Jumatatu, 27 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/09/30
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Canada imetumana ujumbe kwa Ubalozi wa Pakistan kutaka kuachiliwa kwa Dada Romana na Dada Roshan ndani ya Pakistan

Hizb ut Tahrir / Canada imetumana ujumbe rasmi kwa Ubalozi wa Pakistan ndani ya Toronto ukiomba kwa mamlaka za Pakistan kutimiza jukumu (Fard) lao la Kiislamu la kuwaachilia Dada Romana na Dada Roshan. Kama ilivyoelezewa katika taarifa kwa vyombo vya habari waliyokabidhi ubalozi ikiwa ni sehemu ya ziara hii, dada hawa walitekwa nyara na mamlaka za Pakistan na sehemu waliko haijulikani.

Soma zaidi...

Kampeni ya Hizb ut Tahrir Nchini Sweden: Tumia sauti yako, lakini sio katika uchaguzi!

Risala msingi ya kampeni hii imekuwa ni namna gani Waislamu wanavyo weza kuchangamka katika jamii pasi na kulegeza msimamo wa kitambulisho chao cha Kiislamu.  Kampeni hii na yaliyomo ndani yake imezungumziwa kwa hamu miongoni mwa Waislamu pamoja na mitandao ya kijamii. Imefaulu kuwasilisha barabara mtazamo wa Kiislamu na kuathiri mdahalo kuhusu uchaguzi nchini Sweden na harakati ya kisiasa ya Kiislamu. Kampeni hii pia iliifikia tanabahi kubwa ya vyombo vya habari na imekashifiwa kwa kufanya kazi dhidi ya demokrasia.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Tanzania ilituma Ujumbe kwa Ubalozi wa Pakistan Jijini Dar es Salaam

Kufuatia utekaji nyara wa aibu kwa dada yetu Romana na Dada Roshan pamoja na mumewe kulikotekelezwa na Mamlaka ya Pakistan kwa sababu tu wanaunga mkono ulinganizi (da'wah) wa Kiislamu kupitia Hizb ut Tahrir, Hizb ut Tahrir / Tanzania mnamo 20 Agosti 2018 ilituma ujumbe kwa Ubalozi wa Pakistan nchini Tanzania kuukabidhi taarifa mbili kwa vyombo vya habari kuhusiana na suala hilo hasa.

Soma zaidi...

Faini ya Kwanza ya Denmark kwa Wanawake Wanaovaa Niqab Itawasukuma Waislamu Kushikamana na Maadili ya Kiislamu Hata Zaidi!

Mnamo Agosti 4, 2018, shirika la habari la BBC liliripoti juu ya mwanamke wa kwanza wa Kiislamu kulipishwa faini nchini Denmark kwa ajili ya kuvaa niqab hadharani. “Bunge la Denmark liliidhinisha mswada mnamo Mei 2018 wa kumwadhibu yeyote anayevaa niqab kwa faini” (BBC, 31 Mei 2018). Kwa sasa sheria hiyo haitaji burka na niqab kwa majina, bali inaeleza, “Yeyote anayevaa nguo inayofinika uso hadharani ataadhibiwa kwa faini”. Marufuku hiyo ilipangwa kuanza utekelezwaji wake mnamo Agosti 2018. Mnamo Ijumaa 3 Agosti 2018 mwanamke wa Kiislamu mwenye umri wa miaka 28 aliyekuwa amevaa niqab katika soko kuu la hadhara mjini Horshom, km 25 (maili 15) kaskazini mwa Copenhagen, alishambuliwa kwa nguvu na mwanamke mwengine aliyepinga vazi lake na kuchukua hatua mikononi mwake kumvua kwa lazima vazi hilo la Kiislamu. Polisi waliitwa katika eneo hilo la “vita” na baada ya kuangalia kanda ya CCTV walimweleza mwanamke huyo wa Kiislamu kuwa angelipishwa faini ya kroner 1,000 ($155; £120) baada ya kukataa kuvua niqab hiyo kwa agizo la polisi. Kwa sasa faini hiyo imeongezeka mara kumi zaidi hadi kroner 10,000 ($1,500; £1,200) kwa wahalifu wanaorudia kosa.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu