Juu ya Kumbukumbu ya 97 ya Kuvunjwa Dola ya Khilafah:
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hakuna ikhtilafu kuwa sharia za Dola ya Khilafah ni miongoni mwa fiqhi ya vitendo, na wala si katika maswala ya Aqeeda.
Hakuna ikhtilafu kuwa sharia za Dola ya Khilafah ni miongoni mwa fiqhi ya vitendo, na wala si katika maswala ya Aqeeda.
Mwishoni mwa mwezi huu mtukufu wa Rajab, mataifa ya kirasilimali na ya kikoloni baada ya kupangiliwa vizuri kwa njama na mikakati ya muda mrefu yalifaulu kuivunja Dola ya mwisho ya Kiislamu ya Khilafah Uthmaniya ambayo makao yake makuu yalikuwa nchini Uturuki, tukio ambalo lilifikia kileleni mwake mwishoni mwa Rajab 1342 H / Machi 1924 M.
Mwishoni mwa mkutano wa 32 wa kamati ya kieneo ya kupambana na ugaidi ya Shirika la Ushirikiano la Shanghai (SCO), uliofanywa mnamo Alhamisi, Aprili 5, 2018 jijini Tashkent, Jenerali Sergev Smirnov,
Kuanzia mwanzoni mwa kazi ya Hizb ut Tahrir nchini Uzbekistan, watu waliitikia ulinganizi kwa moyo mkunjufu – watu tofauti tofauti, kutoka matabaka mbali mbali walivutiwa na fikra za Hizb.
Katika ripoti iliyo chapishwa na kituo cha habari cha Al-Jazeera idhaa ya Kiingereza, maafisa wa Umoja wa Mataifa (UM) walishutumu kuendelea kukamatwa kiholela kwa watoto katika Ardhi Tukufu (Palestina) na umbile la Kiyahudi, ikisema kuwa “Unyimaji uhuru huu kwa watoto hawa ni wa kitaasisi, kinidhamu, na ulio enea pakubwa”. Msururu wa ripoti za UM zilizo wasilishwa katika lile linaloitwa Baraza la Haki za Kibinadamu zimeonyesha jinsi hali za maisha za watu wa ardhi tukufu ya Palestina na Ukingo wa Magharibi na Gaza zilivyo zidi kudorora kwa zaidi ya mwaka mmoja uliopita, na jinsi watoto wanavyo himili ukatili wa uvamizi wa umbile la Kiyahudi, kwa mujibu wa Kate Gilmore, Naibu Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa UM.
Tangu Februari 18, majeshi katili ya serikali ya Syria yakisaidiwa na jeshi la anga la Urusi yameendelea na mashambulizi yao makali dhidi ya eneo la Mashariki mwa Ghouta, baada ya kuligawanya kuwa sehemu tatu za kivita. Natija yake, yaliweza kudhibiti zaidi ya asilimia 80 ya eneo hili lililo karibu na mji mkuu wa Damascus, ambalo tangu mwaka wa 2012 limekuwa ngome kubwa zaidi na muhimu zaidi kwa makundi ya upinzani.
Mnamo Jumanne, Machi 6, wanawake kutoka nchi 55 walitoka katika “msafara wenye utu” kuanzia Istanbul mpaka Hatay. Lengo lao likiwa ni kunyanyua rai jumla juu ya wanawake 6,736 wakiwemo wasichana 417 wanaoteseka katika magereza ya serikali ya Assad, wakisubiri kifo chini ya mateso na ubakaji wa kila siku. Magereza hayo yamejaa wanawake wazee, waja wazito na wanawake waliojifungua punde tu kabla ya vifungo vyao. Inajulikana kuwa wanawake wanaopitia uchungu wa ubakaji na mateso aghalabu hujiua wanapo pata fursa ya kufanya hivyo.
Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa linalo shughulikia ufadhili wa watu (UNFPA) limesema kuwa wanawake katika kambi za wakimbizi nchini Syria wamekuwa wakidhulumiwa kimapenzi na wanaume wanaotoa misaada kwa niaba ya UM na mashirika ya kimisaada ya kimataifa. Ripoti hiyo, “Sauti kutoka Syria 2018”, ili eleza kwa kina namna wanawake wakimbizi wa Syria wanavyo lazimishwa kutoa ngono kama badali kwa chakula kutoka UM, na kwamba dhulma hii imeenea maeneo yote kusini mwa Syria.
Zaidi ya mashambulizi ya angani 2000 yalifanywa na jeshi la anga la Urusi (mashambulizi 1150) na jeshi la anga la Syria (mashambulizi 900) na kuangamiza watu na ardhi; yaliangamiza mahospitali, masoko ya mboga na viwanda vya kuoka mikate, yakiuwa mashahidi 900 na kujeruhi raia 2000 wasiokuwa na silaha.
Mnamo 22 Februari, shirika la Kiingereza la kuchunguza haki za kibinadamu za watu wa Syria lilisema kuwa zaidi ya watu 400 waliuwawa, ikiwemo watoto 150 katika shambulizi baya la mabomu lililopita la siku 5 Mashariki mwa Ghouta lililofanywa na majeshi katili ya Syria na Urusi, ambayo yanalenga kiholela nyumba za raia, maduka, mashule, mahospitali na masoko, yakiwaacha watoto wakiwa wamezikika katika vifusi vya majumba. Watoto wamelazimika kutafuta hifadhi katika mapango, mashimo au mivungu ya nyumba zao huku 'wakisubiri zamu yao kufa'.