Alhamisi, 17 Safar 1446 | 2024/08/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Marufuku ya Niqab huko Uholanzi imepelekea Stara kuwa ni Uhalifu, Inathibitisha kwa Mara Nyingine Namna Ubaguzi wa Dini Umekita Mizizi ndani ya Nidhamu ya Kisekula ya Kihuria

Mnamo 1 Agosti, marufuku ya Niqab yalianza rasmi ndani ya Uholanzi, yakiwazuia wanawake Waislamu kutovaa kizuizi nyusoni mwao wanapokuwa katika taasisi za umma, ikijumuisha shule, hospitali na afisi za serikali pamoja na mabasi na treni.

Soma zaidi...

Wanawaogopa Watoto… Je, Jeshi Kubwa la Waislamu Itakuaje?!!

Majeshi vamizi ya umbile la Kiyahudi yalimwita mtoto Malak Sidr (umri wa miaka 8, kutoka katika mji wa Hebron (Al-Khalil) baada ya kuvamia nyumba ya familia yake katikati mwa mji huo na kumpa babake ilani ya kutaka kumhoji mtoto huyo kwa mashtaka ya kuleta usumbufu kwa walowezi hao.

Soma zaidi...

Kama Ambaye Hali Ilikuwa Bora kabla Kuwasili kwa Maelfu ya Wanawake na Watoto Wakimbizi!

Mnamo 10/05/2019, maamuzi yalipitishwa na Baraza la Ulinzi wa Juu kuvunjilia mbali majengo hayo ya simiti katika kambi za wakimbizi na kuipa kila familia sehemu iliyojengwa kwa mashiti na mbao ndani ya saa 24 za ubomozi huo wa vyumba vya simiti ambao haukufanyika.

Soma zaidi...

Mauaji Dhidi ya Watoto wa Yemen yanaendelea, ilhali Wauaji wanacheza dori ya Waweka Amani

Mnamo 26 Aprili, Umoja wa Mataifa ulipeperusha ripoti kwamba idadi ya waliofariki ndani ya Yemen kutokana na mzozo unaoendelea unatarajiwa kupita 230,000 mwishoni mwa 2019. Utafiti kwa kichwa “Tathmini ya Athari ya Vita Juu ya Maendeleo ndani ya Yemen”,  pia iliripoti kuwa Wayemen 131,000 watakuwa wamefariki kutokana na athari mbaya za vita baina 2015 na 2019 mfano kutokana na njaa, maradhi na kukosekana kwa kliniki za afya. Kwa mujibu wa UN mwishoni mwa mwaka, mapigano yatakuwa yamechukuwa maisha ya watu 102,000.

Soma zaidi...

Ongezeko la Takwimu Sio Jipya Bali Halina Budi kwa Zabuni za Kifedha Kabla ya Kongamano la Wafadhili la Brussels kwa Ajili ya Syria

Vita katili nchi Syria dhidi ya raia vimeingia mwaka wake wa tisa mnamo Machi 15. Zaidi ya watu nusu milioni wamekufa, kwa mujibu wa ripoti za kimataifa, na shirika la Uangalizi wa Haki za Kibinadamu la Syria limenakili vifo 19800 vya watoto tangu 2011. Inakisiwa watoto milioni 8.6 wanahitaji msaada wa dharura, na sasa zaidi ya watoto milioni 6 hawana makao au wanaishi kama wakimbizi, na baadhi ya milioni 2.5 yao hawendi shule. Zaidi ya watoto milioni 3 wako katika hatari ya mabomu ya ardhini, huku takriban asilimia 40 ya wale waliouwawa na mabomu ya ardhini wakiwa ni watoto. 

Soma zaidi...

Janga la Watoto Wachanga Linafichua Hali Mbaya ya Sekta ya Afya Nchini Tunisia na Kudhihirisha Kufeli kwa Serikali Hiyo Katika Kuchunga na Kulinda Watu Wake!

Janga chungu liliitingisha rai jumla nchini Tunisia wiki jana! Watoto wachanga kumi na tano walikufa katika Hospitali ya Wassila Bourguiba kwa mujibu wa takwimu rasmi na idadi inazidi kuongezeka. Mnamo Ijumaa, Machi 15, msemaji wa Afisi ya Mkuu wa Mashtaka ya Ummah alisema “idadi ya watoto wachanga waliokufa katika Hospitali ya Wassila Bourguiba ilikuwa ni 15.” Janga hilo lilifuatiwa na jengine baya zaidi, kila mojawapo likiifichua dola hiyo kuwa haiangalii watu wake!

Soma zaidi...

Hakutakuwepo na Hadhi, Usalama na Ustawi kwa Wanawake Waislamu Bila ya Kusimamisha Khilafah Rashidah

Rajab hii inatukumbusha tukio baya mno, miaka 98 iliyopita pale Ummah wa Waislamu ulipopoteza dola yake adhimu, uongozi wake wa Kiislamu, mlinzi na ngao yake –Khilafah. Tokea wakati huo, wanawake Waislamu na familia zao wamejipata katika maangamizi ya mauaji, njaa, uvunjwaji, adhabu, kukosewa heshimu, umasikini wa kupindukia, upweke, ukandamizaji na madhila yasiyovumilika. Tumetoka kutoka kuwa chini ya dola iliyokuwa ina tawaliwa na viongozi wachamungu wakiwahudumia Ummah kwa huruma na kujali mahitaji yao kama alivyoamrisha Mwenyezi Mungu (swt)… kiasi kwamba Ummah upo chini ya viongozi wasiojali lolote kuwahusu, wanaoiba mali zetu kwa kujitajirisha, na kuwaadhibu Waislamu wanaoshikamana kikamilifu na Dini yao. Kutoka kuwa dola kubwa yenye kubeba Jihad kueneza Uislamu ili ikomboe miji, na iliyowafanya maadui zake kutetemeka kwa uoga kila wanapofikiria kumdhuru mwanamke Muislamu…tumekuwa wahanga wa mauaji na uvamizi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu