Vichwa vya Habari 23/11/2022
- Imepeperushwa katika Vichwa vya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
China imefunga moja ya mikataba mikubwa zaidi ya gesi asilia majimaji (LNG) pamoja na Qatar yenye thamani ya dolari bilioni 60, Shirika la Habari la Qatar lilitangaza. Mkataba huo wa kihistoria na nchi yenye uchumi wa pili kwa ukubwa duniani unatazamiwa kuimarisha usalama wa kawi wa Beijing kwa miongo kadhaa na ni mapinduzi makubwa kwa China huku nchi zikikimbilia kufunga mikataba ya kawi kutokana na uhaba unaosababishwa na vita vya Urusi na Ukraine.