Jumatatu, 27 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/09/30
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Makongamano ya Kimataifa, Mipango ya Amani, Pasi na Kukomesha Wala Kupunguza Mashambulizi ya Mabomu ya Urusi!

Matukio ya umwagikaji damu yanayojiri Mashariki mwa Ghouta na Idlib; Mtandao wa Kutetea Haki za Kibinadamu wa Syria umesema kwamba raia wapatao 370 wameuwawa Mashariki mwa Ghouta tangu mwanzoni mwa mwaka huu, ukitaja kuwa miongoni mwa wafu ni watoto 63 na wanawake 72. Katika eneo la Idlib, hususan mji wa Sarakib, ambao ndio uliolengwa kwa dhoruba hii tangu mnamo 25 Disemba, Warusi na serikali ya kihalifu ya Syria zimemwaga chuki zake dhidi yake, ikitangazwa na baraza lake la mji kuwa eneo lililo kabiliwa na janga, ambapo idadi ya vifo mwezi Januari ilikuwa ni watu wapatao 30 na zaidi ya raia 60 kujeruhiwa. Hii ni ikiongezewa na kulengwa kwa mashule na mahospitali, ambazo idadi yake kubwa haziendeshi tena shughuli zake.

Soma zaidi...

Watoto wa Iraq … Uhalisia Unaoogofya na Mustakbali Unaotoa Bishara ya Miaka Mingi ya Kuzorota!

Hazina inayoshughulikia maswala ya watoto ya Umoja wa Mataifa (UNICEF) imesema katika ripoti iliyotolewa mnamo Ijumaa 19/1/2018 kuwa watoto 270 waliuwawa nchini Iraq mwaka jana kwa sababu ya vita vilivyo anzishwa na serikali ya Iraq dhidi ya ISIS. Vita hivi pia vilisababisha watoto 1.3 milioni kukosa makao miongoni mwa 2.6 milioni waliokosa makao kutokana na vita hivi vya miaka mitatu. Kulingana na taarifa hiyo, watoto milioni nne katika mikoa ya Nineveh na Anbar waliathirika na ghasia hizo na watoto wengi walilazimika kushiriki katika vita safu za mbele. Taarifa hiyo ilifichua kwamba umasikini na mizozo ilisababisha kusita kwa mchakato wa elimu kwa watoto milioni tatu kote nchini Iraq, baadhi yao wakikosa kabisa fursa ya kukaa ndani ya darasa katika maisha yao yote, huku zaidi ya robo ya watoto wa Iraq wakiishi ndani ya umasikini.

Soma zaidi...

Taasisi za Dola Nchini Tanzania Zimewakamata kwa Dhulma Wanachama Watatu wa Hizb ut Tahrir Bila ya Sababu Yoyote!

Hizb ut Tahrir / Tanzania inashutumu vikali vitendo vya mamlaka za dola zilizo wakamata wanachama wake watatu na kuwafungia pasi na kuwa na mawasiliano yoyote bila ya maelezo au uwakilishi wa kisheria kwa zaidi ya mwezi mmoja kinyume na sheria kisha kubuni mashtaka ya uongo na maovu dhidi yao ya 'njama ya kutekeleza ugaidi' na 'utekelezaji ugaidi'. 

Soma zaidi...

Siasa za Chuki na Migawanyiko ni Dalili Tosha ya Kufilisika Kifikra kwa Siasa ya Demokrasia na Wafuasi Wake

Hatimaye, rais Uhuru Kenyatta ameapishwa kuhudumu kwa muhula wa pili kwenye sherehe iliohudhuriwa na viongozi wa mataifa mbalimbali na kususiwa na wanasiasa wa upinzani. Hafla hii imekuja huku nchi ikighubikwa na migawanyiko ya kikabila, semi za chuki na umwagikaji wa damu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu