Jumanne, 28 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/10/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaelekea Wapi, Enyi Munao Simamia Muongozo wa Utoaji Fatwa wa Kiulimwengu?!!

Baadhi ya wanaume wa Al-Azhar wanaendelea kutembea juu ya barabara ya kuushambulia Uislamu na Hukmu zake pasi na maono wala hofu kwa Mwenyezi Mungu (swt). Wanaendelea kuifanya Al-Azhar Al-Sharif – ambayo ilikuwa ndio ngome dhidi ya njama za maadui wa Uislamu – jukwaa ambalo wanavishambulia vipengee vya Uislamu na Hukmu zake zinazo husiana na wanawake. Meza ya Utoaji Fatwa wa Kiulimwengu ya Jumba la Fatwa la Misri (Dar al-Ifta) zilisema kuwa, “fatwa juu ya kadhia ya ndoa kwa watoto wadogo zimeifunga ndoa kwa watoto wadogo katika mahusiano ya kijinsia pekee, na kwamba Hizb ut Tahrir imeifunga ndoa katika mahusiano ya kijinsia pekee, ikiondoa upande wa kisaikolojia, kiafya, kiakili na mambo ya kimwili, na kuweka mbali kiwango cha uvumilivu na jukumu ambalo mkataba wa ndoa unalazimisha juu ya pande zote mbili …” Hili, kwa kuanzia, linagongana na yale ambayo Quran Tukufu imeeleza kuhusu fahamu ya ndoa kama utulivu na huruma.

Soma zaidi...

Jinsi Siasa Inavyo Fanana na Zamani … Matukio Yanaendelea Kama Wanavyo Endelea Watazamaji!

Wanajeshi madhalimu wa umbile la Kiyahudi walimuua msichana kutoka Palestina kwa kummiminia risasi katika kituo cha upekuzi cha al-Za’im, mashariki mwa ardhi iliyo kaliwa Al-Quds (Jerusalem). Shahidi huyo ni mwanafunzi wa shule ya upili aliyekuwa amebeba mkoba wake wa shule wakati wa kuuwawa kwake; aliuwawa kutokana na madai ya kujaribu kutekeleza oparesheni ya kudunga kisu. Majeshi hayo vamizi yalizuia wahudumu wa ambulensi kutomfikia ili kumpa tiba. Aliachwa kuvuja damu hadi kufa.   

Soma zaidi...

Maradhi ya Utaifa Yamepelekea Kukamatwa kwa Wanawake na Watoto Wanaonyanyaswa wa Rohingya na Serikali ya Saudia

Mamia ya Waislamu wa Rohingya wanawake na watoto, waliokimbia mauwaji na ubakaji wa halaiki kutoka kwa Mabudha wenye misimamo mikali nchini Myanmar, wanaendelea kuzuiliwa pasipo kujulikana hatima yao katika Kituo cha Kizuizi cha Shumaisi nchini Saudi Arabia, baada ya kutafuta hifadhi katika dola hiyo.

Soma zaidi...

Je, Watoto wa Kambi ya Wakimbizi ya Al-Rukban Wataachwa Wafe kwa Baridi na Njaa, Huku Wakikosa Mtu Yeyote wa Kuwaokoa?!

Watoto kumi na tano wasio na makao, wengi wao wakiwa wachanga, wamekufa nchini Syria kutokana na baridi kali na ukosefu wa matibabu, kwa mujibu wa ripoti ya UNICEF mnamo Jumanne 15/1/2019. Watoto, 13 kati yao walio chini ya umri wa mwaka mmoja, walifariki katika kambi ya Al-Rukban kusini mashariki mwa Syria, karibu na mpaka wa Jordan. Al-Rukban na kambi nyenginezo zinakumbwa na uhaba mkubwa sana wa misaada ya kibinadamu, pindi wakimbizi wanapowasili baada ya safari nzito baada ya kukimbia ngome ya mwisho ya ISIS mashariki mwa nchi hiyo. Geert Cappelaere, mkurugenzi wa UNICEF wa eneo la Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, alisema “Baridi kali zaidi na hali mbaya za maisha katika Al-Rukban zimesababisha maisha ya watoto kuongezeka kuwa hatarini,” aliongeza, “Kwa mwezi mmoja tu, kwa uchache watoto wanane wamekufa – wengi wao wakiwa chini ya umri wa miezi minne, na mdogo wao zaidi akiwa umri wa saa moja.”   

Soma zaidi...

Majanga Halisi Maovu Hata Bila ya Kuwepo Dhoruba za Barafu

Wakimbizi katika kambi za kinyama kadha wa kadha wameyaomba usaidizi mashirika ya misaada na wametoa wito kwa msaada wa dharura kutoka kwa mamlaka husika. Wamesema kuwa ni kiwango kidogo pekee cha msaada ndio kimewafikia wakaazi katika kambi, ambacho hakitoshi kwa asilimia 10 ya idadi jumla ya wakimbizi katika kambi, katika wakati ambapo kuna uhaba mkubwa wa mafuta na njia za kujikanza moto katika hali mbaya za anga kama hizo ambazo zimelikumba eneo zima la Ash-Sham.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia Inatangaza Uzinduzi wa Kampeni: Na nani aliye mbora zaidi katika kuhukumu kuliko Mwenyezi Mungu

Tunisia hivi sasa imo katika kipindi kigumu baada ya wale tuliowafikiria kuwa ni watawala kuyatelekeza majukumu yao msingi na kuziwachia dola za msalaba za kikoloni na wafanyikazi wake ndani ya Umoja wa Ulaya na Shirika la Fedha la Kimataifa kuamua sera za kiuchumi, kifedha na kijamii mpaka nchi ikadhibiti usambaratikaji wa kiuchumi licha ya kwamba kulikuwa na madeni makubwa.

Soma zaidi...

Kuwapokonya Ummah Utawala wao, Kuwakandamiza na Kushambulia Matukufu yao ni Moja katika Uhalifu Mkubwa dhidi ya Uislamu na Waislamu

Tawala za ukandamizaji na udhalimu hususan utawala wa kihalifu na ukandamizaji wa Ash-Sham, umekuwa ukiwapokonya Ummah maamuzi yao, ukiyakosea heshima matukufu yao, na kuwafuatilia kinyama kupitia taasisi za ujasusi ili kuwatia hofu kiasi kwamba watu wameshindwa mpaka kuzungumza na ndugu zao kuhusu masuala ya ummah.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu