Jumanne, 14 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/10
Saa hii ni: 19:54:48 (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Wananchi Wanataka Kupinduliwa kwa Serikali na Kusimamishwa kwa Utawala wa Kiislamu

Aden, mji mkuu wa muda wa serikali ya Yemen, umeshuhudia maandamano matatu ya wanawake na wanaume katika wiki mbili zilizopita. Kutokana na mateso yanayoendelea kwa wananchi, maandamano ya hasira yamefanyika mjini Aden, wakidai huduma za msingi na kukemea hali ngumu ya maisha na huduma duni. Maandamano haya yalijumuisha kauli mbiu dhidi ya muungano wa Waarabu, serikali ya Yemeni, na Baraza la Mpito, ambalo linadhibiti mji mkuu wa muda, Aden. Maandamano haya pia yalishuhudia milio ya risasi na kukamatwa kwa baadhi ya waandamanaji. Maandamano haya yalifanywa na wanawake na wanaume kwa siku tofauti. Kilichotia fora ni kuregea kauli mbiu isemayo “Wananchi wanataka kupinduliwa kwa serikali,” ambayo inatukumbusha Mapinduzi ya Kiarabu dhidi ya ukandamizaji na udhalimu.

Soma zaidi...

Maandamano ya Kulaani yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir, Wilayah Bangladesh: “Palestina, Kashmir, Arakan – Khilafah pekee ndiyo Suluhisho”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (23/05/2025) baada ya swala ya Ijumua, iliandaa maandamano ya kulaani katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong dhidi ya wimbi jipya la mashambulizi ya umbile lililolaaniwa la Kiyahudi kuchukua udhibiti wa Ukanda wote wa Gaza.

Soma zaidi...

Nia na Malengo ya Ziara ya Afisa wa Uingereza nchini Uzbekistan

Mnamo Mei 13, 2025, Lord Cocker, Waziri wa Ulinzi wa Uingereza, alifanya ziara rasmi nchini Uzbekistan. Ziara hii ni muhimu kwani ni ziara ya kwanza rasmi nchini Uzbekistan kwa mwakilishi wa serikali mpya ya Uingereza. Wakati wa ziara yake, alikutana na uongozi wa jeshi la Uzbekistan, akiwemo Naibu Waziri wa Ulinzi Kanali Jenerali Hamdam Qarshiyev na Kamanda wa Walinzi wa Kitaifa Luteni Jenerali Rustam Juraev. Mikutano hii ilithibitisha kujitolea kwa Uingereza katika kuimarisha ushirikiano wa ulinzi wa nchi mbili na Uzbekistan. Lord Cocker pia alitoa hotuba katika Chuo cha Jeshi la Uzbekistan, mara ya kwanza kwa Waziri wa Ulinzi wa Uingereza kuzungumza katika chuo hicho.

Soma zaidi...

Ujerumani Yapoteza Fursa ya Kihistoria

Katika maadhimisho ya miaka 60 ya kuanzisha mahusiano ya kidiplomasia na umbile la Kiyahudi, Jamhuri ya Shirikisho ya Ujerumani inapoteza fursa yake ya kihistoria ya kujikomboa kutoka katika hatia iliyotungwa dhidi ya Mayahudi. Badala yake, shauku ya kile kinachoitwa "maslahi makuu ya kitaifa" - kisingizio kinachotumiwa kuhalalisha uungaji mkono usio na masharti kwa umbile la Kiyahudi - yamefikia kilele kipya kwa tangazo kwamba kuunga mkono umbile hili ni "msingi wa kuwepo kwa Ujerumani"!

Soma zaidi...

Bunge la Ulaya na Maazimio ya Ukoloni Mambo Leo

Wiki iliyopita Bunge la Jumuiya ya Ulaya (EU) lilitoa mwito kwa Tanzania kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kutatua kesi waliyosema ina msukumo wa kisiasa ya kiongozi wa chama cha upinzani, kutoa uhuru zaidi wa kisiasa kupitia majadiliano, kufanya mabadiliko ya sheria za uchaguzi,kuheshimu haki ya vyama kushiriki katika uchaguzi huru nk.

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina ilimuua Rami Zahran, Kisha Mzee Mmoja, Ikikamilisha Uhalifu wake Dhidi ya Watu wa Palestina

Mnamo siku ya Jumanne,13/5/2025, vikosi vya usalama vya Mamlaka ya Palestina vilimuua kijana Rami Zahran kutoka kambi ya wakimbizi ya Al-Far'a huko Tubas. Kisha wakafuatilisha hili kwa kumuua mzee mmoja (Abu Khalil al-Saba'neh) kutoka mji wa Jenin. Huu ni mwendelezo wa jinai zake dhidi ya watu wa Palestina, zikiwemo za mauaji, uchomaji moto, ukamataji, uvamizi wa misikiti, na unyang'anyaji mali ya Wapalestina kinyume cha sheria, kula mali zao kwa njia ya dhambi na fujo.

Soma zaidi...

Mwisho wa Enzi ya Awami League, Chama Kinara cha Siasa za Kisekula - ni Onyo la Kihistoria kwa Vyama Vilivyopo vya Kisiasa na Nyuso Mpya za Kisiasa

Kwa kuanguka kwa dhalimu Hasina na tangazo rasmi la kupigwa marufuku kwa shughuli zote za chama kiovu cha Awami League, enzi ya giza ya siasa za chama kikuu cha kisekula -Awami League imekamilika. Kuangamia huku kwa Awami League, mrithi wa 'All India Muslim League' iliyoanzishwa mwaka wa 1906, hakutokani na mlingano wa kisiasa wa mamlaka ya kundi lolote la kisiasa, bali ni ukweli wa kihistoria na usioepukika. Hamu ya Waislamu wa India ni kuishi chini ya utawala wa Kiislamu-Khilafah.

Soma zaidi...

Kukabidhi Uendeshaji wa Operesheni za "Bohari la Kontena la New Mooring " kwa Kampuni ya Wakoloni yenye Ushawishi wa Marekani "DP World" kutatishia Ubwana wa Nchi

Bila kujali ubwana wa nchi, serikali ya mpito inaendelea na mchakato wa kukabidhi huduma na mabohari mbalimbali ya Bandari ya Chittagong muhimu kimkakati na kiuchumi kwa wageni kwa jina la kuongeza uwezo wa bandari kwa kisingizio cha uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni (FDI). Kama sehemu ya hili, mchakato wa kukabidhi Bohari Kuu la Kontena la New Mooring (NCT) la Bandari ya Chittagong linalojitosheleza na la juu zaidi la kuzalisha mapato kwa kampuni ya DP World uko katika hatua zake za mwisho (Daily Jugantor, Mei 6, 2025).

Soma zaidi...

Kanuni Mpya za Kifedha Katu Hazitookoa Raia kutokana na Masaibu ya Kiuchumi

Kwenye Mswada wa Fedha wa 2025/26 uliowasilishwa bungeni, uliosifiwa na serikali iliyoko madarakani kama kichocheo kikubwa cha kiuchumi kwa kuwa hautatoza ushuru mpya au kuongeza uliopo katika mapendekezo ya bajeti ya mwaka huu, serikali inaweka mikakati zaidi katika usimamizi wa kodi na kujaribu kuziba mianya hiyo na kufanya ukusanyaji wa kodi kwa ufanisi. Mswada huu unalenga kupunguza hatua za kuongeza kodi na umependekeza msamaha kutoka kwa VAT ya litania ya bidhaa ambazo kwa sasa hazijakadiriwa.

Soma zaidi...

Hatua Mpya za UN na za Kanda za Kuoanisha Serikali Tawala ya Afghanistan ndani ya Mfumo wa Kisekula wa Dunia

Katika siku za hivi karibuni, Umoja wa Mataifa umekuwa ukifuatilia shughuli zake nchini Afghanistan kwa kasi zaidi kuliko hapo awali. Ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Masuala ya Kibinadamu jijini Kabul na Kandahar, pamoja na mwaliko wa Amir Khan Muttaqi-Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali tawala nchini Qatar, inaashiria juhudi mpya za kuendeleza mipango ya kimataifa na kushawishi serikali ya Afghanistan.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu