Jumatano, 16 Safar 1446 | 2024/08/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kama Umma Mmoja: Waislamu Wanasimama pamoja na Watu wa Bangladesh Dhidi ya Dhalimu Sheikh Hasina

Watu wa Bangladesh—zaidi ya 92% yao ni Waislamu na sehemu ya mojawapo ya Waislamu wengi zaidi duniani—wamejitokeza katika maandamano ya amani yanayoongozwa na wanafunzi dhidi ya dhalimu Sheikh Hasina. Maandamano ya hivi punde yalizuka baada ya serikali inayoongozwa na Hasina kujaribu kuongeza mgawo wa nafasi za kazi serikalini kwa kuwapendelea wafuasi watiifu wa serikali badala ya wagombea wenye sifa stahiki. Sera hii ni ya hivi punde tu katika mfululizo wa vitendo vya rushwa na uonevu vinavyofanywa na serikali ya Awami League tangu iingie mamlakani mwaka wa 2009.

Soma zaidi...

Waislamu wa Pakistan Wanashikiliwa Mateka na Watawala kwenye Mpango Angamivu wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa

Mnamo tarehe 13 Julai, 2024, Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) ulithibitisha katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kwamba Pakistan na IMF wamefikia makubaliano ya kifurushi cha mkopo wa msaada wa dolari bilioni 7, wakidai kuwa “Programu hiyo mpya inalenga kuunga mkono juhudi za mamlaka za kuimarisha utulivu wa uchumi mkuu.”

Soma zaidi...

Utawala wa Hasina kwa Kutumikia Uingereza, Unashiriki katika Vita vya Wakala ili Kulinda Utawala wa Junta wa Myanmar unaoungwa mkono na Uingereza ambao uliua Waislamu wa Rohingya

Mamia ya wanajeshi wa Kikosi cha Walinzi wa Mipaka ya Myanmar (BGP) na Jeshi kwa mara nyengine tena wanakimbilia Bangladesh kwa makaazi salama kutokana na mapigano makali yanayoendelea kati ya kundi la waasi la Arakan Army na junta ya kijeshi ya Myanmar huko Rakhine.

Soma zaidi...

Kujadili Yasiyoweza Kujihami

Baada ya juhudi zilizoratibiwa za Wazayuni zenye lengo la kukashifu sauti zinazoiunga mkono Palestina, zilizoundwa na mfululizo wa makala ya magazeti ya udaku na vipindi vya TV vinavyofafanuliwa kwa batili na dosari, ilidhihirika kwamba wengi wao hawakustahili jibu la heshima hata kidogo.

Soma zaidi...

Sera ya Serikali ya Kisekula nchini Uturuki inayokula Njama Dhidi ya Mapinduzi ya Ash-Sham ndiyo Sababu ya Kulipuka kwa Kiota cha Mapinduzi katika Ukombozi

Kauli za maafisa nchini Uturuki kuhusiana na maridhiano na utawala uliopitiliza na kufunguliwa kwa mipaka kwa ajili ya maandalizi ya uhalalishaji mahusiano na utawala huo, na vitendo vinavyouandama vya ubaguzi wa rangi dhidi ya watu wa Syria hasa wa Kayseri ni matokeo ya kimaumbile ya maneno ya uchochezi dhidi ya watu wa Syria, wakimbizi wanaoukimbia utawala wa Assad, na wanasiasa nchini Uturuki, wawe wenye mamlaka au wa upinzani, yote haya si lolote bali ni kuonyesha sura halisi ya utawala wa Uturuki, ambao unatekeleza mpango wa Marekani katika eneo hilo kufikia kile wanakiita suluhisho la kisiasa na kurudisha yale mabaki ya mji uliokombolewa kwenye kumbatio la utawala wa kihalifu.

Soma zaidi...

Mauaji ya Kikatili dhidi ya Watu Wetu mjini Gaza Bila Uwajibikaji! Lini Tutayaona Majeshi ya Waislamu Yakiinuka?!

Wizara ya Afya mjini Gaza imetangaza kuwa mashahidi 79 na majeruhi zaidi ya 289, baadhi yao wakiwa katika hali mahututi, wamewasili katika hospitali ya Nasser Medical Complex kufuatia mashambulizi ya mabomu kwa kambi za watu waliokimbia makaazi yao huko Mawasi Khan Yunis. Mauaji haya yanajiri baada ya uvamizi huo kufanya mauaji ya kutisha katika eneo la viwandani la kitongoji cha Tel al-Hawa, katika vitongoji vya Mji wa Gaza, na katika kambi za eneo la kati, na kusababisha zaidi ya mashahidi 100, na kuongeza kwa kasi idadi ya majeruhi.

Soma zaidi...

Serikali ya Misri Inayakusanya Makundi ya Sudan kwa Manufaa ya Marekani na Kumakinisha Mamlaka yake, Sio kwa Manufaa ya Taifa au Watu wa Sudan!

Mnamo siku ya Jumamosi, tarehe 6 Juni 2024, kongamano la vikosi vya kisiasa vya kiraia vya Sudan lilizinduliwa katika mji mkuu wa Misri, Cairo, katika jaribio jipya la Misri kumaliza vita vinavyoendelea nchini Sudan. Waangalizi wanaamini kuwa jaribio hili linaweza kuweka msingi wa mazungumzo mapana, huku wengine wakipuuza umuhimu wa mafanikio ambayo linaweza kufikia. (Al-Araby Al-Jadeed).

Soma zaidi...

Kongamano la Cairo Larudisha tena Utawala ule ule Uliosababisha Migogoro na Kuichana Nchi

Jana, Jumamosi, tarehe 6 Julai 2024, lile linaloitwa Kongamano la Kisiasa na Majeshi ya Kiraia ya Sudan lilifanyika katika mji mkuu wa Misri, Cairo; nukta muhimu katika taarifa ya mwisho zilizotolewa zilikuwa: “...wanakongamano pia walisisitiza ulazima wa kushikamana na Azimio la Jeddah na kuzingatia taratibu za utekelezaji na maendeleo yake ili kuendana na maendeleo katika vita…

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu