Vita vya Fitna Vinaweza Tu Kwisha kwa Kuunganisha Pakistan na Afghanistan kama Dola Moja ya Khilafah
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Pakistan ilipoteza wanajeshi ishirini na watano katika Dera Ismail Khan wa Khyber Pakhtunkhwa, mrengo wa masuala ya vyombo vya habari wa jeshi (ISPR), ulisema mnamo tarehe 12 Disemba 2023. Tehreek-i-Jihad Pakistan (TJP), kundi jipya linaloshirikiana na Tehreek-i-Taliban Pakistan (TTP), ilidai kuhusika na shambulizi kwenye kituo cha ukaguzi.