Jumatatu, 27 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/09/30
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Onyesho la Mshikamano nchini Malaysia huku Hali mjini Gaza Ikizidi kuwa Mbaya

Hali mjini Gaza inazidi kuwa mbaya. Umbile haramu la Kiyahudi linaendelea na mashambulizi yake, na kusababisha idadi ya vifo ambayo sasa imefikia 37,000, na zaidi ya 82,000 kujeruhiwa. Inajulikana sana kuwa hakuna maeneo salama kabisa yaliyosalia kwa wakaazi wa Gaza kutafuta kimbilio kutokana na mashambulizi ya umbile hilo haramu la Kiyahudi. Takriban Waislamu wote wa Gaza sasa wanalazimika kuyahama makaazi yao, wakitafuta hifadhi hadi kusini mwa Rafah, karibu na mpaka wa Misri.

Soma zaidi...

Vifo vya Hajj ni Kosa la Utawala wa Saudi kutokana na Ukosefu wao wa Ustawi kwa Wageni wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu

Zaidi ya mahujaji Waislamu 1,300 waliripotiwa kufariki wakati wa Hija ya kila mwaka, au hija ya Makka, mwezi huu nchini Saudi Arabia, ambapo halijoto imepanda zaidi ya nyuzi joto 50 (nyuzi 122 za Fahrenheit). Mfiduo usiodhibitiwa wa joto kali unaweza kusababisha aina mbalimbali za madhara ya kiafya yanayojulikana ikiwemo kufeli kwa viungo vya mwili na hata kifo.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Kutaka Kuhamasishwa Majeshi ili Kuinisuru Gaza Kutaendelea licha ya Ukamataji Mashababu wa Hizb ut Tahrir!

Watawala wa Pakistan wanawatia mbaroni miongoni mwa safu za Hizb ut Tahrir/Wilayah Pakistan ili kuizuia Hizb kutaka kuhamasishwa jeshi la Pakistan kuinusuru Gaza. Lakini Umma mzima unatoa wito kwa majeshi yake kupigana jihad ili kufikia moja kati ya mema mawili ili kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa, basi ukamataji huo utawazuia vipi watu wake?!

Soma zaidi...

Modi Atafuta Ushindi wa Uchaguzi kupitia Mateso ya Waislamu na Kuvunja Misikiti yao na Nyumba zao

Siasa za uchaguzi za Modi zinaegemea kueneza chuki za kidini dhidi ya Waislamu, katika maisha yake yote ya kisiasa. Wakati alipokuwa ni Waziri Kiongozi wa Gujrat mnamo 2002, Narendra Modi, alisimamia mauaji ya Waislamu zaidi ya elfu mbili. Mnamo tarehe 1 Machi 2002, katika kilele cha uchinjaji Modi alidai kwamba, “Kila kitendo kina majibu sawa na majibu ya kinyume yake (Har kriya ki pratigriya hoti hai).” Baadaye, akiwa waziri mkuu amesimamia uharibifu wa misikiti, ubomoaji wa nyumba za Waislamu na mashambulizi ya makundi ya watu dhidi ya jamii za Waislamu.

Soma zaidi...

Hakuna Uamuzi wa Kisiasa wa Mahakama Utakaositisha Wito wa: “Israel” Lazima Iondolewe na Palestina Yote Ikombolewe

Mnamo siku ya Jumanne tarehe 25/6/2024, nilihukumiwa kifungo cha nje siku 60 katika Mahakama ya Jiji la Copenhagen kwa kutoa wito wa ukombozi wa Palestina. Jaji anayeendesha kesi aliamua wakati wa kutoa hukumu kwamba hotuba yangu ya 2021 katika suala hilo haikuelekezwa kwa Mayahudi kama kundi la kidini, lakini alitoa wito wa kuondolewa kwa umbile haramu la Kizayuni linaloitwa “Israel” kupitia uingiliaji wa kijeshi. Wito huu ulitangazwa na mahakama ya jiji kuwa sio halali!

Soma zaidi...

Mashirika ya Leo ya Vyombo vya Habari si Chochote isipokuwa ni Chombo cha Dola Ovu za Kilimwengu

Ingawa vyombo vya habari vinaitwa “nguzo ya nne ya demokrasia,” vikionyesha kutoegemea upande wowote na fikra yake, kama mamlaka ya mahakama kwa mfano, uhalifu uliofanywa na serikali ya Kiyahudi huko Gaza, na katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, ulitosha kufichua madai haya. Uhalifu huo ulifichua ukweli kuhusu vyombo vya habari na wanahabari. Jinai hizo zilionyesha wazi kwamba hakuna mamlaka ya kimaadili au uhalali, bali kwa ajili ya nguvu ya unyama, inayowakilishwa na dola za kimataifa na silaha zao duniani, ikiwemo Ulimwengu wa Kiislamu, ikiwa ni pamoja na watawala, serikali, na taasisi za vyombo vya habari.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu