Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 409
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Theluthi moja ya Pakistan ilikabiliwa na mafuriko. Zaidi ya watu 1500 walipoteza maisha. Nyumba milioni moja ziliharibiwa. Watu milioni thelathini na tano waliathiriwa na mafuriko, wakiwemo watoto milioni kumi na sita.
Kenya inagubikwa na wasiwasi wa kiwango chake cha madeni kufikia shilingi 9.1 trilioni. Sajili ya hivi punde ya deni la Hazina ya Kitaifa inaonyesha deni la taifa lilifikia Sh 8.2 trilioni kufikia Disemba mwaka jana. Jumla ya mkopo wa nje ulikuwa Sh 4.174 trilioni huku mikopo ya kimataifa ikiwa Sh1.782 trilioni, kibiashara Sh1.208 trilioni na baina ya Sh1.17 trilioni. Kenya huenda ikalazimika kukagua kikomo chake cha deni angalau mara mbili katika muda wa miezi 24 ili kuunda nafasi ya kukopa kwa serikali itakayokuja baada ya ile ya Uhuru Kenyatta.
Viongozi wa mamlaka nne zinazojitangaza kuunga mkono uvamizi wa Urusi katika maeneo ya Luhansk, Donetsk, Zaporizhzhia na Kherson ya Ukraine walitangaza nia yao ya kufanya "kura za maoni" kuhusu maeneo yao yatakayojiunga na Shirikisho la Urusi kuanzia Septemba 23-27.
Kuporomoka kwa jengo la makaazi katika eneo la Al-Weibdeh katikati mwa mji mkuu, Amman, siku ya Jumanne, kumesababisha vifo vya watu 9 na kujeruhi wengine 10, katika hali isiyokwisha, huku msako wa kuwatafuta manusura ukiendelea kwenye vifusi. Kuna habari ambazo hazijathibitishwa juu ya uwepo wa zaidi ya watu 10 chini ya vifusi, ambao kati yao wako hai, na Manispaa ya Amman imeondoa watu kwenye majengo 4 karibu na jengo lililoporomoka.
Mnamo Novemba 20,1922, katika Kongamano la Lausanne, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza George Curzon aliweka masharti manne kwa nchi yake kukubali kuutambuliwa uhuru wa Uturuki, nayo nii: kuondolewa kabisa kwa Khilafah, kufukuzwa khalifa nje ya mipaka, kunyang'anywa pesa zake, na tangazo kwa dola ya kisekula!
Benki Kuu ya Zimbabwe hivi karibuni imezindua sarafu mpya ya dhahabu inayoitumainia kutokamana nayo itapunguza mahitajio ya pesa za kigeni.
Utawala katili wa China unaendelea na mauaji na ukatili katika eneo la Turkestan Mashariki ambayo iliikalia kimabavu kwa miongo kadhaa bila ya kupungua, ambapo dola ya China, ambayo imewafungia mamilioni ya Waislamu wa Uyghur katika kambi za uzuizi kwa jina la (utoaji elimu), inatumia mateso kama silaha ya kutaka kuwaondoa Waislamu wa Turkestan Mashariki kutoka kwenye kitambulisho chao cha Kiislamu kwa kushajiishwa na watawala walio kimya katika nchi za Kiislamu
Tangu kuanzishwa kwake, Mamlaka ya Palestina (PA) imekuwa ikifanya kazi kwa uovu, hofu na vitisho ili kuwatiisha watu wa Palestina na kuwafanya kuwa windo rahisi kwa maadui zao. Mara hufinika uhalifu wake kwa sheria na mara nyingine hupuuza sheria.
Hizb ut Tahrir [HT] ni chama cha kisiasa cha kilimwengu ambacho fikra yake ni Uislamu na lengo lake pekee ni kurejesha njia ya maisha ya Kiislamu kwa kuirejesha tena Khilafah. Tokea kuanzishwa kwake mnamo 1953, katika Al-Quds (Jerusalem), fikra yake na njia yake ya kufikia lengo hili zimechimbuka katika ufahamu wa ndani wa Uislamu, Aqida yake na nidhamu zake.