Nini Kinachotofautisha Uteuzi wa bin Mubarak kutoka kwa bin Abdul Malik katika Serikali ya Aden?!
- Imepeperushwa katika Yemen
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo tarehe 6/2/2024, uamuzi ulitolewa na Baraza la Rais mjini Aden kumteua Ahmed Awad bin Mubarak kuwa Waziri Mkuu wa serikali ya Aden, akimrithi Maeen Abdul Malik. Uteuzi wa Ahmed bin Mubarak umekuja baada ya Baraza la Rais kufeli katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wake kuafikiana juu ya idadi ya wagombea wa nafasi ya uwaziri.