisha kwake kwenye mazungumzo hayo ni kuimarisha “juhudi za amani nchini Sudan”. Nairobi imetetea uamuzi wake wa kuwa mwenyeji wa kufanya mazungumzo na kikosi cha wapiganaji yanayolenga kusainiwa kwa mkataba wa kisiasa. Maafisa wa Kiutawala wa Sudan wameiona hatua hii kama jaribio la kuanzisha utawala mwengine sambamba na ule wa Khartoum, hatua hii ya Kenya imepelekea kulaumiwa kwake kwa kukiuka ubwana wa Sudan na kujihusisha na matendo ya kiuhasama.

Soma zaidi...

Miaka Miwili Iliyopita Baada ya Tetemeko la Ardhi la Februari 6 Bado Mateso Hayana Mwisho

Mnamo Februari 6, 2023, matetemeko makubwa mawili ya ardhi yenye kipimo cha 7.8 na 7.5, yaliyopiga kusini na katikati mwa Uturuki na kaskazini mwa Syria, yaliathiri mikoa 11 na kusababisha uharibifu mkubwa na kupoteza maisha. Takriban watu 54,000 nchini Uturuki na 8,500 nchini Syria walipoteza maisha katika matetemeko haya ya ardhi huku kitovu cha matetemeko hayo kikiwa Kahramanmaraş. Jumla ya waliopoteza maisha ilizidi 62,000, na mamilioni ya watu wakabaki bila makao. Hata hivyo, baadhi ya wataalamu wa huru na rasilimali za ndani zinaonyesha kuwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi.

Soma zaidi...

Watawala wa India Wanatumia Sheria ya (Kuzuia) Shughuli zisizo halali ya 1967 kupiga Vita Uislamu na Waislamu, wakimwemo Mashababu wa Hizb ut Tahrir

Katika kampeni yake inayoendelea dhidi ya Hizb ut Tahrir, Shirika la Kitaifa la Upelelezi la India lilimkamata Bava Bahrudeenand Kabeer Ahmed Aliyar mnamo 3 Februari 2025, baada ya miezi kadhaa ya unyanyasaji. Vyombo vya habari vya India viliripoti kwamba "walikula njama na wengine kueneza fikra ya Hizb ut Tahrir huko Tamil Nadu, ambalo ni shirika lililopigwa marufuku." Kisha mamlaka zikanasibisha kesi yao na kesi inayoendelea ya Dkt. Hameed Hussain chini ya Sheria ya (Kuzuia) Shughuli Zisizo Halali (UAPA) ya 1967!

Soma zaidi...

Marufuku ya Kyrgyzstan dhidi ya Niqab ni Jaribio la Kutapatapa la Utawala wake wa Kisekula Kukandamiza Kuibuka kwa Kitambulisho cha Kiislamu Miongoni mwa Watu wake

Kyrgyzstan imekuwa nchi ya hivi punde zaidi katika Asia ya Kati kupiga marufuku Niqab. Hatua hii ya kisheria ilianza kutekelezwa mnamo tarehe 1 Februari 2025 na ukiukaji huu utatozwa faini ya 20,000 som ($230). Nguo za Kiislamu za wanawake na ndevu za wanaume zimekuwa zikilengwa na serikali za Asia ya Kati kwa muda mrefu, ambapo dola zenye nguvu ya kisekula zinaogopa ushawishi unaoongezeka wa Uislamu. Wabunge wa Kyrgyzstan wametoa kisingizio duni kwamba marufuku hiyo inahitajika kwa sababu za usalama, ili nyuso za watu zionekane na watu binafsi kutambuliwa. Lakini wapinzani wanasema marufuku hiyo inawanyima wanawake uhuru wa kuvaa wanavyotaka.

Soma zaidi...

Enyi Majeshi! Chagueni kati ya Watawala hawa ambao ni Watiifu kwa Trump, na Khalifa Rashid ambaye ataikomboa Gaza na Palestina nzima kupitia Nguvu za Kijeshi!

Mnamo Jumanne 4 Februari 2025, akiwa ameketi ubavuni mwa muuaji wa Gaza, Benjamin Netanyahu, Rais Trump wa Marekani alitangaza, "Marekani itauchukua Ukanda wa Gaza, na tutafanya kazi nayo pia." Tamko la kiburi la Trump kuhusu Gaza ni kofi kwenye uso wa watawala wa Waislamu, ambao wametekeleza kwa utiifu amri ya Marekani, na kuzuia vikosi vya majeshi ya Waislamu kupigana na umbile la Kiyahudi, na hivyo kuruhusu mauaji ya Waislamu nchini Palestina. Watawala wa sasa wa Waislamu, kama wale waliotangulia, wanajifunza kwamba Marekani haiwajali wao, au viti vyao vya khiyana. Marekani itaendelea kuwadhalilisha na kuwashusha hadhi mbele ya dunia na watu wao wenyewe. Kwa hakika, kushiriki katika mfumo wa dunia unaoongozwa na Marekani, na kushikamana na sheria za kimataifa na taasisi za kimataifa, si chochote ila unyenyekevu na utiifu kwa Marekani na rais wake. Hata hivyo watawala hawa hawajali. Hata hivi sasa wanakimbilia kumfurahisha na kumtuliza bwana wao, Amerika, wakijaribu kuwasilisha kwake "mpango wa amani wa Waarabu" wao wenyewe.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu